facebook likes

Saturday, July 6, 2013

Piga kura hapa kumuokoa Nando asitoke kwenye jumba la Big Brother The Chase.

Nando
Nando mmoja ya wawakilishi wa Tanzania kwenye jumba la Big brother the chase, wiki hii amekuwa nominated kwenye group la watu ambao wanaoweza kutoka kwenye jumba hilo. Mtu wangu wa nguvu una nguvu na nafasi kubwa ya kumuokoa Nando abakie kwenye jumba lile na aendelee kuiwakilia 254 vizuri. Hapahapa unaposoma hii story bonyeza HAPA na utaweza kupiga kura moja kwa moja na utamuokoa Nando wiki hii na pia kama ni bahati yako unaweza kushinda zawadi kutoka DSTV.

Usajili unaomiliki Headlines NBA !

imageMchezaji wa Los Angeles Lakers Dwight Howard hatimaye amefikia maamuzi ya timu atakayoichezea baada ya kuwa kwenye hali ya utata kwa muda mrefu . Howard ameamua kujiunga na Houston Rockets ambayo ilikuwa moja ya timu tano zilizokuwa zinataka kumsajili.
Howard alijiunga na Lakers akitokea Orlando Magic msimu uliopita ambapo alicheza Lakers kwa mkataba mfupi huku akiwa na uchaguzi wa kusajiliwa na timu nyingine kwa muda mrefu .
Los Angeles Lakers walimtumia nyota wake Kobe Bryant kumshawishi Howard kubakia na Lakers lakini mchezaji huyo alivutiwa na Houston Rockets ambayo ilimuahidi kusajili wachezaji wengine nyota ambao wataipa timu hiyo nafasi ya kuwania ubingwa.
Timu nyingine zilizokuwa zinamsaka Dwight Howard ni Dallas Mavericks,Golden State Warriors na Brooklyn Nets .
Howard amesaini mkataba wa miaka mitano na timu hiyo ambapo ataungana na nyota wengine kama Jeremy Lin na James Harden huku Wakitarajia kumuongeza Josh Smith toka Atlanta Hawks kuongeza nguvu.

Picha za Mtanzania @Wakazi akiwa Airport Dar kuelekea South Afrika kufanya show BBA kesho @BigBroAfrica

.
.
Rapper Mtanzania Wakazi ambae ndio amechaguliwa na Multichoice kwenda kufanya show kwenye stage ya shindano la Big Brother Africa 2013 Johannesburg South Africa jumapili July 7, tayari ameondoka Dar es salaam Tanzania saa tisa kasoro alasiri.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

SH. 500/- SASA ITAKUWA SARAFU BADALA YA NOTI ILI KUIFANYA ISICHAKAE HARAKA



KUTOKANA na kuchakaa haraka kwa noti ya shilingi 500 na kiwango chake kudumu kwenye mzunguko kwa miezi sita tu, Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imesema inatarajia kubadili noti hiyo na kuwa ya sarafu.

Akizungumza na gazeti la Tanzania Daima juzi  kwenye viwanja vya maonesho ya kimataifa ya biashara, jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Fedha, Abdul Dollah, alisema mabadiliko hayo yatafanyika hivi karibuni na sarafu hiyo itadumu kwenye mzunguuko kwa zaidi ya miaka 20 huku ikiwa na ubora wake.

Dollah alitaja sababu nyingine ya uchakavu huo ni kutokana na noti hiyo kushikwa na watu wengi kwenye mzunguko huku baadhi yao wakishindwa kuzihifadhi vizuri: 


“Tofauti na noti nyingine kama vile zile za sh 5,000 na 10,000 hizi utakuta mara nyingi uchakavu wake si kama ule wa sh 500 kwa sababu noti hizi watumiaji wake wengi ni wale wenye akaunti benki.”

WAZIRI MAGUFULI ATAMANI KUWA RAIS WA TANZANIA......ANADAI KWAMBA YUPO TAYARI KUGOMBEA MWAKA 2015 ENDAPO ATAKIDHI MASHARTI


 Katika hali inayoonyesha kuwa Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, anautamani urais, amesema anaweza kutangaza nia hiyo kama atakidhi masharti yatakayowekwa kwenye Katiba mpya.

Alisema iwapo Katiba ijayo itakuja na sifa ambazo atakidhi vigezo kuna uwezekano mkubwa wa kuwania nafasi hiyo na kwamba iwapo atapungukiwa sifa zinazohitajika kwa mujibu wa Katiba hataingia kwenye kinyang’anyiro hicho.

Dk. Magufuli ambaye pia ni Mbunge wa Chato alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na wazee wa wilaya hiyo kwenye ukumbi wa ‘Mshikamano Saccos’, muda mfupi baada ya mzee Paschal Nyambibo (87) kumsihi agombee nafasi hiyo mwaka 2015 kutokana na sifa zake za uchapakazi ndani ya serikali.

Nyambibo alisema kutokana na uwajibikaji mzuri aliouonyesha Dk. Magufuli tangu mwaka 2000 akiwa Naibu Waziri wa Ujenzi na katika wizara mbalimbali, Watanzania wamekuwa na imani kubwa na uwajibikaji wake na kwamba anastahili kupeperusha bendera ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ifikapo mwaka 2015.

Licha ya kauli hiyo kusababisha minong’ono mingi kwa wazee waliohudhuria kikao hicho, Dk. Magufuli alionekana kutuliza hali hiyo kwa kusema isubiriwe Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano iwapo itakuwa na masharti ambayo yatamfanya kujitathimini iwapo ana sifa za kugombea au vinginevyo.

Hata hivyo, Dk. Magufuli hakusita kuonyesha hisia zake za kukerwa na baadhi ya wananchi wanaobeza maendeleo aliyotekeleza katika jimbo lake tangu alipochaguliwa kuwa Mbunge.

Alimshutumu hadharani aliyekuwa Katibu wa CCM wilaya ya Chato kabla ya kuhamishiwa wilayani Mbogwe, Gervas Stephano, kuwa hana shukrani.

Dk. Magufuli alimwelezea katibu huyo kuwa hana fadhila kutokana na mambo mengi aliyomtendea tangu akiwa katibu wa ofisi yake ya jimbo ambapo alimsaidia kupanda ngazi na kuwa Katibu wa CCM wilaya Chato, Kwimba, Kasulu, Kilosa na kurejea tena Chato kabla ya kuhamishiwa wilaya ya Mbogwe mkoani Geita  kuendelea na wadhifa huo.

“Tatizo lenu watu wa Chato hamna shukrani…mambo mengi nimefanya hapa Chato, lakini yote mnaona ziro…hata niliowasaidia kama Gervas naye sasa hivi ananiponda…lakini nawashukuru sana wazee wangu kwa kunikumbusha niliyoyafanya kwenye jimbo letu kupitia risala yenu nzuri,
” alisema Dk. Magufuli.

“Kutokana na hali hiyo ninawazawadia Sh. 1,000,000 mfanye sherehe ya kujipongeza kwa kuwa natambua mmejitesa sana mpaka kufanikisha kikao hiki cha leo…na kwa kuwa hamna mradi wowote wa kuwaingizia kipato kama wazee, ninaahidi kuwapa Sh.   3,000,000 kutoka mfuko wa jimbo, ili muanzishe walau saccos ya kukopeshana,” alisema.

Baadhi ya viongozi na wananchi wamekuwa wakilitaja mara kwa mara jina la Waziri Magufuli miongoni mwa watu wanaodhaniwa kutaka kugombea nafasi ya urais wa Tanzania mwaka 2015, ingawa mwenyewe amekuwa akikanusha uvumi huo.

Mbali na Dk. Magufuli, wengine ndani ya CCM wanaotajwa  ni pamoja na aliyekuwa Waziri Mkuu ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa; Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, ambaye anajiita mtaji wa urais; Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe; Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa Ushirikiano wa Kimataifa –CCM, Dk. Asha-Rose Migiro na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano na Mambo ya Nje, Bernard Membe, ambaye alipata kusema anasubiri kuiteshwa na Mungu kuwania nafasi hiyo.



Nipashe:

OFFICIAL DSTV BIG BROTHER PARTY AT NYUMBANI LOUNGE


DSTV pamoja na AIRTEL wanakuletea special Viewing party ya Big Brother Eviction Show Kila Jumapili ndani ya NYUMBANI LOUNGE kuanzia saa mbili usiku. Wiki hii Ndani ya Big Brother Rapper Mtanzania WAKAZI atatumbuiza.

MWANACHUO WA MWAKA WA KWANZA ALAANI KITENDO CHA KUPIGWA "EXILE" NA MADENTI WENZIE


Vitendo  vya  wanafunzi  kupigana  exile( kumpisha room ili angonoke na mpenzi wake)   vimekuwa  vikishika  kasi  ya  ajabu  katika  hosteli  za  wanafunzi  wa  vyuo  vikuu  mbalimbali ambao  kwao  limekuwa  ni  jambo  la  kawaida...!!

Hali  imekuwa  ni tofauti  kidogo  kwa  mwanafunzi  wa  chuo kimoja  hapa  nchini  ambaye  yuko  mwaka  wa  kwanza na anategemea kuingia mwaka wa pili.



Akiongea  na  mtandao  huu  kwa  sharti  la  kutotajwa  jina , mwanafunzi  huyo  amefunguka  na kudai  kuwa  Exile  imemuathiri  sana  kisaikolojia.Imemfanya  aishi  kama  mtumwa  huku  taaluma  yake  ikiyumba  kwa  kasi.

Hili  ni   simulizi  la  mwanafunzi  huyo:  
"Maisha ya shule yana changamoto  nyingi sana.Kwa  mtu  yeyote  ambaye  ni  mcha  mungu  ni  lazima  itamuwia  vigumu  sana  kukabiliana  na  hali hii.


"Nasema  hivi  kwa  sababu  ndani  ya  hosteli  huwa  tunaishi  watu   tofauti  wenye malezi  tofauti.Kasheshe  ni  kwetu  sisi  first  year...


"Mazingira  kwetu  ni  mageni  na  ndani  ya  hosteli  tunaishi  na  mabraza  wa  miaka  ya  juu  wenye  wapenzi  wao  hapo hapo chuoni ambao  huwaleta  vyumbani   na  wakati mwngine  hulala  nao.


"Wanapokuja  na  wapenzi  wao  vyumbani  ni  lazima  uwapishe  wafanye  mambo  yao.Na  ukiwapisha  maana  yake  utoke  kwa  zaidi  ya  masaa  matatu  mpaka   matano


"Ndani  ya  chumba  changu  tulikuwa  tunaishi  watatu, mmoja  mwaka  wa  pili, mwingine  wa  tatu  na  mimi  mwaka wa kwanza.Wote  hao  walikuwa  na  wapenzi  wao  hapo hapo  chuoni.


"Siku  zote  za  wikiendi  walikuwa  wamezigawana.Mmmoja  ilikuwa  ni  jumamosi  na  mwingine  jumapili.Yaani  kwa  kifupi  ni  kwamba  sikuwa  na  uhuru wa  kukaa  chumbani   siku za wikiendi  na  wakati  mwingine  hata  siku  za  wiki.


"Nimeamua  niwe  muwazi  maana hali  hii  imekuwa  ni  kero  kwangu   na  imekuwa  ikiniathiri  sana  kisaikilojia  na  kusababisha  taaluma  yangu  iyumbe  nikilinganisha  na  nilipokuwa  naanza.


"Naomba  nitoe  ombi  kwa  wanafunzi wenzangu.Sote  tuko  vyuoni  kutafuta  maisha  na  zile  hosteli  tunazilipia  kwa  gharama  sawa.Kwa  nini  umsumbue  mwenzako  wakati  gesti  zipo?..Yangu  ni  hayo  tu"



AJALI MBAYA YA BASI LA SUMMRY YAUA WATU TISA NA WENGINE KUJERUHIWA VIBAYA.




Basi la kampuni ya Sumry limetumbukia mtoni Iku na kuuwa watu tisa na kujeruhi wengine hamsini na tatu.


Ajali hiyo imetokea katika kijiji cha Sitalike wilaya ya Mlele mkoani Katavi
Tukio hilo la kusikitisha lilitokea saa sita usiku kuamkia Julai 5, 2013 basi hilo lilipokuwa likitokea mjini Sumbawanga kuelekea Mpanda mkoani Katavi likiwa na abiri waliokuwa wametoka Mbeya.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Katavi Emanuely Nnley alisema jana kuwa ajali hiyo ilihusisha basi aina ya Nissan Diesel lenye namba T909 AZT mali ya kampuni ya Sumry lililokuwa likiendesha na dereva aliyetajwa kwa jina na Stephano Chimane maarufu kwa  jina la Ntungu.


Alisema basi hilo lilipofika katika daraja hilo lenye kona kali na mteremko dereva wake alishindwa kulimudu na kulenga daraja hali iliyosababisha tairi za nyuma kupanda juu ya ukingo na kutumbukia mtoni ambapo dereva wa basi hilo aliweza kutoka na kukimbilia kusikojulikana 
Mkuu wa mkoa wa Katavi Dr Rajabu Rutengwe alitoa rambi rambi kwa wafiwa wote na kuwapa pole wahanga wa ajali hiyo mbaya kutokea tangu mkoa huo uanze.

HABARI KWA HISANI YA http://lukwangule.blogspot.com

PICHA ZA SIKU: MASHINDANO YA MAGARI YA GHARAMA YASIYO RASMI YA WACHEZAJI WA MAN UNITED: ANDERSON KIBOKO AINGIA MAZOEZINI NA GARI LA MILLION 286

MERC-URIAL TALENT ... Anderson turns up in his £168,395 SLS
    Anderson akiingia na gari yake aina ya Mercedez yenye thamani ya  £168,395 
Leo asubuhi wachezaji wa Manchester United walikuwa na mashindano yasiyo rasmi ya kuonyesha magari yao ya thamani wakati wakiwasili kwenye uwanja wao wa mazoezi AON Carrington. Mchezaji wa kibrazil Anderson pamoja na kutokuwa mmoja ya wachezaji wanaolipwa fedha nyingi sana na United - yeye ndio alikuwa mchezaji aliyekuja na gari la thamani zaidi Mercedez ambalo linauzwa kiasi cha millioni 286,271,500 za kitanzania.

Rio Ferdinand — Jaguar XJ Portfolio (£70,385)

Rio Ferdinand

Wayne Rooney — Range Rover Sport Autobiography (£84,895)

Rooney

Nemanja Vidic — Mercedes M Class (£47,385)

Vidic


Ryan Giggs — Range Rover Sport Autobiography (£98,395)

Giggs

Phil Neville — Porsche Cayenne (£86,895)

Neville

Rafael and Fabio da Silva — Chevrolet Captiva (£32,000)

Fabio & Rafael

Michael Carrick — Mercedes M Class (£47,386)

Carrick

Ashley Young — Range Rover Sport Autobiography (£68,995)

Young

Alex Buttner — Chevrolet Camaro Coupe (36,785)

Buttner

Msiba wa makeup Artist maarufu Nigeria

.

.
Makeup artist maarufu wa Nigeria Adenike maarufu kama ‘Ewar’ ambae alifanya hiyo kazi kwa miaka tisa, amefariki muda mfupi tu baada ya kujifungua mtoto wa kike Sagamu Nigeria.
Waliokaribu na familia yake wamesema matatizo yaliambatana na blood pressure pamoja na BP ambapo alifariki asubuhi ya July 4 2013.. #R.I.P

HILI NDO GARI LA MBAO LILILO TENGENEZWA TANZANIA


Naibu waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Lazaro Nyalandu mwenye suti akipewa maelezo na afisa wa maliasili juu ya gari lililotengenezwa kwa miti ambalo linawavutia wengi bandani hapoNaibu waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Lazaro Nyalandu mwenye suti akipewa maelezo na afisa wa maliasili juu ya gari lililotengenezwa kwa miti ambalo linawavutia wengi bandani hapo Simba kivutio cha banda  (PICHA NA TULIZO KILAGA WA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII)
…………………………………………………………….
Hussein Makame-MAELEZO
GARI ya mbao iliyobuniwa na mkazi wa kijiji cha Nyololo mkaoni Iringa, Keneth Mwangoka imeokoa shilingi Bilioni moja kwa mwaka kwa kuhamasisha kuhifadhi mazingira katika msitu wa Sao Hill ulioko mkoani humo.
Akizungumza na MAELEZO katika viwanja vya Maonesho ya 37 ya Sabasaba jijini Dar es Salaam jana, Afisa Misitu wa Wizara ya Maliasili na Utalii kutoka Msitu wa Sao Hill mkoani Iringa, Fidelis Mwanalikungu alisema gari hiyo ilibuniwa kwa kushirikiana na Kikundi cha Sanaa cha Imehe kilichopo katika kijiji cha Nyololo.
Alisema kikundi hicho kwa kutumia gari hiyo ambayo huvutia watu kuiangalia, kinaeleimisha vijini 58 vinavyozunguka msitu wa Sao Hill kudhibiti matumizi ya moto unawashwa na wakulima wakati wa kuandaa mashamba yao kwa ajili ya kilimo.
Alifafanua kuwa uhamasishaji huo umefanikiwa kupunguza moto kutoka matukio 143 yaliyokuwa yanasababisha hekta za misitu 500 hadi 1000 kwa mwaka hadi kufikia matukiio manne tu kwa mwaka yaliyounguza hekta 17 za misitu.

“Ukiweka hizo hekta 500 hadi 1,000 katika thamani ya fedha unakuta tulikuwa tunapoteza kuanzia Milioni 840 mpaka Bilioni moja kwa mwaka kutokana na kuungua kwa msitiu huo, sasa hii ni hasara kubwa” alisema Mwanalikungu.
Alisema kutokana na elimu inayotolewa kushirikisha kikundi hicho, wameweza kuhifadhi zingira ya msitu huo wa asili wa Serikali, vyanzo vya maji na kuhifadhi mazingira ya vijiji hivyo.
Aliongeza kuwa kwa mujibu wa utafiti uliofanyika mwaka 2009 uliobaini kuwa kutoka mwaka 2010 kurudi nyuma miaka 11 kulikuwa kuna matukio mengi ya moto yenye wastani wa matukio 143 kwa mwaka.
“Ilipofika mwaka 2011 tukaangalia ni mikakati gani tunaweza kuichukua kwa kuwashirikisha wanavijiji, ndipo tukagundua wazo la kusema tukiwa na gari kama hili linalovutia watu, tukaweka mabango ya kuelimisha tunaweza kufikisha ujumbe kwa urahisi zaidi” alisema Mwanalikungu.
Akizungumzia gari hiyo, Keneth Mwangoka gari hiyo aina ya Toyota Hiace aliinunua kutoka kwa mtu ambaye alitaka kuiuza kama chuma chakavu na aliitengeneza ili iweze kusaidia katika kuwavutia wanajiji na kupata njia ya kuwapata kwa urahisia wanakijiji a kufikisha ujumbe.
 Mwangoka ambaye ni fundi wa gari hiyo, alisema gari hiyo ina injini ya Toyota 1S, robu tatu ya vitu vilivyotengeneza ni mbao na inatumia mafuta lita moja kwa kilomita nane.

ALIYEFUNGWA PAMOJA NA MANDELA AMTEMBELEA MANDELA HOSPITALINI KUMJULIA HALI


Denis Goldberg akishuka kwenye gari hospitalini alikolazwa Mandela Jumatatu iliyopita alipokwenda kumtembelea.
Rafiki mmoja wa karibu wa Nelson Mandela jana alidai kwamba rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini anayeumwa alikuwa 'mwenye fahamu zake kamili' wakati alipomtembelea hospitalini wiki hii.

Denis Goldberg, mwanaharakati mweupe wa kupinga ubaguzi wa rangi na mfuasi wa chama tawala cha African National Congress (ANC), alihitilafiana na  maoni ya kitabibu yaliyowasilishwa mahakamani wiki hii, ambayo yanaeleza kwamba Mandela amekuwa kwenye 'hali ya kulala tu' kwa siku tisa zilizopita na familia yake ilikuwa ikijadiliana kuhusu kuzima mashine zake za kuokolea maisha.
Ripoti hizo za kitabibu juu ya hali ya Mandela zimeibuka wakati wa kesi ya mahakamani wiki hii kati ya wanafamilia ya Mandela wanaovutana wakigombea kuhusu wapi atakapozikwa mshindhi huyo wa Tuzo ya Amani ya Nobel.
Goldberg, ambaye alifungwa jela kwa miaka 22 wakati wa mashitaka maarufu ya Rivonia ya mwaka 1964 ambayo yalishuhudia Mandela akihukumiwa kifungo cha maisha, alisisitiza kwamba alimtembelea Mandela Jumatatu na kwamba alimwona 'dhahiri ni mtu anayeumwa sana,  lakini alizisikia sauti na kujaribu kuongea."
Aliongeza: "Alikuwa amelala fofofo wakati nilipoingia pale. Nilizungumza na kumweleza mimi ni nani na akafungua macho yake na kunitazama. Niliongea naye kwa takribani dakika kumi na alionesha kuelewa nilichokuwa nikiongea. Alinitambua mimi ni nani."
Goldberg, ambaye alitumikia hukumu yake kwenye gereza la wazungu mjini Pretoria wakati Mandela alisafirishwa kwa meli kwenda Kisiwa cha Robben, alisema Mandela mwenye miaka 94 'alikuwa hana nguvu lakini alikuwa mwenye fahamu zake kamili."
Aliongeza: "Hakuweza kujibu sababu hawezi kuongea, akiwa na mipira kwenye koo lake, lakini alikuwa akitingisha taya lake kana kwamba anataka kuongea. Hakika nilishangaa sana - baada ya taarifa nilizokuwa nimezisikia."
Huku wengi wa watu wa Afrika Kusini wamekata tamaa kwenye ukweli kwamba Mandela hawezi kupona, taarifa zinazokinzana kuhusu afya yake zimesababisha hofu kuu, huku mmoja wa watangazaji akiishutumu serikali ya ANC kwa kupotosha umma.

BAADA YA JOYCE KIRIA KUSHAULIWA AMWAMBIE MUMEWE AACHANE NA SIASA na Hii ndo kauli na MSIMAMO wake kuhusiana na USHAURI HUO

   IMENUKULIWA MOJA KWA MOJA TOKA KWA JOYCE KIRIA

Hapa kuna swala nahitaji kuliweka sawa, naamini tutaelewana fans zangu wote.




My Hubby Henry Kilewo.


My Hubby Henry Kilewo akiwa katika shughuli zake za kisiasa.


Nimeolewa na mwanasiasa, mume wangu Henry Kilewo ni katibu wa CHADEMA mkoa wa Kinondoni, Ila mimi si mwanasiasa(nahudumia watu wote wenye vyama na wasio na vyama).



Our Wedding Day, Nikila kiapo, "KWA TABU NA RAHA"

Muda nakubali kuolewa naye nilifahamu fika kuwa yeye ni mwanasiasa, Ila nitamsupport mume wangu kwa kazi yake aliyoichagua, siwezi kumwambia AACHE SIASA, Hilo kwa kweli HALIWEZEKANI, Hata yeye hajawahi hata siku moja kuniingilia katika kazi yangu ya kutetea haki za wanawake na maendeleo ya wanawake kwa ujumla(WANAWAKELIVE) na kuniambia niiache.


Hubby Henry Kilewo kikazi zaidi.

Ila nina swali la kuuliza hapa "KILA MTU ANAPOPATA TATIZO KATIKA KAZI YAKE ANATAKIWA KUIACHA???" Mfano Daktari akipata tatizo katika kazi yake aache? Ama Mwalimu ama mtu yoyote yule kwa kazi anayoifanya akipata changamoto anatakiwa kuacha????


My family, Hubby Henry With Our Boys, Lincon na Linston.

Fans Wangu wote naamini mtakuwa mmenielewa na mtaendelea kuwa nami all the way, Msimamo wangu ni huu, Nitasimama upande wake na kuendelea kumsupport mume wangu Henry, SIASA ni kitu anachokipenda SIWEZI KUMWAMBIA AACHE

source-http://www.joycekiria.com/

Hiki ndiyo kitu usichokijua kuhusu mchumba wa Mabeste ambaye anatarajia kupata mtoto na Mabeste hivi karibuni.

306540_332593690173224_2037399722_n


Kama hii ilikupita mtu wangu wa nguvu basi nakupa nafasi ya ujua kwamba msanii Mabeste hivi karibuni atakuwa baba na mchumba wake anaitwa Lisa William. Mabeste ambaye watu wengi wamemjua kupitia ngoma yake “Baadaye sana” na baadaye kufanya video ambayo pia ilifanya vizuri. Lisa William ambaye pia alikuwa video model wa ngoma ya “Sirudi tena” ya Mabeste anatarajiwa kujifungua hivi karibuni na pamoja kutengeneza familia na Mabeste.
mabeste2
Nakupa nafasi ya kuangalia video ya Sirudi tena umuone mama kijacho wa mtoto wa Mabeste akiwa kazini na baba kijacho wake Mabeste wa B Hits Music Group.
mabesta3
mabeste
mabeste4

Kuwa wa kwanza kuona kionjo cha reality show ya Wema Sepetu.

wema
Wema Sepetu alitangaza kwamba anaandaa reality show yake chini ya kampuni anayoimiliki “Endless Fame”. Muda umefika wa kuanza kuonyesha hiyo show yenyewe na Wema ameshatoa teaser au kionjo cha reality show hiyo ambayo inaonyesha baadhi ya vitu vinavyohusika kwenye show hiyo. Kwenye hii teaser inamuonyesha Wema anazungumzia kazi, mahusiano na katajwa Diamond humo,ziara za Wema na maisha ya nyumbani.

MTANGAZAJI DIDA SHAIBU (WA KIPNIDI CHA MITIKISIKO YA PWANI) AOLEWA NA SASA NI MRS EZDEN JUMANNE.


Dida wa Ezden ndo habari ya mujini

Maharusi wakiwa na nyuso za furaha mara baada ya kufunga ndoa 
Bwana harusi akimchum mke wake halali wa ndoa Dida
Mashallah the newly weds Mr & Mrs Ezden Jumanne.
Hongera sana Dida na Ezden tunawatakia kila la kheri katika ndoa yenu.
PICHA KWA HISANI YA http://www.jestina-george.com.

Superman Dwight Howard kuitosa L.A Lakers?


dm_130620_dwight_howard_image
Dwight Howard mchezaji wa ligi ya NBA nchini marekani kwenye timu ya Los Angels Lakers akiwa na mkali mwezake kama Kobe Brayant, inasemekana anataihama timu hiyo hivi karibuni. Dwight Howard ambaye aliwahi kutembelea Tanzania na kutoa misaada kwenye shule ya sekondari Kipok huko Arusha mbele ya waziri mkuu kwa wakati hule mheshimiwa Edward Lowassa, alitokea timu ya Orlando Magic msimu uliopita na kujiunga na Lakers ili kuunganisha nguvu na Kobe, lakini wamepata matokeo mabaya sana msimu huu ulioisha. Mategemeo makubwa ya washabiki wa Lakers ilikuwa ni kumuona Howard akitengeneza pacha na Kobe kama ilivyokuwa kwa Kobe na mkali mwingine aliyestaafu Shaq Oneil.
2

DWIGHT HOWARD AKIMZAWADI JEZI YAKE RAIS KIKWETE IKULU YA DAR ES SALAAM
Tetesi zinasema kwamba huenda Dwight Howard akahamia Huston Rockets ambapo kuna wakali wengine kama James Harden. Kama akihama litakuwa pigo kubwa sana Lakers kwasababu Howard atakuwa ameitumikia timu hiyo kwa msimu mmoja tu.Kwa mujibu wa mtandao wa kuaminika wa NBA ambao umeongea na wakala wa mchezaji huyu, amesema kwamba mteja wake bado hajafanya maamuzi wapi pakwenda lakini atatoa maamuzi yake hivi karibuni.
howard1 DWIGHT HOWARD AKIKABIDHI MSAADA WA MILLIONI 90 HUKO ARUSHA howardDWIGHT HOWARD AKIWA NA MHE LOWASSAdwight-howard-hasheem-thabeet-2009-10-12-21-40-47DWIGHT HOWARD AKIPAMBANA NA HASHEEM THABEET UWANJANIkobe-dwight-howard-lakers
 DWIGHT HOWARD NA KOBE BRAYANT

Umezisikia taarifa za Rais Kikwete kuwa refa wa Simba na Yanga jumapili hii?




Naona hii ni historia kabisa aisee….. yani Rais Jakaya Kikwete anaweza hata kuingizwa kwenye kitabu cha kumbukumbu za dunia kwa kukubali mwaliko wa kuwa refa na kuchezesha mechi ya Wabunge wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania wa timu za Simba na Yanga jumapili July 7 2013.
Taarifa ambayo nimepewa na Global Publishers ambao ndio waandaaji, ni kwamba Rais amekubali kuwa refa kwenye Tamasha la Matumaini litakalofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam ambalo sehemu ya mapato yake yatasaidia elimu Tanzania.
Ni mara ngapi tunamuona President wetu kwenye sehemu rasmirasmi akiwa mgeni rasmi? ni mara ngapi tunatamani kuona upande wake wa pili kwenye ishu kama hizi? basi Jumapili hii itakua burudani na pia vichekesho… yani ukijaribu kutengeneza picha President na umri wake, na umbo lake, na cheo chake alafu apulize filimbi?????
Yani anakuwa refa na jezi zake kabisa…. na tumeshamzoea siku zote huwa anatokelezea hivi yani….
.
.
.
.
.
.
.
.

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...