facebook likes

Thursday, August 8, 2013

TAHADHARI: FEDHA NI HATARI KWA AFYA YAKO

RIPOTI ya Wiki imegundua kuwa, fedha ni hatari kwa afya ya binadamu kwani huweza kusababisha madhara makubwa.
Katika uchunguzi, ilibainika kuwa fedha za noti na zile za sarafu huweza kukusanya na kusambaza vimelea vya magonjwa hatari kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

.....SOMA ZAIDI....


Kuhakikisha ukweli wa jambo hilo, Ripoti ya Wiki ilifanya mahojiano na mtaalam wa magonjwa mbalimbali, Dk. Richard Marise na kusema kuwa tafiti mbalimbali duniani zimeripoti kuhusu vimelea vinavyoweza kusafirishwa kupitia fedha ambavyo ni Staphylococcus Aureus, Escherichiacoli,Fecal Bacteria na sumu nyingine.
“Tafiti nyingi zilizofanywa katika nchi zilizoendelea, zimegundua kuwa vimelea hatarishi kwenye fedha hasa za noti ambapo vingi hutokana na uchafu utokao kwa mwanadamu mwenyewe kwa mfano; kinyesi, mkojo na jasho.
“Vimelea hivyo kwa pamoja husababisha magonjwa kama boils (magonjwa ya ngozi) pneumonia, toxic shock syndrome (homa za sumu mwilini), diarrhea (kuharisha), gum diseases (magonjwa ya fizi), homa za vipindi na meningitis (uvumbi wa bongo) ambao kama hakuna matibabu huweza kusababisha kifo,” alisema Dk. Richard.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...