facebook likes

Saturday, July 27, 2013

WAHITIMU WA VYUO VIKUU NCHINI SASA KUKOPESHWA FEDHA ZA KUANZISHA MIRADI ILI KUKABILIANA NA CHANGAMOTO YA UKOSEFU WA AJIRA...!!

 

WASOMI watakaohitimu vyuo vya elimu ya juu nchini kuanzia mwaka huu watakopeshwa mabilioni ya fedha ili waanzishe miradi itakayowawezesha kujiajiri. Hatua hiyo ni matokeo ya Programu ya Wizara ya Kazi na Ajira inayolenga kukuza ajira kwa vijana wahitimu wa vyuo hivyo, kwa kushirikiana na vya elimu ya juu, taasisi za fedha na wabia wa maendeleo.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Msemaji wa Wizara hiyo, Ridhiwani Wema alisema, Sh bilioni 54 zitahitajika kufanikisha miradi 1,000 itakayotekelezwa kwa awamu tatu kwa miaka mitatu ya utekelezaji. Kwa mujibu wa Wema, kati ya fedha hizo, Sh bilioni 4.4 ni za mafunzo na kuandaa vijana ili wakopesheke na Sh bilioni 50 zitakuwa dhamana.


"Lengo la kuanzisha programu hii ni kuongeza fursa za ajira 30,000 za moja kwa moja kwa wasomi hao kwa kipindi hicho. Tunaamini miradi watakayoanzisha itafanya wajiajiri na kuajiri wengine.

"Katika kuhakikisha programu hii inafanikiwa, Serikali imekubaliana na Benki ya CRDB kutoa mikopo kwa vijana, mara utekelezaji utakapoanza rasmi. Utaanza kwa kuendeleza programu ya mfano iliyoanzishwa na Idara ya Kilimo, Uchumi na Biashara katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA)," Wema alisema.

Alisema, baada ya hapo, wahitimu wa vyuo vingine vya elimu ya juu nao watafikiwa na kuandaliwa vizuri kwa mafunzo ili wawe wajasiriamali kupitia miradi watakayoianzisha kwa kutumia mikopo watakayopewa. Wema alifafanua kuwa wahusika watalazimika kuandika mapendekezo ya miradi yao ambayo yataangaliwa na kupangiwa kiasi cha fedha, ili waweze kukopeshwa tayari kwa kuanza kuitekeleza.

"Miradi itakayoanzishwa itatoa mnyororo mzima wa thamani, kwa mfano mradi wa alizeti na ukamuaji mafuta. Tumejiridhisha kuwa miradi hiyo itapunguza wimbi la vijana kukimbilia mijini, kwa sababu itakuwa ikitekelezwa katika maeneo watakakokuwa wahitimu hao ambayo si ya mjini pekee," alisema.

Wema alifafanua kuwa katika awamu ya kwanza vijana 600 kutoka SUA watahusika kumiliki miradi 200 ya kujiajiri na kuajiri wahitimu wengine 5,400, wakati katika awamu ya pili, vijana 900 kutoka vyuo vingine wataanzisha miradi 300. Kwa maelezo yake, awamu ya tatu itahusisha wahitimu 1,500 wa vyuo vingine ikiwamo VETA itakayokuwa na miradi 500 itakayozalisha ajira 13,500.

"Hivyo ndivyo tutakavyotumia programu hii kupunguza tatizo la ajira na kuhakikisha wanaoandika mapendekezo yenye ushawishi na yanayoelezea miradi inayotekelezeka watakopeshwa," alisema na kuongeza kuwa muda utakapofika, wahitimu wataandikishwa na kutambuliwa kupitia mikoa na wilaya wanamoishi.

Watapeliwa ajira Wakati mikakati ya ajira ikiwekwa ili kukomboa vijana wasomi nchini, Jeshi la Polisi Dodoma linamshikilia Mariam Tawakali (28) akidaiwa kutapeli wahitimu wa vyuo vikuu kwa ahadi ya kuwapa kazi ya kuandikisha wananchi wanaotarajiwa kupewa vitambulisho vya uraia chini ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Hayo yalithibitishwa jana na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, David Misime akisema Mariam alikamatwa juzi katika Barabara ya Sita, Dodoma, baada ya Polisi kupata taarifa kutoka kwa raia wema.

Alisema mtuhumiwa alikutwa na vitambulisho vitano vyenye majina tofauti ya Mariam Tawakali na Monica Emmanuel Ngaso (28), mkazi wa Nkuhungu, Dodoma.

Miongoni mwa vitambulisho hivyo ni cha Mkutano Mkuu wa CCM, wa Novemba 11-13, mwaka jana ambapo kazi yake ilionesha kuwa ni mhudumu.

Kingine ni cha kampuni ya Thaker Singh Coast Action chenye jina la Monica Emmanuel Ngaso, kazi Katibu Muhtasi, nacho kitambulisho cha New Dodoma Hotel chenye jina la Mariam Tawakal kazi yake Katibu Muhtasi na cha Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima chenye jina la Mariam Tawakali, kikionesha ni mwalimu wa taasisi hiyo kijijini Chamwino.

Kamanda Misime alisema Mariam alitangazia wananchi, kwamba kazi ya kuandikisha vitambulisho vya uraia kwa Dodoma itaanza mwezi ujao.

Pia waliwaeleza kuwa atakayehitaji kazi hiyo awasilishe maombi kwake akiambatanisha vyeti vya elimu ya sekondari au chuo, picha za vitambulisho na fedha taslimu Sh 110,000 za kiingilio. Aidha, aliwaambia atakayepata nafasi atalipwa mshahara wa Sh 400,000 kwa mwezi kwa miezi mitatu ambapo kazi hiyo itakuwa imekamilika.

Alisema mtuhumiwa huyo alifanikiwa kukusanya vyeti, picha na fedha kwa wananchi 29 wengi wao wakiwa wahitimu wa vyuo vikuu mwaka huu.

Kamanda Misime alisema Polisi inatoa hadhari kwa wananchi kuwa makini na wanaofanya vitendo hivyo na kuwataka kutoa taarifa mapema wanapotilia shaka watu wa aina hiyo ili hatua za kuwadhibiti zichukuliwe mapema.

Alitaka wananchi kuelewa kuwapo matapeli wanaobuni miradi ya kujipatia fedha kwa udanganyifu na kuwataka kuchukua hadhari mapema kwa kukataa kurubuniwa ajira na kutoa fedha bila kuthibitisha.

Alisema Polisi inafuatilia kuona uhalali wa vyeti vya wanafunzi hao wa vyuo vikuu na kuona ni kosa gani Mariam atashitakiwa nalo. Pia alitaka waliotapeliwa kufika Polisi kutoa ushahidi kabla ya kesi haijafikishwa mahakamani.

Liverpool yakaribia kuuzwa.


Kikosi cha Liverpool .

Kikosi cha Liverpool .
Siku chache baada ya kukaribia kumuuza nyota wake Luis Suarez wamiliki wa klabu ya Liverpool ambao ni kampuni ya Fenway Sports Group wako mbioni kuiuza klabu hiyo.
Kampuni hiyo yenye maskani yake huko Boston nchini Marekani ambayo inaongozwa na mfanyabiashara John W Henry iliinunua klabu ya Liverpool toka kwa wafanyabiashara George Gillett na Tom Hicks huku wakiwa na mtazamo wa kibiashara wa kutengeneza fedha kupitia klabu hiyo jambo ambalo halijatokea katika kipindi cha miaka minne ya umiliki wao.
John W Henry aliinunua Liverpool kwa paundi milioni 300 na anataka kuiuza kwa paundi milioni 350. Kwa mujibu wa taarifa toka benki moja ya huko Marekani klabu hiyo imewekwa sokoni kwa mtu yoyote atakayekuwa tayari kuinunua .
Henry anaonekana kuchoshwa na kitendo cha kutotimia kwa malengo ya kibiashara aliyokuwa ameiwekea Liverpool ambapo katika kipindi cha miaka minne klabu hiyo bado imeshindwa kushiriki ligi ya mabingwa na haijaweza kuwa na ubora wa kuwania ubngwa wa ligi ya England .
image
Pamoja na hayo Liverpool pia imekuwa ikipata hasara kwenye soko la wachezaji ambapo mara kadhaa imekuwa ikishindwa kurudisha thamani ya fedha zinazotumika kwenye matokeo uwanjani na hata kwenye mauzo ya wachezaji . Moja ya hasara kubwa ambazo zimemkera mmiliki John W Henry ni kitendo cha kununuliwa kwa Andy Caroll kwa paundi milioni 35 kabla ya kumuuza kwa paundi milioni 19 huku akiwa hajawahi kufanya vizuri kulingana na thamani ya fedha iliyotumika kumsajili.
Uongozi wa Fenway Sports Group ulikutana na kampuni ya mafuta ya Saudi Aramco ya huko Saudi Arabia kujadiliana uwezekano wa kampuni hiyo ya mafuta kuidhamini Liverpool lakini vingozi wa Saudi walikuja na wazo la kuinunua kabisa klabu hiyo . Hadi sasa kampuni mbili zinazomilikiwa na mabilionea wa kimarekani zimeripotiwa kuwa na wazo la kununua Liverpool lakini hakujakuwa na ofa rasmi.

NAENDA : Fabregas ataka kutua Man United


  BARCELONA,HISPANIA
CESC Fabregas amenong’ona kwa rafiki zake. Amewaambia “Ninataka kucheza Manchester United, nataka kuungana tena na Robin Van Persie”.
Jina la kiungo huyo limekuwa likitamba katika vyombo vya habari nchini England na Hispania huku Manchester United ikikataliwa dau la Pauni 30 milioni kwa ajili ya kumpeleka Old Trafford.
Kocha wa United, David Moyes, aliwaambia waandishi wa habari juzi Alhamisi nchini Japan akisema mazungumzo ya kumchukua staa huyo wa zamani wa Arsenal, yanaendelea na hayajafa kama inavyofikiriwa.
Ukweli ni kwamba Fabregas amewaambia rafiki zake kuwa anataka kwenda England huku akiachana na Barcelona kwa mara nyingine tena baada ya kuachana nayo utotoni alipotimkia Arsenal.
Inasemekana Fabregas amefurahishwa na ahadi aliyopewa na Manchester United ya kucheza katika kikosi cha kwanza huku pia akifurahia kuungana tena na rafiki yake, Robin Van Persie.
Katika kikosi cha sasa cha Barcelona, Fabregas, hana uhakika wa namba ya kudumu. Ujio wa staa wa Brazil, Neymar, katika kikosi chao unaweza kumaliza kabisa matumaini yake ya  kupata nafasi kikosi hapo.
Fabregas pia anaamini kuwa anaweza kutwaa taji la Ligi Kuu England akiwa na United kama vile alivyotwaa taji la Ligi Kuu  Hispania msimu uliopita. Staa huyo alitwaa Kombe la FA na Ngao ya Jamii tu katika kipindi chote alichocheza Arsenal.
Barcelona bado imesisitiza kwamba staa huyo wa timu ya taifa ya Hispania hauzwi ingawa inaeleweka kwamba hatima yake itaamuliwa na kocha mpya, Gerrard ‘Tata’ Martino, aliyetua klabuni hapo mapema wiki hii akitokea Argentina.
Arsenal ingekuwa katika nafasi nzuri ya kumsajili staa huyo kutokana na kipengele cha mauzo yake kwenda Barcelona kuwapa fursa ya kuweza kumsajili kwa kiasi cha Pauni 25 milioni.
Lakini haionekani kama kocha, Arsene Wenger, ana hamu ya kumsajili staa huyo kutokana na utajiri alionao katika sehemu ya kiungo ambapo Jack Wilshere na Santi Cazorla wameikamata vema.

KILA LA KHERI TAIFA STARS USHINDI LEO LAZIMA


011-1
Wachezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Satrs’ ambao wanasakata kabumbu ndani ya nchi wakijifua katika Uwanja wa Taifa wa Mandela uliopo Nambale nchini Uganda. Stars ipo nchini Uganda na inatarajia kushuka katika dimba la uwanja huo kumenyana na The Cranes ya Uganda Jumamosi kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa Ndani CHAN kila la kheri Stars.Katika mchezo wa kwanza uliofanyika Daressalaam Stars walifungwa bao 1-0.
005-1
015-2
016-2

WAKAGUZI WA MAHESABU WAPONGEZWA NEW YORK MAREKANI


Na Joseph Msami wa Radio ya Umoja wa Mataifa
Mapema wiki hii wajumbe wa bodi ya ukaguzi wa Umoja wa Mataifa walikutana mjini New York Marekani ambapo pamoja na mambo mengine walitia saini ripoti za ukaguzi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa kwa mwaka wa fedha 2012. Miongoni mwa wajumbe hao ni Ludovick Uttouh, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali yaTanzania ambaye aliwakusanya wakaguzi wa mahesabu kutoka Tanzania na wafanyakazi kadhaa wa ubalozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa hapa New York kwa hafla wima (cocktail party).
Lengo la hafla hii ilokuwa kuwapongeza wakaguzi kwa kazi nzuri na pia kushukuru ubalozi kwa ushirikiano walioutoa.

Pichani kulia ni  mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali Ludovick Utoh akiongea  wakati wa hafla hiyo.Aliyeko naye hapo pembeni ni mwakilishi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Balozi Tuvako Manongi.

Chanzo:Swahili Tv

‘RAMA MLA WATU’ APELEKWA MIREMBE KWA UKICHAA

 Ramadhan Seleman ‘Rama Mla watu’, aliyekuwa akishikiliwa na dola kwa tuhuma za mauaji ya mtoto, Salome Yohana licha ya kuondolewa hatia hiyo huku akiwekwa chini ya uangalizi baada ya kubainika kuwa na matatizo ya akili, Jumatano iliyopita alirudishwa hospitali ya waalifu ya Isanga iliyopo Mirembe, Mkoani Dodoma. 
Rama alipandishwa basi ya Shukrani majira ya saa moja asubuhi akiwa na askari wawili waliokuwa wakimlinda kuhakikisha wanamfikisha kwenye hospitali hiyo, mpaka akili yake itakapotengemaa ndipo ataachiwa uraiani.
Kijana huyo alisafirishwa kupelekwa hospitalini huko kufuatia amri iliyotolewa na Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam katika kesi yake ya mauaji iliyokuwa ikiwakabili na mama yake, Khadija Musa, baada ya kubainika kuwa alitenda kosa hilo akiwa na matatizo ya akili.

DIAMOND PLATNUMZ IS IN KENYA ...DO YOU WANNA KNOW WHY?

Tanzanian bongo star Diamond jetted in last night through J.K.I.A. with his crew and at first it was not clear why he was in Kenya way before his Standard Group’s Diamond tour.

It has now been revealed that Diamond is in Kenya for a performance courtesy of Coca Cola in a planned major advertising drive for one of their brands.

Diamond is currently Coca Cola’s brand ambassador and thus his visit to Kenya. The deal with coca cola has seen him take home a brand new ride. 

source:The Kenyan Daily Post

INSPIRATIONAL SONG: Naeto C - Share My Blessings featuring Asa



LYRICS

Verse 1 (Naeto C)All white kaftan like the stripe on a tom tomSee how we got famous where we come fromwalahi it’s from teaspoons to lump sums – What a conundrum!All I did was make lines like when ABC bus comesNow they saying tread softly with cautionYou attract the wrong people when they know about your fortuneI’m worried maybe that’ll be my portion.I don’t need a new cut to feel level headedMy experience has justified where I’m headedSo when they talk about the things that I do wrongI just pat them on the back like a new bornCos as the rumor’s starts to spread like a bed sheetI’m calculating money on excel spread sheets.I’m too blessed to be stressedSo I’m giving out some love cos I’m getting it in excessNow that you should respect.
Pre-Hook (2x)It’s moving over meIt’s taking over meAnd I’m feeling my way up now.
Hook (2x)When heaven puts a hand on meCome and share my blessings.
Verse 2 (Naeto C)1st day of the yearmy best friend died in a car crash.Couple of months before that, I survived in a car crash.Now that’s the irony of lifeShe was good enough to be a wifeI only cry once a year but that year, I cried thrice.So dear friend, let me give you an adviceKeep your loved ones close cos they won’t live twiceI should have told her how I felt but I couldn’t be precise.I didn’t reply her emails even though she broke down her feelings in detail.I was busy dealing with all sorts of femaleNow it’s hard for me to even open up my gmailI wish she had the same luck as mebut that’s what i couldn’t give unluckily.And so I pray that my blessings extendto the rest of my family and friends.Pre-Hook (2x)It’s moving over meIt’s taking over meAnd I’m feeling my way up now.
Hook (2x)When heaven puts a hand on meCome and share my blessings.
Verse 3 (Asa)Gbogbo ohun tan fe…iyen lan fe f’omode ati awon agbaEh Iya miIreti miKoni dofoKoni daruLaiI’m moving onThis little light of mineI’m gonna let it shine (let it shine)Pre-Hook (2x)It’s moving over meIt’s taking over meAnd I’m feeling my way up now.
Hook (4x)When heaven puts a hand on meCome and share my blessings.la la la la la la la lala la la la lala la la la la la la (la)yes Boss!

MWANAMKE APEWA KICHAPO KIKALI BAADA YA KUZINI NA MCHUNGAJI WA KANISA JIJINI DAR



MWANAMKE anayejulikana kwa jina la Nabii Juliana wa Kanisa la Miracle Assemblies of God, amepigwa na wananchi wenye hasira kali baada ya kudaiwa kuingilia ndoa ya Mchungaji Richard Kiondo.


Tukio hilo la aina yake ambalo lilikusanya umati wa watu, lilitokea hivi karibuni maeneo ya Ukonga Mazizini, jijini Dar ambapo nabii huyo alipigwa hadi kuchaniwa nguo.

Akielezea mkasa huo, mtoto wa mchungaji wa kanisa hilo, Christina Kiondo alisema baba yake alikuwa akishirikiana kwa huduma ya kanisa na Nabii Juliana lakini katika ushirika huo anaamini wawili hao walikuwa na uhusiano usiofaa. 

Alisema kisa cha nabii huyo kupigwa, hivi karibuni mwanamke mmoja alikwenda nyumbani kwa Mchungaji Kiondo na kuwaeleza watoto hao kwamba anamdai baba yao shilingi 40,000, kitu ambacho kiliwashitua sana kwa kuwa baba yao anaishi kwa nabii na pia hawakujua fedha hizo alikopa kwa ajili ya familia gani.

Mtoto mkubwa wa mchungaji huyo, alimtuma mdogo wake nyumbani kwa nabii huyo kwa lengo la kwenda kumuita baba yao ili aje kuzungumza na mwanamke huyo.

Ilidaiwa kuwa, mtoto huyo alipofika alikutana na nabii na kumwambia amemfuata baba yake lakini alimfukuza.
 

“Baadaye alikuja hapa nyumbani na kuanzisha varangati kitu ambacho hakikukubalika kwa majirani kwani tangu siku nyingi wanajua uhusiano wake wa baba.
 

“Majirani walitoka kwa wingi baada ya kumsikia nabii akitufanyia fujo, walianza kumshushia kipigo mpaka alipokuja kuokolewa na mjumbe wa eneo hili na kupelekwa polisi,” alisema Christina.

Akizungumza na mwandishi wetu, mjumbe wa eneo hilo Joseph John ‘Mzee Kasheshe’ alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo alikiri kutokea kwa tukio hilo.

Kwa upande wake, mke halali wa mchungaji huo ambaye yuko Mbagala kwa matibabu, alisema alizipata taarifa za nabii huyo kupigwa.

Aliongeza kuwa tangu zamani mama huyo alikuwa akienda na mumewe nyumbani hapo akidhani kuwa wote ni watumishi wa Mungu hivyo hakuwahi kuwatilia shaka hadi baadaye sana aliponyetishiwa na watu. 

Kufuatia kipigo hicho, Nabii Juliana alipofika polisi alitoa malalamiko yake na kufungua kesi yenye kumbukumbu: MAZ/RB/2246/2013 KUHARIBU MALI. 


source-GPL 

HAYA NDO MAJIBU YA RAIS MUGABE KWA RAIS OBAMA JUU YA NDOA YA JINSIA MOJA



RAIS WA ZIMBABWE MUGABE KAMCHANA OBAMA,KASEMA HIVIII "Then we have this
American president,Obama, born of an African father, who is saying we will not give you aid if you
don’t embrace homoséxuality," Mugabe said. "We ask, was he born out of homosexuality? We need
continuity in our race, and  that comes from the  woman, and no to  homoséxuality. John and
John, no. Maria and Maria, no."

Eviction Show: Namibia’s Sunny Boy To Perform

sunny boy namibia 62















This Sunday on the live Eviction show, Namibia’s Sunny Boy is expected to perform on the Big Brother Africa stage. Talking about the young talented dude, he always had a dream of making good music that would touch the hearts of many as he grew up.
Sunny boy has now been in the game for almost ten years and with this time, he has managed to do four albums and he has actually created his own unique Hikwa style a mix of tight Kwaito beats with a Hip Hop flow from from genres like Kwaito and Hip Hop led. He has done killer hits like Balance, Serious, Summertime and Heat It Up among others.
The talented Namibian lad has also won awards like the NBC Music Award and Namibia Music Awards and lent his fame to greater causes, like the Namibia Red Cross Society and Special Olympics Namibia.
Sunny boy’s voice pattern, flow and rhyme delivery are compared to that of Nas who is highly praised as one of Hip Hop’s greatest poets. He also mentions South African kwaito artists, Brickz and Brown Dash as his influences.
Annabel, Elikem and Sulu are up for possible eviction this week. Please vote for your favourite housemate to keep them in the Game.

RAIS KIKWETE ATOA WIKI MBILI KWA MAJAMBAZI KUSALIMISHA SILAHA-LA SIVYO KUSAKWA POPOTE

AKIONGEA KWA UJASIRI akiwa ngara:ametoa wiki mbili kwa majambazi kusalimisha silaha na kujisalimisha. "NIMECHOKA"tutafanya operation kubwa ambayo haijawahi kutokea KAGERA,GEITA NA KIGOMA kwa kuvishirikisha vyombo vyote vya ulinzi mnavyovijua, akivitaja, JWTZ, POLISI NA USALAMA WA TAIFA.

Ametahadhalisha kuwa wageni waanze kuondoka wenyewe na kurudi nchini kwao, "tutawasaka majumbani kwao, misituni, walikochimbia silaha zao na risasi" - TAYARI NIMESHAWASILIANA NA VIKOSI VYOTE VYA ULINZI"


Source:Chanel Ten.

Ukatili gani huu-Mama abanika mikono ya mwanae motoni


Mtoto Bryton Evarist (9) mkazi wa Temeke, Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, amejeruhiwa vibaya baada ya kuunguzwa mikono kwa kubanikwa kwenye jiko la mkaa na mama yake mzazi.
Mwanamke aliyefanya unyama huo ni Asa Barnaba (24), ambapo inadaiwa baada ya tukio hilo alimfungia ndani kwa muda wa wiki mmoja na kumlazimisha kula na kuoga kwa kutumia mikono aliyomuunguza.
Tukio hilo linadaiwa kufanywa wiki tatu zilizopita majira ya usiku, baada ya mtoto huyo kudaiwa kula samaki wa kitoweo.
Akisimulia mkasa huo akiwa Hopitali ya Temeke, mtoto huyo ambaye ni mwanafunzi wa darasa la tatu Shule ya Msingi Kibasila, alisema mama yake alichukua hatua hiyo baada ya kukasirishwa na kitendo hicho.Kusoma zaidi bofya
Alisema siku ya tukio, alirudi nyumbani mapema akitokea shuleni, alipofika nyumbani kwao alikuta chakula pamoja na mboga mbili aina ya maharage na samaki.
Bila ya kutambua kwamba samaki hao waliwekwa kwa ajili ya kitoweo cha usiku, aliamua kula na kuyaacha maharage.
“Mama aliporudi na kukuta nimekula samaki, aliniuliza kwa nini nimekula, lakini nilikataa kwa kuogopa kupigwa,” alisema.
Hata hivyo, baada ya kubanwa sana, mtoto huyo aliamua kukubali kula ndipo mama yake alipochukua jiko la mkaa lenye moto na kumuweka mikono yake juu ya moto uliokuwa unawaka.
“Alichukua mikono yangu na kuniweka kwenye jiko, nilihisi maumivu makali sana,” alisema.


SIRI YABAINIKA
Akiongea na NIPASHE Jumamosi, Afisa Ustawi wa Jamii wa Manispaa ya Temeke, Sharifa Ally, alisema mtoto huyo aligundulika kufanyiwa unyama huo baada ya wiki moja akiwa katika hali mbaya.
Alisema aligundulika baada ya kutoroka na kwenda kuomba msaada kwa wapita njia ili wamsaidie kumpeleka hospitali.

“Inashangaza sana kuona mama mzazi akiwa na moyo wa kikatili, muda wote alikuwa akienda kazini na kumuacha mtoto wake ndani akioza mikono,” alisema Sharifa.
Sharifa, alisema hatua hiyo ilisaidia mtoto huyo kupelekwa kituo cha Polisi cha Chang’ombe na kisha kufikishwa Hospitali ya Temeke.
“Akiwa hospitalini, sisi Ustawi wa Jamii na Jeshi la Polisi tulisimamia kwa karibu matibabu yake pamoja kuangalia namna na kumfungulia kesi mhusika,” alisema.

MAMA AKIRI
Mama wa mtoto huyo alipoulizwa sababu ya kufanya kitendo hicho, alisema aliamua kumchoma moto mtoto wake baada ya kuchoshwa na tabia yake ya wizi kwa muda mrefu.
“Huyu mtoto ana tabia ya wizi, mwanzo alikuwa akiniibia hela ndani, nilimuonya sana na wakati mwingine nilimpiga lakini hakusikia, ndipo alipokula mboga niliamua kumchoma moto ili asirudie,” alisema Asa.
Hata hivyo, alisema anajutia kufanya tukio hilo na hakufikiria kwamba mtoto wake angepata majeraha kama aliyonayo kwa sasa.
Baba wa mtoto huyo aliyejitambulisha kwa jina moja la Evarist akiongea kwa simu kutoka mkoani Kigoma, alisema bado hajapata taarifa ya tukio hilo na alionyesha kusikitishwa kwake.
“Aisee! sijapata kabisa taarifa ya jambo hilo, nasikitika sana,” alisema na kukata simu.
Alipotafutwa Kamanda wa Mkoa wa Polisi wa Temeke, Engelbert Kiondo kwa njia ya simu, hakupatikana baada ya mtu aliyepokea kueleza yupo nje kikazi.

CHANZO: NIPASHE

MKULIMA AUWA WANAWE WAWILI HUKO KIGOMA.....BANGI YATAJWA KUWA CHANZO...!!

JESHI la Polisi mkoani Kigoma linamshikilia mkulima mkazi wa kijiji cha Mvugwe, Kasulu, Thobias Majuto kwa kuua watoto wawili kwa makusudi. Akizungumza na gazeti hili mjini hapa juzi Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Fraiser Kashai alisema mkulima huyo inadaiwa alifanya mauaji hayo Jumatano saa mbili asubuhi nyumbani kwake

Akieleza tukio hilo, Kamanda Kashai alisema mtuhumiwa alimchukua mtoto wake mkubwa, Loyce Majuto (2) na kumchoma kisu kifuani na kukishindilia hadi alipokata roho. Kama vile haitoshi alimchukua mtoto mwingine mwenye umri wa miezi mitatu ambaye hakuwa amepewa jina na kumbamiza chini mara tatu hadi kufa.

Wakati akifanya vitendo hivyo mkewe alikuwa nje akipika na baada ya kusikia vilio alikimbilia ndani kujua kulikoni, ndipo akakuta mtuhumiwa amefanya unyama huo wa kutisha. Kutokana na mauaji hayo mwanamke alipiga yowe na umati wa watu kijijini hapo kujitokeza na kumkamata mtuhumiwa na kumpiga na baadaye kumfikisha Polisi Makere.

Kamanda alisema sababu kuu ya vitendo hivyo ni matumizi ya dawa za kulevya aina ya bangi kwa muda mrefu na hivi sasa anashikiliwa Polisi wilaya ya Kasulu wakati upelelezi wa shauri hilo ukiendelea.

Mauaji Sumbawanga, Habari kutoka Sumbawanga, zinasema Polisi inashikilia wanandoa kwa tuhuma za kusababisha kifo cha mtoto wao wa kike mwenye umri wa miaka miwili wakati wanapigana kwa kilichoelezwa ni wivu wa kimapenzi.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda jana akizungumzia tukio hilo alisema lililotokea saa 5:30 usiku wa kuamkia Julai 22, baada ya wanandoa hao Livinus Choma (31) na Grace Choma (28), wakazi wa Malangali mjini hapa, kurejea nyumbani wakiwa wamelewa.

Alisema baada ya kurejea nyumbani wakitoka katika kilabu cha pombe za kienyeji, ulizuka ugomvi kutokana na mke kumtuhumu mumewe kuwa na uhusiano kimapenzi na wanawake wengine hali iliyomkera mume na kupigana.

Ilielezwa kuwa wakiwa wanapigana, mume alimsukuma mkewe, akamwangukia mtoto wao huyo aitwaye Esther na kupoteza fahamu, hali iliyochanganya wazazi wakiamini amekufa.

Kwa mujibu wa Kamanda Mwaruanda, wanandoa hao walimchukua mtoto huyo katika hali hiyo na kwenda kumtelekeza katika nyumba jirani wakiamini amekufa, kisha wakapiga simu kwa Diwani wa Kata hiyo wakidai kuwa mtoto wao amepotea katika mazingira ya kutatanisha.

Diwani Anthony Choma wa Kata ya Malangali, aliuarifu uongozi wa Serikali ya Mtaa na kwa pamoja walishirikiana na wazazi hao kumtafuta mtoto huyo na kumkuta hana fahamu pembeni mwa nyumba ya jirani yao.

Kwa mujibu wa Diwani Choma, ili kunusuru maisha ya mtoto huyo, walimkimbiza katika hospitali ya mkoa mjini hapa, lakini alifariki dunia muda mfupi baada ya kuanza matibabu. Kamanda Mwaruanda alisema mama wa mtoto huyo alipohojiwa Polisi, alikiri wao kuwa chanzo cha kifo hicho.

Pia alikiri kumtelekeza karibu na nyumba ya jirani ili isijulikane kuwa wao ni wahusika, na kutaka ijulikane kuwa jirani yao ndiye aliyemwiba na kumwua.

Alisema baada ya uchunguzi wa awali kukamilika, wanandoa hao watafikishwa mahakamani ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.

Imeandikwa na Fadhil Abdallah, Kigoma na Peti Siyame, Sumbawanga.

SOURCE: HABARI LEO

Jayz sneaks up behind a surprised Beyonce and gives her a kiss during her Concert (PHOTOS)


Jay Z surprised his wife on stage when she was performing in Philadelphia as part of her Mrs Carter World Tour.The rapper snuck up behind Beyoncé and then threw his arms und her and gave her a sweet smooch.


The crowd erupted in cheers..How sweeeeeeet. See more photos below: 


KIUNGO WA AZAM HUMPHREY MIENO ATAJWA KWENDA KUZIBA NAFASI YA WANYAMA CELTIC





Victor Wanyama ameondoka Celtic Football Club na kujiunga na klabu inayoshiriki kwenye ligi kuu ya England - Southampto baada ya kukamilisha uhamisho wa wa £12.5million. Sasa ikiwa ni wiki kadhaa tangu kiungo huyo wa Kenya kuondoka, kocha wa Celtic Neil Lennon, amesema Wanyama alikuwa ndio kiungo wake bora wa ushambuliaji kwenye timu yake na sasa wanahitaji mbadala wake.
Kutokana na hilo sasa zimeibuka taarifa kwamba kocha huyo ambaye ni nahodha wa zamani wa Celtic anamuwania kiungo mwingine kutoka Kenya Humphrey Mieno. Mieno ambaye kwa sasa ni mchezaji wa Azam FC  inayoshiriki kwenye ligi kuu ya Tanzania.
Celtic, itabidi ifanye haraka kumsaini mchezaji huyo wa Azam FC kwa kuwa kuna vilabu vingi barani Afrika kama miamba ya soka ya Tunisia Esperance na Club Africain zinamuwania kwa nguvu mchezaji huyo ambaye alihamia Azam akitokea Sofapaka ya Kenya.
Mpaka sasa sio Celtic wala Azam FC ambazo zimethibitisha kuhusu taarifa hizi.

Harvard Falls To 8th On Forbes’ Top Colleges List, What’s Number 1?

If you’re entering college, you want to go to the best institution you possibly can. If this is the case, what’s the first school that comes to mind? 
More than likely, your answer is “Harvard University.” The Ivy League school is historically known as one of the greatest schools in the world.

According to Forbes, however, it is only the eigth best school in the nation.


In its list of America’s Top Colleges 2013, Forbes ranks Harvard University right behind the United States Military Academy at West Point, New York.

With the cost of a four-year undergraduate degree approaching a quarter million dollars, there’s no surprise people are doing what they can to find the best institution possible.


So what school tops the list? According to Forbes, Stanford University in California reigns supreme. Stanford was followed by another Californian school, Pomoma College.


Many other familiar names made the list, while another small college, Swarthmore College, was awarded the sixth spot.


Did your school make the list? Check out the top 10 below!


Stanford University

Pomona College
Princeton University
Yale University
Columbia University
Swarthmore College
United States Military Academy
Harvard University
Williams College
Massachusetts Institute of Technology

DJ KHALED PROPOSES TO NICKI MINAJ ON MTV WITH $500,000 DIAMOND RING [VIDEO].


DJ Khaled is all about unity. When he drops his seventh album, Suffering From Success, on September 24, he will no doubt bring together rap's top names for a collection of all-star tracks, but lately Khaled is looking for another type of union.

On Thursday (July 25), the charismatic hitmaker proposed to his YMCMB labelmate Nicki Minaj in front of  MTV News cameras. "Nicki Minaj, I'm at MTV, I'am going to be honest with you; I love you," Khaled said to camera, speaking directly to Pink Friday MC. "I like you, I want you, I want you to be mine."

Khaled had a lot to get off of his chest, first telling Nicki how he feels about her, before he popped the big question: "Nicki Minaj, will you marry me?"

The We the Best CEO was clear and direct with his message. In fact Khaled is so serious that he went to MTV studio with a 10 karat radiant cut diamond ring from Rafaello & Co. in Manhattan's famed diamond district. The ring is valued at about $500,000.

"We got the same symptoms, we're both suffering from success," he said, noting Minaj's hectic schedule which includes live shows, recording sessions and filming "The Other Woman" alongside actress Cameron Diaz. "[If] you gotta take your time and think about it, I overstand, but I know I have to be here today to let you know how serious I am and how serious this is to me."

So what's it going to be Nicki?

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...