facebook likes

Tuesday, July 23, 2013

Chris Brown na Drake kuungana kwa mara ya kwanza tangu ugomvi wao



20130214-chris-x600-1360873933

Chris Brown na Drake sio marafiki kabisa na wamekuwa na ugomvi kwa muda mrefu sana. Hivi sasa kuna kitu kimoja cha msingi ambacho kitawafanya waungane na kusahau tofati zao. Baada ya ugomvi uliotokea kwenye club moja ya usiku huko New York ambapo uliwahusisha Chris Brown na Drake na mwisho wa siku watu kadhaa walipata majeraha hasa Chris Brown aliumia sehemu ya kidevu na bodyguard wake kupasuka kichwani.
Hivi sasa wamiliki wa club hiyo wamewafungulia mashataka mahakamani Chris Brown pamoja na Drake na kuwataka wawalipe dola millioni 16 kama fidia baada ya kusababisha hasara na kuharibu jina la eneo hilo. Sababu hii ndiyo pekee itawaunganisha Chris Brown na Drake ili waweze kuyakabili mashataka haya. Labda mawakili wa Chris Brown na Drake wanaweza kukutana na kuongea wenyewe kwa niaba ya wateja wao au wao wenyewe kukutana.
519545b6b5fc11e1bf341231380f8a12_7
Chris Browm alipoumia baada ya ugomvi ndani ya club
chris-brown-drake-fight-club-WIP
Hii ni sehemu ya ndani ya club baada ya ugomvi kutokea
Chris-Browns-bodyguard
Body guard wake Chris Brown baada ya kupata majeraha siku ya ugomvi mwaka jana

HII NDIO KAULI YA SINTAH BAADA YA KUTISHIWA MAISHA NA SHILOLE

















Akiongea kwa njia ya simu toka nyumbani kwake Sintah baada ya mtandao huu kutaka kueleza anachukuliaje vitosho hivyo vya Shilole ambapo alisema" Kaka naambiwa sana na watu hasa wanaofatilia mitandao eti natafutwa kupigwa na Shilole sasa ninacho shangaa huyo Shilole anapafahamu kwangu aje basi anipige au kwenye ofisi zangu anapajua namkaribisha vizuri sana jamani" Alisema Sintah

 

Aidha Sintah aliongeza kusema kuwa" Mimi huwa sio mtu wa maneno yeye aje tu anipige na sio kutangaza kwenye mitandao kuwa ananitafuta anipige hayo mambo ya bifu siku hizi watu wanayachukulia upuuzi kutafuta pesa ndio mpango mzima hivyo mimi namshauri Shilole kama underground wa sanaa nchini aachane na bifu badala yake akazane kwenye mambo yake ya kutafuta pesa kwa ajili ya maisha yake na familia kwani uzee unakuja" Alisema Sintah
Chanzo cha ugomvi huo ulitokana na Sintah kuandika habari kwenye mtandao wake kuwa Shilole hawezi kuimba na Jennifer Lopez wa Marekani bora hata Linah wa THT anaweza kufanya hivyo kwa hiyo Shilole aache kuidanganya jamii. Mtandao wa Sintah uliandika hivyo
Aidha Mashabiki mbalimbali hasa wasomaji wa kwenye mitandao wamemuunga mkono Sintah kuhusu kauri yake" Ni kweli jamani Shilole hawezi kuimba na Jennifer Lopez hayo ni masihara jamani kwenda marekani ndio aje kuongea ulojo kiasi hicho kwanza ikumbukwe kuwa wasanii wote wa tanzania kule Marekani hawajulikani hata, hasa kwa sisi tunaofatilia tunajia" Alisema mfanyabiasha wa kimataifa aliyejitambulishia kwa jina la Hamu Juma

ROSE NDAUKA AKANUSHA HABARI ZILIZO SAMBAA KUWA NI MJA MZITO


Mwanadada Rose ndauka amekanusha habari zilizoandikwa jana kwenye mitandao mbalimbali nchini kuwa huenda yu mjamzito kutokana na tukio la kuugua ghafla na kupandwa na kichefuchefu alipokuwa location akitengeneza Filamu yake mpya (kama nayoonekana pichani)
Akizungumza na mtandao wa Swahili World Planet, Rose ndauka amesema kuwa habari hizo si za kweli na wala yeye hajaongea jambo kama hilo
 "sio kweli na kilichoandikwa sijakiongea" hata sijui wamepata wapi hizo taarifa. Alinukuliwa akisema Rose ndauka

BANDARI YA MOMBASA KENYA WAMEFUNGUA OFFICE KIGALI-MWAYKEMBE SISI TUMEJIPANGAJE


Kufuatia kikao cha triple K (Kenyatta, Kagame na Kaguta (Mseveni)) kilichofanyika Kampala mwezi uliopita, jana bandari ya Mombasa wamefungua rasmi ofisi yao Kigali kwa ajili ya kuhudumia nchi za Rwanda, Burundi na DRC. Moja ya mambo waliyokubaliana triple K ni kuondoa matatizo yote yanayofanya biashara baina ya nchi hizi kuwa ngumu.
Sote tunafahamu mahusiano mabovu yaliyopo kati ya Rais Kikwete na Rais Kagame kwa sasa. Ni ukweli usiopingika kwamba kwa sasa Bandari ndio cash cow ya Tanzania, hakuna cha kilimo, madini, utalii au chochote utakachotaja. Kama kumbukumbu zangu bado ziko poa, bandari inaingiza over 50 bil kwa mwezi. Swali ninalojiuliza, hivi tumejipangaje ili kuwa competitive zaidi in case nchi hizi nne kwa maana ya DRC, Burundi, Rwanda na Uganda zitaamua kwa kiasi kikubwa kuanza kutumia bandari ya Mombasa? Think of hayo mapato niliyotaja, ajira, biashara za mafuta, hotel n.k.


BBA UPDATES:NANDO NA DILLISH WAONDOA TOFAUTI ZAO BAADA YA NANDO KUTANGAZA KUWA DILLISH ALIMSHIKA SEHEMU NYETI


Uh-oh is Dillish and Nando's friendship on the rocks? The two former Diamonds spent a good portion of the night airing out their differences.
From the looks of things, today's comical court session had some not so funny consequences. The Namibian was not impressed by Nando sharing in front of everyone that she had jokingly touched his penis.
She felt that he was being inappropriate talking about things that are real during a joking court session. "You come in the shower and touch my boob and I laugh because it is just a joke. I didn't go around sharing that with everyone," said Dillish.
The Namibian told her buddy that the reason that their friendship has changed is because she doesn't know if she can just joke around with him anymore without knowing if he will take things personally. She said: "That's why I only want to chill with Melvin, because I know that he will just laugh about things".
Meanwhile Nando said that he was not happy with Dillish assuming that he takes things personally without asking him. "I hate when you make me feel like sh*t," said the Tanzanian.
In the end, the two both agreed that they still like being friends and they went back to their playful ways; laughing and joking with one another.

TID"SIO KWELI KWAMBA NYIMBO ZA ALI KIBA ZINAPENDWA MUSCAT OMAN, MIMI NDIO NAPENDWA ZAIDI HUKO"

Khalid Mohamed, Top In Dar (T.I.D) ambae pia ni mmiliki wa Top Band amepinga vikali taarifa zinazoonesha kuwa Nyimbo za msanii mwenzake Ali Kiba zinasikilizwa zaidi Muscat huenda kuliko msanii mwingine wa Bongo Fleva.

Taarifa hizi zilizotolewa na mtandao wa Bongo5 ambao ulipata maelezo ya kina baada ya kuchat na mtanzania aishie nchini Muscat aliyetambulika kwa jina la Rayya Al Habsi aliyewapa tathmini kuhusu nyimbo za kibongo zinazosikilizwa zaidi huko mjini Muscat,Oman.

Rayya alisema nyimbo za Ali Kiba zinasikilizwa sana lakini pia wasanii wengine wanaopendwa ni Diamond Platinumz, Ommy Dimpoz na Dully Sykes.

Rayya aitaja pia upande wa mduara kuwa ni AT, Off side Trick na Kilimanjaro Band, na kwamba band inayofunika zaidi ni Twanga Pepeta.

Taarifa hizi zinakuja wakati ambapo T.I.D amepata deal la kwenda mjini Muscat kupiga show akiwa na band yake ‘Top Band’, na hivyo ameona kama taarifa hizi zimepotoshwa na yeye ndiye alistahili kutajwa katika nafasi aliyopewa ‘Ali Kiba.’ Na kwamba yeye ameshapiga show mara mbili na anaenda kwa mara ya tatu akiwa na band yake.

Kupitia ukurasa wake wa facebook T.I.D a.k.a Mnyama amedondosha  maelezo confidently.

“This came after I have been mentioned perfoming well its too late for this reminder its my time,and they listen to me alot its my third time perfomin there and this time with my band.”

Kisha akaambatanisha na kichwa cha habari chenye picha ya Ali Kiba kama kilivyoandikwa na Bongo5, yenye kichwa cha habari “Nyimbo za Ali Kiba zinasikilizwa zaidi Muscat ‘huenda’ kuliko msanii mwingine wa Bongo Flava.”
Well, yale yanaweza kuwa ni maoni ya Rayya, maoni sio utafiti rasmi japo unatoa picha ya jumla. Lakini inaonekana kama Top In Dar hataki kuwa Down any where hivi hivi.

Wanawake waliovaa pensi hadharani kwa mara ya kwanza.

Hii ni picha inayowaonyesha wanawake waliothubutu kuvaa kaptula kwa mara ya kwanza nchini Canada, unaambiwa walisababisha ajali ya barabarani kutokana na jinsi ambavyo walivuta hisia za watu ambao hawakuweza kujizuia kuwakodolea macho wakiacha kufanya shughuli zao.
Hii ilitokea huko Toronto mwaka 1937.
image

Umeshawahi kuona picha ya Marais wanne wote wa Kenya ndani ya chumba kimoja?



image
Hakuna yoyote aliyetarajia kushuhudia picha hii ikiwa na historia zilizofanana kwa wote waliojitokeza ndani yake .
Upande wa kushoto ni rais wa kwanza wa Kenya Mzee Jomo Kenyatta akifatiwa na mtoto wake amba,e wakati huo alikuwa mdogo sana kiumri Uhuru Muigai Kenyatta ambaye ndiye rais wa sasa wa Kenya….  aliyeinama kidogo ni Rais wa tatu wa Kenya Emilio Mwai Kibaki ambaye wakati huo alikuwa na wadhifa mkubwa kwenye serikali ya Mzee Kenyatta na hivi karibuni yeye (kibaki) ndio aliyemkabidhi Uhuru Kenyatta madaraka baada ya kuongoza kama rais wa tatu wa Kenya na aliyesimama ni Rais wa pili wa Kenya Daniel Toroitich Arap Moi .
Marais Wote hawa ndani ya picha moja, haijawahi kutokea,

Breaking News!!!! Malkia Elizabeth apata kitukuu.


Wazazi wapya..Prince William na Mkewe Kate Middleton.
Wazazi wapya..Prince William na Mkewe Kate Middleton.

Kate Middleton na msaidizi wake wakati anafanya shopping ya mtoto wake.
Kate Middleton na msaidizi wake wakati anafanya shopping ya mtoto wake.
Mke wa mjukuu wa Malkia wa Uingereza Kate Middleton amejifungua mtoto wake wa kwanza ikiwa imepita miezi zaidi ya 12 tangu alipoolewa rasmi kwenye familia ya kifalme.
Middleton na Mumewe ambaye ni mjukuu mkubwa wa malkia Elizabeth Prince Williams wameeleze furaha yao baada ya kupata mtoto huyo ambaye moja kwa moja anaingia kwenye kizazi cha Ufalme ambapo anakuwa mrithi wa tatu wa kiti cha Ufalme baada ya babu yake ambaye Prince ni Prince Charles na baba yake Prince William ambaye atarithi toka kwa Prince Charles.
Kate Middleton ambaye wadhifa wake rasmi ni “Duchess of Cambridge” alijifungua mtoto huyo kwenye hospitali ya St Marrys iliyoko eneo la Paddington . Hospitali hiyo ndipo alipoazaliwa baba mzazi wa mtoto huyo na Mume wa Katte Middleton ambaye ni mjukuu wa Malikia Elizabeth Prince Williams akizaliwa na Marehemu Princess Diana mwaka 1982.
Kate Middleton akifanyiwa vipimo vya nguo wakati alipokuwa mja mzito.
Kate Middleton akifanyiwa vipimo vya nguo wakati alipokuwa mja mzito.
Taarifa za kuzaliwa kwa mtoto huyo zimepokewa kwa furaha na wanasiasa mbalimbali duniani ambapo waziri mkuu wa Uingereza David Cameroon na Rais wa Marekani Barack Obama wameongoza orodhanya watu mashuhuri waliotuma salamu za pongezi kwa mtoto huyu mpya kwenye faimilia ya Malkia Elizabeth.

Video: Interview ya Hasheem Thabeet ndani ya kituo cha Television cha Kenya



ulikua unajua kuwa Hasheem Thabeet ni mchezaji bascket mrefu kuliko wachezaji wote wa NBA? kama ulikuwa hujui hilo basi Chukua hiyooo!!!!!!!!!.
Hasheem Thabeet akifanyiwa mahojiano na  kipindi cha television cha "The Trend" kupitia NTV ya kenya


Kelly Rowland aokolewa baada ya kupotea baharini kwa masaa 12

Wasamwahi huwa tunasema "maneno huumba", nikiangalia hii story inayomuhusu Kelly Rowland kuokolewa baharini, nakubaliana kabisa pale nikiifikia video ya wimbo wa Destinys Child "Survivor" ambayo kuna kipande kinamuonyesha Kelly akiwa katikati ya bahari huku akiwa hajui pa kuelekea.
 In reality hii imetokea  kwa Kelly siku ya Ijumaa ambapo aliokolewa baada ya kukaa baharini na kutokujua wapi pa kuelekea kwa masaa 12.
Rowland na wengine nusu dazeni walikuwa kwenye chombo cha baharini kwaajili ya kwenda kujionea  nyangumi  (Ijumaa asubuhi) wakiangalia kujiingiza katika nyangumi, lakini ghafla walikutana na wimbi lenye urefu wa futi 5 na kusababisha ukungu, hatimae kuwapotezea muelekeo.
Nahodha wa meli akawa dhaifu na hajiwezi kutokana na hali hiyo, hata hivyo Master wa bandari alifanikiwa kupiga mahesabu yake na kufanikiwa kurudisha meli hiyo .
Nahodha Nuhu Santos alifawaokoa kila mmoja na kuwarudisha mida ya saa 5 ya Ijumaa usiku huku kila mmoja akiwa anatetemeka kivyaake.
Santos anasema siku ya pili yake, alipokea shukran binafsi kutoka kwa Rowland mwenyewe alipokutana nae  akiwa na mkewe out kwa ajili ya dinner, na Kelly aliwalipia chakula walichokula. Mpaka dakika hii Kelly hajaongea lolote juu ya hilo.
Kelly akiwa na aliemuokoa

Picha: Quick Rocka (The Switcher) akiwa ndani ya studio zake mpya "Switcher Records"


Tuddy Thomas nae alipita kucheki vitu vipya ndani ya studio mpya ya Quick Rocka

Mark Zuckerberg alishawahi kuhisi 50 Cent amefanya kazi kwake (facebook)




50 Cents hajawahi kumaliza high school, lakini alishawahi kuaminiwa kuwa "mkuu wa maendeleo ya biashara  na mauzo" kupitia facebook 2005.

Wakati nafasi ya  mwanzilishi mwenza wa Facebook, Saverin Eduardo (mkuu wa maendeleo ya biashara  na mauzo) kuchukuliwa na Kevin Colleran, Zuckerberg alimchanganya kijana huyo na mega superstar 50 Cent kutokana na picha ya profile yake inayomuonyesha akiwa na 5o Cent.


Hivi ndivyo jinsi ilivyokuwa siku ya kwanza walipokutana Zuckerberg na Colleran uso kwa uso..

Zuckerberg alipanga kukutana na Colleran mbele ya Virgin  Megastore iliyopo New York Union Square, Colleran alifika akiwa amechelewa na hivyo kuelekea moja kwa  moja alipo Zuckerberg huku akipokea simu kutoka kwa huyo huyo Zukerberg akimuuliza "Uko wapi", Colleran akamjibu nimpo mbele yako. Zuck alimuangalia kwa mshangao sana, alidhani muuza matangazo ya facebook ni yule jamaa aliekuwa akionekana  mweusi na tafu sana kwenye profile picture (50 Cents)

Rais wa Facebook na mwanzilishi wa Napster, Sean Parker alimwambia Colleran kuwa mkutano na Zuckerberg ulikuwa wired sana sababu "sisi tulidhani ungekuwa African-American."

Wakati wa mkutano wao, 50 Cent alikuwa tayari kashauzwa rekodi zaidi ya milioni 8 na album yake ya kwanza Get Rich Or Die Trying, na moja ya single zilizofanikiwa sana kwenye radio kwa muda wote  "In Da Club" na alikuwa kashasainiwa Dr Dre na Eminem.

"WAGANGA MSITOE DAWA KWA MAJAMBAZI ILI TUSIWAKAMATE....TUPENI DAWA SISI ILI TUWAKAMATE"


Inaripotiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Polisi katika wilaya ya Mufindi, PCD Ambwene Manyasi amewataka waganga wa jadi kuacha mara moja kuwapatia majambazi dawa za kutokukamatwa na polisi, na badala yake waganga hao wawapatie askari polisi dawa za kuwaona na kuwakamata wahalifu.

Eliasa Ally wa gazeti la Majira anaripoti kutoka Mufindi kuwa kauli na wito huo umetolewa na OCD huyo katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mufindi, wakati akizungumza na waganga wa jadi na tiba asilia kutoka Mudindi.

OCD amesema ni jukumu la kila mwananchi kuuchukia uhalifu na kulisaidia jeshi la polisi kutimiza wajibu wake. Amenukuliwa akisema ifuatavyo:

"Ninyi waganga wa jadi na tiba asili kazi yenu kubwa ni kutibu magonjwa yanayowasibu watu na siyo kutibu mbinu za majambazi ili wasiwe wanakamatwa wanapofanya uhalifu, hapo tutakuwa hatusaidiani, badala ya waganja kuwa wachonganishi, wawe waunganishaji wa wananchi, polisi na jamii. 


"Badala ya kutoa dawa ya sisi polisi tusiwaone wala tusiwamamate majambazi, sasa nyinyi waganja mtoe dawa ya kutuwezesha kuwaona na kuwakamata kiurahisi majambazi wanaofanya uhalifu katika jamii yetu, huo ndiyo ushirikiano na polisi jamii tunayoizungumzia."

Aliwataka waganga hao kuhakikisha kuwa shughuli zao haziwi chanzo cha kutokea kwa maovu, kufumbia macho maovu na kusababisha jamii iwachukie waganga na polisi.

OCD alisema Jeshi la Polisi limejikita katika mambo makubwa matatu ambayo aliyataja kuwa ni polisi jamii, hali ya weledi na hali ya usasa.

NAY WA MITEGO ASHANGAA KUONA WASHINDI WA BSS WAKIFULIA LICHA YA KULIPWA PESA ZA KUTOSHA


 Hit maker wa Muziki Gani, Nay Wa Mitego ametuma salamu kwa mwandaaji ya shindano la Bongo Star Search, Rita Paulsen kuhusu zawadi wanayopewa washindi wa shindano hilo ambayo huwa haiwafikishi popote.
 
“Hizi Salamu ziende kwa Madam Rita na bongo star search. Mshindi analipwa nini mbona kama magumashi?! Namuona Walter Chilambo kapigika km zamani, haji ramadhani kachoka yupo kitaani. 

"Nauliza milioni hamsini zao anazila nani, acheni ubabaishaji wekeni mambo hadharani. #966#, salam zao# my new track,” aliandika Nay Wa Mitego kupitia Instagram.

VIJANA WAUANA JIJINI MBEYA WAKIGOMBANIA PENZI LA MSICHANA



Mnamo tarehe 21/07/2012 majira ya saa 23:30hrs huko kijiji cha Nkwangu wilaya ya Chunya mkoa wa Mbeya, Seni s/o Sandu, miaka 20, Msukuma, mkulima na mkazi wa Nkwangu aliuawa kwa kupigwa fimbo kichwani na Tolo s/o Seko, miaka 20, Msukuma, mkulima na mkazi wa Nkwangu.
Chanzo ni ugomvi wa kumgombania msichana aitwaye Holo d/o Kulwa, miaka 16, Msukuma mkulima na mkazi wa Nkwangu.


Mtuhumiwa amekamatwa na taratibu za kumfikisha mahakamani zinaandaliwa.


Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya kamishna msaidizi wa polisi diwani athumani anatoa wito kwa jamii kutojichukulia sheria mkononi kwani ni kinyume cha sheria na kudhibiti hasira zao kwa kuyatatua matatizo ya kimapenzi kwa njia ya mazungumzo ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza.

Signed by, [Diwani Athumani – ACP] kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya. 

Source:Watemi

TIMU ZA NIGERIA ZILIZOVUNJA REKODI YA KUFUNGANA MABAO MENGI ZAFUNGIWA MIAKA 10 - WACHEZAJI, VIONGOZI NA MAREFA WOTE WALA VIFUNGO VYA MAISHA



Wachezaji na maofisa wa timu zilizohusika katika mechi mtoano ambazo ziliishia kwa matokeo ya 79-0 and 67-0 wamefungiwa kifungo cha maisha cha soka.
Plateau United Feeders walishinda 79-0 dhidi ya Akurba FC wakati Police Machine FC waliwafumua Bubayaro FC 67-0.
Klabu hizo nne zimefungiwa kwa miaka 10.
Shirikisho la soka la Nigeria (NFF) kupitia kamati yake ya nidhamu pia limetoa ushauri kwamba marefa waliohusika na michezo hiyo miwili inabidi wafungiwe maisha. 
Plateau United Feeders na Police Machine walienda kucheza mechi zao wakiwa sawa kwa pointi, na hivyo walikuwa wakigombania nafasi ya kupanda daraja.
Feeders ilifunga mabao 72 ya mabao yao katika kipindi cha pili, wakati Police Machine waliripotiwa kufunga mabao 61 baada ya mapumziko ya mchezo. 
Matokeo hayo yalimaanisha kwamba Plateau iliwazidi Police Machine kwa tofauti ya mabao.
NFF ilisema kupitia taarifa yake: "NFF wamekubali mapendekezo yaliyotolewa na watawasiliana na klabu, vyama vya soka vya kanda husika, CAF na FIFA.
"Tutatoa kwa kuchapisha majina ya wachezaji wote pamoja na maofisa kwa pamoja na picha zao na taarifa."

SKENDO: VYETI VYA SHULE YA MSINGI VYAONYESHA RADAMEL FALCAO NI MKUBWA ZAIDI ANAYOSEMA MWENYEWE

Profile ya Falcao inayonyesha na umri wa miaka 27 wakati ni 29.


Wakati masuala ya wachezaji wa soka kufoji vyeti vya kuzaliwa kuficha umri wao halisi ukiwa umewaandama wachezaji wa kiafrika, leo hii zimeibuka ripoti kutoka Amerika ya Kusini zikiripoti kwamba mshambuliaji wa kikorombia Radamel Falcao amefoji umri wake.

Kwa mujibu wa vyeti vyake vya shule ya msingi vinaonyesha nyota huyo wa Monaco amezaliwa mwaka 1984 na sio 1986 kama inavyoonekana kwenye wasifu wake. Falcao alianza kusoma kwenye shule ya msingi ya Colegio San Pedro Claver iliyopo kwenye mji wa Bucaramanga akiwa na miaka mitano mnamo mwaka 1989. 

Kwa maana hiyo Falcao amejipunguzia umri wa miaka 2 katika umri wake wa halisi ambao ni miaka 29 mpaka sasa. Tangu kuanza kusambaa kwa taarifa hizi sio mwenyewe mchezaji wala wakala wake ambaye ajitokeza hadharani na kukanusha.

Cheti cha shule ya Colegio San Pedro Claver kikiwa picha ya Radamel Falcao Garcia aliokuwa mtoto


Cheti cha shule ya msingi cha Bucaramanga

HII NDIYO NYARAKA NYETI YA CCM ILIYONASWA NA CHADEMA


 
Chama cha Demokdrasia na Maendeleo (Chadema) kimesisitiza kuwa kitasimamia azimio la kikao cha Kamati Kuu yake kuhusu kuimarisha kitengo chake cha ulinzi na usalama na kuibua nyaraka ‘nyeti’ za Chama Cha Mapinduzi (CCM) zinazoweka hadharani mikakati ya CCM kufundisha vijana kukabiliana na wapinzani.
Pia kimemtaka Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuachia madaraka kama amechoka kuendelea kuwa kiongozi anayepaswa kusimamia misingi ya uongozi bora, ikiwamo kufuata haki za binadamu, sheria na demokrasia kwa ajili ya ustawi wa jamii ya Watanzania. Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, aliyasema hayo wakati akihutubia mkutano wa hadhara, katika viwanja vya Mahakama ya Mwanzo, Nguzo Nane, mjini Shinyanga juzi.

Alisema ili kujilinda dhidi ya vitendo alivyodai wanafanyiwa na vijana wa Green Guards wanaotoka kikosi cha vijana wa CCM, Chadema itaendelea na mipango ya kuwapa vijana wake mafunzo ya ukakamavu.

Katika mkutano huo uliohudhuriwa na maelfu ya wakazi wa mji huo na vitongoji vyake, Mbowe alionyesha nyaraka mbili za CCM zinazoonyesha kuwa chama hicho kupitia wanachama wa Umoja wa Vijana (UVCCM), kimekuwa kikitoa mafunzo ya ukakamavu kwa vijana wake, huku nyaraka moja ikionyesha kuwa moja ya malengo ya mafunzo hayo ni kukabiliana na upinzani.

“Tunashambuliwa, watu wetu wanapigwa, wanateswa, wanatekwa na wengine kuuawa, kwa sababu tu wanataka mabadiliko na wanapenda Chadema,” alisema Mbowe na kuongeza:

“Majuzi mlisikia Waziri Mkuu, Pinda anasema wamechoka...sasa tunasema, Pinda  kama umechoka ondoka upishe ofisi ya umma hiyo, upishe kwenye ofisi ya watu kama umechoka. Maana kuchoka huko ni kuchoka kwa CCM. Pisheni ofisi siyo za kwenu hizo, ni za Watanzania.”

“Wananchi hapa mkononi nimeshika nyaraka mbili za CCM. Moja ni cheti cha kuhitimu mafunzo na nyingine hapa juu imeandikwa: ‘Sera za Msingi za CCM’. Sasa mi sitawasomea. Naomba aje hapa jukwaani mtu yeyote anayejua kusoma, awasomee mjue tunaposema CCM wamekuwa na kikundi kinachoshambulia, kupiga, kutesa, kuteka na hata kuua Watanzania wenzao eti tu kwa sababu wanaunga mkono Chadema, huwa tunamaanisha nini.”

Mmoja wa wananchi aliyehudhuria mkutano huo wa hadhara, ambao ulikuwa ni sehemu ya shughuli za ukamilishaji wa kuzindua Kanda ya Ziwa Mashariki (mikoa ya  Shinyanga, Simiyu na Mara), alipewa kabrasha kubwa lililoandikwa: “Sera za Msingi za CCM” na kusoma sehemu inayozungumzia majukumu ya jumuiya za chama hicho.

Kifungu cha 9.1 kinachozungumzia UVCCM kinasomeka kuwa:

‘Umoja wa vijana wa CCM unapaswa kuwajenga vijana katika itikadi, ukakamavu na mafunzo yatakayowafanya wajiamini, wawe vijana wenye ari ya kutimiza wajibu wao wakiwa walinzi wa wa chama, viongozi na wagombea wa CCM.’

‘Utaratibu wa kuandaa makambi ya vijana usimamiwe kwa dhati. Chama kiwe na mipango mizuri ya kutafuta na kuwateua wakufunzi watakaofaa kuwapatia vijana mwelekeo unaotakiwa ikiwa ni pamoja na elimu ya uchaguzi/uraia.’ 

‘Mafunzo ya makambi ya vijana, mbali ya kujifunza nyimbo za hamasa yatilie mkazo pia mafunzo ya ukakamavu kwa lengo la kukabiliana na vitendo vya kihuni vya baadhi ya vijana wa vyama vya upinzani,’ inasomeka sehemu ya kitabu hicho cha CCM. Mbowe pia alimwomba mtu huyo asome cheti cha mmoja wa wahitimu wa kile alichodai ni mafunzo ya makambi ya vijana wa CCM.

Cheti hicho kinaonyesha mhitimu alianza mafunzo Juni 27, 2009 na kumaliza Julai 4, 2009, Wilaya ya Dodoma mjini, kimesainiwa na watu wawili; mmoja mwenye jina la Jumanne Kitundu, akiwa ni Katibu wa UVCCM, Dodoma Mjini na mwingine, ni Robert Mwinje, Mwenyekiti wa Umoja huo Wilaya ya Dodoma Mjini.

Pia cheti hicho kinaonyesha mhusika (jina linahifadhiwa) alihitimu mafunzo ya kanuni ya UVCCM, wajibu wa vijana katika chama, ulinzi na usalama, ujasiriamali, ukakamavu, wajibu wa vijana katika uchaguzi, rushwa, Ukimwi, historia ya Tanu na ASP pamoja na maadili.

Katika mkutano huo, Mbowe aliwataka Watanzania kuacha kugombana kwa sababu ya vyama, badala yake wasumbuliwe na waunganishwe pamoja na matatizo yanayowakabili sasa, ambayo alidai yanasababishwa na uongozi mbovu wa CCM.

Alisema Chadema inajiandaa kusambaza ushahidi ilionao wenye tuhuma nzito dhidi ya CCM kushindwa kufanya siasa na kuongoza nchi, badala yake imekuwa ikishambulia, kupiga, kutesa, kuteka na hata kuua watu.

Ushahidi huo umewekwa kwenye kitabu kimoja ambacho kwa mujibu wa Mbowe, kitatolewa nakala nyingi, kinaonyesha matukio mbalimbali ya kisiasa ambayo wananchi wamepigwa, wameumizwa na wengine kuuawa katika shughuli za siasa, huku uchunguzi huru ukiwa haujawahi kufanyika kubaini wahusika wa matukio hayo na sheria kuchukua mkondo wake.

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha), John Heche, katika mkutano huo, aliifananisha kodi mpya ya kadi za simu kuwa ni zaidi ya iliyokuwa kodi ya kichwa ambayo ilifutwa.

KWA WALE WANAFUNZI AMBAO WANAPENDA KUCHEZA MPIRA, AZAM ACADEMY WAMETOA NAFASI YA MAJARIBIO.


image
Majaribio kwa Azam Academy sasa yatafanyika Agosti 6 kuanzia saa moja asubuhi. Wazazi na walezi tunashauriwa kuwagharamia watoto wetu nauli, chakula, malazi na vifaa vya michezo
Majaribio ni kwa siku moja tuu na tunahitaji wachezaji walio chini ya umri wa miaka 15…. kama mchezaji ana miaka chini 17 na ana kipaji cha hali ya juu sana pia atapewa kipaumbele

Baada ya mchakato na kama kijana atafuzu kujiunga na Azam Academy Mzazi/Mlezi atajaza fomu maalum kwa niaba ya kijana

Wachezaji mzingatie kuja na vielelezo vya umri wenu, (Cheti cha kumaliza elimu ya Msingi na Cheti cha kuzaliwa) kwa pamoja

Imetolewa na uongozi wa Azam Academy

image

Source: www.perfecttz.com

KOCHA WA STARS - 'UGANDA NI TIMU BORA AFRIKA MASHARIKI - ILA SAFARI HII KAZI WANAYO NDHIDI YA VIJANA WANGU'




Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen amesema kikosi chake kimejiandaa kuikabili Uganda kwenye mechi ya marudiano ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) itakayochezwa Jumamosi jijini Kampala.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza leo, Kim amesema tangu kikosi chake kimeingia kambini Julai 14 mwaka huu, wachezaji wamekuwa wakifanya vizuri kwenye mazoezi na wako tayari kwa ajili ya mechi hiyo.

“Uganda ni timu bora kwa ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati. Mechi itakuwa ngumu, tunaamini tunakwenda kufanya vizuri. Tayari tunayo mikakati kwa ajili ya mechi hiyo, tunakwenda kuikamilisha Kampala,” amesema Kim.

Hata hivyo, Kim amesema licha ya mwitikio mzuri wa wachezaji kwenye mazoezi lakini wanakabiliwa na changamoto ya wengi wa wachezaji kuwa wamefunga wakati wachezaji wanapokuwa kambini wanatakiwa kula, kunywa na kupumzika.

“Hiki ni kipindi kigumu kwa mpira wa miguu, na suala la kufunga ni la kiimani ambapo hatuwezi kuwazuia wachezaji kufunga. Karibu nusu ya wachezaji wanafunga, hii ni changamoto ambayo tunaiheshimu,” amesema Kim na kuongeza kuwa ni wazi kikosi chake cha kwanza kitakuwa na mabadiliko baada ya beki Shomari Kapombe kwenda kwenye majaribio nchini Uholanzi.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager inaondoka Mwanza kesho (Julai 24 mwaka huu) saa 7.25 mchana kwa ndege ya PrecisionAir na kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe saa 8.15 mchana.

Wachezaji waliomo kwenye msafara huo ni makipa Juma Kaseja, Mwadini Ali na Ali Mustafa. Mabeki ni Aggrey Morris, David Luhende, Erasto Nyoni, Kelvin Yondani, Nadir Haroub na Vincent Barnabas.

Viungo ni Amri Kiemba, Athuman Idd, Frank Domayo, Haruni Chanongo, Khamis Mcha, Mudhathir Yahya, Salum Abubakar na Simon Msuva. Washambuliaji ni John Boko, Juma Luizio na Mrisho Ngasa.

MJANE WA ASKARI ALIYEFIA DARFUR ATUPIWA VIRAGO NA NDUGU WA MAREHEMU

Kibaha/Tanga. Hata kabla ya maziko askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), waliouawa Darfur, Sudan hayajafanyika, mchumba wa mmoja wa wapiganaji hao, Amina Juma ameonja chungu nyingine baada ya kutimuliwa kwenye nyumba aliyokuwa akiishi na marehemu mwenza wake.

Amina ambaye inadaiwa kuwa alikuwa akiishi na Fortunatus Msofe aliyekuwa askari katika Kambi ya Msangani, 36KJ Pwani alisema jana: “Kumekuwa na mzozo wa hali ya juu na ndiyo maana tumeshindwa hata kufika Uwanja wa Ndege kuupokea mwili na hata kesho (leo) sidhani kama nitakwenda... kuna mtafaruku mkubwa wakifamilia.”

Baada ya kutimuliwa, Amina ambaye hawakuwahi kupata mtoto na marehemu Msofe, alilazimika kuondoka kwenye nyumba hiyo na kwenda Mlandizi kwa wazazi wake.

“Nimeishi na Msofe kwa miaka mitatu, akiwa kambini mimi niko hapa na wakati mwingine alikuwa analala huku... lakini leo wamenitimua,” alisema huku akilia. Habari zilizothibitishwa na baadhi ya waombolezaji waliokuwa nyumbani kwa marehemu Visiga, Kibaha zinasema baadhi ya wanandugu walimkana Amina siku chache baada ya kutangazwa vifo hivyo.

Ilidaiwa kwamba Amina alitimuliwa katika nyumba hiyo Ijumaa iliyopita, saa saba mchana baada ya ndugu watatu wa marehemu kufika hapo wakitokea Tanga. Walipofika inadaiwa kuwa walitangaza kusitishwa msiba huo katika nyumba hiyo na kutangaza kutomtambua mke huyo.

Watu hao waliwaeleza waombolezaji kuwa walitumwa na baba mzazi wa marehemu, Willbad Msofe kutoka Kange, Tanga kufika Kibaha kusitisha msiba uliokuwa ukiendelea nyumbani kwa mtoto wake huyo.

Inadaiwa pia kuwa katika msafara huo, alikuwapo mdogo wa marehemu ambaye aliwahi kuishi kwa miaka miwili na Amina hapo Visiga.

Ilidaiwa kuwa walipofika nyumbani hapo walionana na mfiwa, Amina na wazazi wake ambao pamoja na majirani na watu wengine wengi, walikuwa wakimfariji binti yao huyo.

Mmoja wa waombolezaji alisema baada ya salamu wanandugu hao walianza kuulizia mali za marehemu na walikuwa wakimuuliza Amina ambaye aliwaleza kila kitu kilipo na baada ya hapo ndipo walipomweleza kuwa wametumwa na baba wa marehemu kuwa watu hawatakiwi kuomboleza kwenye eneo hilo kwani msiba upo Tanga tu ambako ndiko iliko familia yake.

Alipoulizwa baba wa marehemu, Mzee Msofe alisema: “Mimi ndiye niliyeagiza nyumba ifungwe na ukweli ninamfahamu Amina, lakini simtambui kama mkewe kwa kuwa hawajafunga ndoa... Hata wewe si unayafahamu haya? Uchumba si ndoa na ukifunga ndoa ndipo unatambulika rasmi,” alisema.




Akiwa kwa wazazi wake Mlandizi jana, Amina alisema:

“Namwachia Mungu maana hayo yote nashangaa yanatokea wakati huu mume wangu ‘Fortu’ amekufa, mbona kipindi chote cha miaka mitatu iliyopita familia ya Tanga dada zake na mdogo wake tuliishi nao vizuri kwangu nilipokuwa na marehemu? Nimeishi na ndugu wote lakini hawakuwahi kuhoji, hata nilipokwenda na mume wangu Kange baba na mama Msofe nilikaa nao zaidi ya wiki na hawakunikana, ila nashangaa,” alisema na kulia kwa uchungu.

Akizungumzia kitendo hicho, baba yake Amina, Juma Juma alisema: “Nimeshangaa hizi taarifa. Tulikuwa tunajiandaa kupokea msiba wa mwanetu, lakini leo yanakuja mengine kwa kweli imetushangaza sana.”

“Nasubiri baada ya kumzika marehemu, nitazungumza nao... Kinachonishangaza ni kwamba walituandikia barua ya kumposa binti yangu na tukawajibu na gharama zilikuwa Sh1.2 milioni... Tutazungumza, ngoja hili lipite kwanza,” alisema mzee Juma.

Maisha ya Amina na ‘Fortu’

Akisimulia maisha yao, Amina alisema: “Tulianza kuishi Mbezi Luis mwaka 2010 katika nyumba ya kupanga na nikamshawishi tununue kiwanja na kwa kuwa mimi ni mwenyeji wa Kibaha, niliwatumia marafiki wa familia yangu Mlandizi wakatafutia eneo na mwaka 2011 tulipata na tukaanza ujenzi.

“Tukiwa Mbezi, tulianza kufyatua matofali kisha ujenzi ukaanza Visiga mwaka 2012 mwanzoni na Septemba mwaka huo tulihamia kwenye nyumba yetu na hapo ndiyo ilikuwa makazi yetu hadi marehemu anaondoka kwenda Darfur.

“Wakati wote huo ‘Fortu’ alikuwa keshaniposa na hata barua zote za posa zipo na tulikuwa tukisubiri utaratibu wa kijeshi marehemu kukamilisha miaka sita ya kukaa kambini kisheria ndipo aruhusiwe kuoa.

“Fortu alikamilisha miaka hiyo mwaka 2012 mwishoni na wakati akijiandaa kwa kufunga ndoa ndipo ikatokea safari ya Darfur mwanzoni mwa mwaka huu na tukakubaliana tusitishe kwanza akirudi tukamilishe, lakini haikuwa.... Halafu wananifukuza wanasema hawanijui,” alieleza huku akiangua kilio.

CHANZO : MWANANCHI

HUYU NDIO KOCHA MPYA WA FC BARCELONA - SOMA WASIFU WAKE NA MAFANIKIO YAKE KAMA KOCHA NA MCHEZAJI


FC Barcelona imefikia makubaliano rasmi kumsaini Gerardo Martino kuwa kocha mkuu wa timu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili, kwa mujibu wa mtandao rasmi wa FC Barcelona.
  
Kilichobakia kwenye makubaliano hayo ni kusaini mkataba baada pande zote mbili kukubalina kila kitu.

Ratiba rasmi ya kuwasili kwake Nou Camp, utiaji saini wa mkataba na kutambulishwa rasmi itatangazwa msaa kadha yajayo. 

Gerardo ambaye anajulikana kama ‘Tata’, alizaliwa jijini Rosario (Argentina) November 20, 1962. Ana uzoefu mkubwa wa soka la America ya Kusini, kwanza kama mchezaji na baada kama kocha, kazi yake ya mwisho ilikuwa kuiongoza klabu ya Newell's Old Boys, ambao alishinda nao ubingwa wa mwaka huu.

Gerardo Martino anakuwa kocha wa nne raia wa Argentina kuifundisha FC Barcelona baada ya Roque Olsen, Helenio Herrera na César Luis Menotti.

WASIFU WA KOCHA GERARDO MARTINO TATA

FFU WAPATA AJALI, MMOJA AFARIKI, WAKIENDA KUTEMBEZA KICHAPO

Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wakiwa kazini. (Picha  kutoka Maktaba)

Askari mmoja wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Mkoani Kilimanjaro, Fidelis Mwaliyatabu, amefariki dunia papo hapo na wengine tisa akiwamo Mkuu wa Kikosi hicho kujeruhiwa vibaya baada ya gari lao kupinduka katika kijiji cha Kilingi, wilaya ya Siha, wakati wakienda kuzima vurugu za wananchi.
Ajali hiyo ilitokea wakati kikosi hicho kikielekea katika kijiji cha Karansi kwa ajili ya kukabiliana na wananchi waliokuwa wakiandamana kupinga wenzao waliokamatwa usiku wa manane baada ya kuvamia mashamba mali ya Shirika la Roho Mtakatifu-Kilasara.
Taarifa kutoka kijijini humo zilieleza kwamba wanakijiji waliamua kuandamana baada ya wenzao watano kukamatwa na Jeshi la Polisi nyakati za usiku kwa mahojiano kutokana na kukabiliwa na tuhuma za kushawishi wanakijiji wenzao kuvamia maeneo ya Shule ya Kilasara na kusababisha hasara kubwa kwa shule hiyo.
Kufuatia kukamatwa kwa watuhumiwa hao, wanakijiji waliamua kuandamana hadi katika kituo cha polisi ili kuwatoa wenzao hali ilisababisha jeshi hilo kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya, jambo ambalo lilishindikana kutokana na wingi wa watu walikuwa wanaandamana.
Inadaiwa kuwa wananchi hao walijikusanya na walianza kuandamana kuanzia majira ya saa 7 usiku kuelekea kituo cha polisi ili kuwatoa wenzao walikuwa wanashikiliwa.
Wananchi wanaoshikiliwa na jeshi hilo ni John Sokoine, Abeli Solomoni, Christopher Solomon na aliyetambuliwa kwa jina moja tu la Julius. Wote walikamatwa usiku wa kuamkia jana.
Mnamo Juni 11, mwaka huu majira ya mchana wananchi wa kijiji hicho walivamia eneo lenye ukubwa wa hekta mbili na kufyeka mazao mbalimbali yaliyokuwa shambani hapo kwa madai kuwa wamiliki wa shule hiyo wamechukua eneo hilo kinyume cha taratibu.
Kwa upande wake, Mkuu wa Shirika la Roho Mtakatifu, Kanda ya Afrika, Padri Jerome Okama, aliushutumu uongozi wa kijiji hicho kwa kuvifumbia macho vitendo vya wananchi kujichukulia sheria mkononi wakati wakitambua kuwa eneo hilo lenye ukubwa wa hekta 8.9 linamilikiwa na shirika hilo kihalali.
Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Robert Boaz, akizungumza na mwanahabari wetu kwa njia ya simu kutoka wilayani humo jana jioni, alisema askari hao walipata ajali hiyo majira ya saa 6.45 mchana katika kijiji cha Kilingi nje kidogo ya mji wa Sanya Juu.
Alisema askari hao wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC na wengine wamelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Ugonjwa wa Kifua Kikuu ya Kibong'oto ilioyopo wilayani Siha na kwamba watano kati yao hali zao ni mbaya.
Alitaja gari la Polisi lililopinduka na kuua kuwa ni Toyota Land Cruiser lenye namba PT 2070 lililokuwa likiendeshwa na Sajenti Herman Dancan. Chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi na kuacha njia na kupinduka.
Aliwataja waliojeruhiwa katika ajali hiyo kuwa ni Mkuu wa FFU mkoani hapa, ASP Nonino, Renatus Misigalo, Alfonce Joseph, Koplo Elifuraha Lenare, Peter Albert, Bashiri Yusuph, George Mwakyusa na Gaspar Mwapunda.
Alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Kibong'oto.

WAWEKEZAJI WA KICHINA NOMA-HADI KWENYE MAHINDI YA KUCHOMA MMHH




Mitaa ya Buguruni Mchina Akiuza Mahindi ya Kuchoma

HUYU NDO MTANZANIA MREFU KULIKO WOTE TANZANIA ANAMZIDI HATA HASHIMU THABITI


Huyu ni Baraka kijana mrefu  kitanzania


Inasemekana ni kijana mrefu kuliko wote Tanzania. Kijana huyu (katikati pichani) ambaye anadhaniwa ni mrefu kuliko vijana wote Tanzania anaishi maeneo ya Gongolamboto, Banana jijini Dar es salaam. Kijana huyu huwa haonekani sana mitaani, lakini aliingia mjini siku hiyo na kuleta kizaa zaa kikubwa pale alipoibuka mitaa ya Aggrey, Kariakoo. Alikuwa kivutio kwa kila aliyemuona, alifunga mtaa watu wakimshangaa na kumgombania kupiga nae picha. Kila aliyetaka kupiga nae picha alitoa Shilingi elfu moja Tsh. 1000.

Picha hiyo amepigwa ndani ya Kinyozi (Salon) aliyoingia kupunguza nywele zake na umati wa watu walikuwa nje ya kinyozi huyo kumsubiri atoke. Mpaka sasa hajajulikana jina lake kamili na anafanya nini. Inasemekana kuna watu wanamfuatilia kumsaidia umaarufu.

Hapa Hasheem Thabit alipokutana na Baraka
 
JULIUS CHARLES
UKIMUANGALIA kwa mara ya kwanza mchezaji wa Tanzania anayecheza timu ya kikapu ya Oklahoma City Sounders inayoshiriki Ligi ya Kikapu Marekani (NBA), Hasheem Thabit unaweza kujiridhisha kwamba ni mrefu kuliko Watanzania wote uliowahi kuwaona. Ana futi 7.3.
Lakini mjini Bagamoyo katika Mkoa wa Pwani kwenye shule ya Lord Barden yupo mchezaji anayemzidi Hasheem kwa urefu akiwa na futi 7.5. Si mwingine namzungumzia Julius Charles (18) ni maarufu zaidi maeneo ya Bagamoyo, na umaarufu huo umetokana na kimo chake huku wengi wakimuita mpinzani wa Hasheem Thabit  kutokana na urefu alionao ambao umepitiliza na ukikutana naye lazima utishike au ubaki ukimshangaa.

POLISI MKOANI MWANZA YAFAFANUA KWA KINA KUHUSU VIELELEZO VYA KESI VILIVYOIBIWA KITUONI HAPO



WATU wasiofahamika idadi yao wanaodhaniwa wezi, wameiba vielelezo katika stoo ndogo ya Kituo Kikuu cha Polisi Kati, Wilaya ya Nyamagana, mkoani Mwanza baada ya kuvunja madirisha.

Tukio la wizi huo lilifanyika Julai 15, mwaka huu, majira ya usiku wa kuamkia Jumatano katika jengo la Polisi Wilaya ya Nyamagana.

Akizungumza na gazeti la MAJIRA jana, Kamanda wa Polisi Mkoa Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Ernest Mangu, alisema wezi hao kabla ya kuingia ndani ya jengo hilo, walivunja dirisha la ofisi za Elimu, Ukaguzi Kanda ya Ziwa na walipofanikiwa kuingia ndani, walivunja dirisha na kuingia kwenye ofisi za Polisi Nyamagana na kutanua nondo kwa jeki na kisha kuingia kwenye stoo ndogo ambamo vielelezo hivyo vilitunzwa na kuiba begi moja la nguo na kompyuta mbili mpakato.

Moja ya kompyuta hizo ni kielelezo katika kesi ya ujambazi ambayo mtuhumiwa alikamatwa nayo, ambaye kwa sasa yuko mahabusu katika Gereza Kuu la Butimba.

Kamanda Mangu alisema kompyuta ya pili ni kielelezo cha kesi ya uharibifu wa mali inayomkabili fundi mmoja na begi la nguo ambazo mwenye nazo hafahamiki.


Begi hilo liliokotwa na polisi baada ya kuwakurupusha wezi hao waliokimbia na kulitelekeza.

Alieleza kuwa eneo walikopitia wezi hao usalama wake ni mdogo kwani ni uchochoroni na hakuna ulinzi wala mwanga wa taa, hivyo wanajaribu kuangalia kuboresha usalama wa hapo na maeneo jirani.

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...