facebook likes

Saturday, August 3, 2013

new Joint_ Nelly ft Nicki Minaj & Pharrell - Get Like Me (official video)



new Joint_ Soulja Boy - I'm The Man(official video)



new Joint_ ROBIN THICKE'S NEW 'BLURRED LINES' VIDEO, ftJIMMY FALLON AND THE ROOTS



new Joint_ PLIES - ''PAINT A PICTURE'' (official audio)



Beyonce and Jay Z called demons in D.C.


Two protesters set up shop outside The Mrs. Carter Show at the Verizon Center in Washington D.C. warning  Mrs Obama and other concert goers that Beyonce and Jay Z were possessed by demons.

Founder of the Pray at the Pump movement, Rocky Twyman, tells Afro.com
"We believe that this couple is virtually destroying our youth. If you go on the Internet, you’ll see stories about how they’re both part of the Illuminati and you can see Jay-Z’s use of the Satanic triangle symbol when he performs."
"Jay-Z even declared himself to be God by referring to himself as Jehovah, and we don’t think that this is the image that our young people need to be glorifying.”
Tyman hopes his movement will catch on with protests in every city on the rest of Beyonce's tour.

"Genevieve is the hottest chick in Nollywood" - Ramsey Noah says


Ever wondered if the rumour that Ramsey Noah and Genevieve Nnaji once dated is true? Nigeria's finest actor clears the air on that. He also talks about the time when a crazy fan stalked him at his home in front of his wife, and claimed to be sent by God. 

Watch the exclusive interview with Emma Emerson of Golden Icons after the cut...

BARUA KWA MH. RAIS KUTOKA KWA JOHNSON NGUZA (PAPII KOCHA)


AKIFIKISHWA MAHAKAMANI ENZI ZA KESI YAKE

MF/NA: 836'04 Johnson Nguza
(Papii Kocha) Gereza Kuu Ukonga
S.L.P 9091
Dar es Salaam
Mh. Rais Jamuhuri ya Muungano Tanzania

YAH: MAOMBI YA KUPEWA MSAADA (MSAMAHA) WA KUFUTIWA ADHABU YA KIFUNGO NILIYOPEWA NA MAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI KISUTU.

Husika na somo hilo hapo juu. Mimi ni mfungwa katika gereza kuu Ukonga. Kwa heshma na taadhima na kwa kutambua utu na huruma yako ya kiMUNGU ulionayo dhidi ya binadamu wenzako pamoja na mamlaka uliokabidhiwa na Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania. Naanguka na kushika miguu yako mitukufu muheshimiwa rais....Nakuomba msaada (msamaha) kwako muheshimiwa rais, kwa njia hii ya maandishi kusudi niweze kuondolewa adhabu ya kifungo cha maisha gerezani, niliyohukumiwa na mahakama tajwa hapo juu. Mh.Rais mimi nimefungwa nikiwa bado kijana mwenye umri mdogo, na ukweli kutoka moyoni sikufanya kosa hilo.

Si mimi, baba yangu Nguza wala ndugu yangu yeyote aliyefanya kitendo kile. Lakini wenye mamlaka wakatuona tuna hatia na kuamua kuteketeza kizazi chetu gerezani.

Natamani kiama ifike ili mwenyezi Mungu aweke wazi ukweli wote uliojificha nyuma ya pazia. Mpaka sasa natambua wazi hatima pamoja na dhamana ya maisha yangu ipo katika mikono yako mitukufu Mh. Rais Naomba huruma yako muheshimiwa Rais maana mimi ni mtoto wako ninaehitaji huruma yako wewe mzazi. Lakini pia sisi ni binadamu wenye nafsi na miili kama wengine. Waliotumia mamlaka yao kutuweka gerezani nao ni binadamu pia, wenye miili na nafsi.

Ipo siku nafsi zetu zitapaswa kutoa hesabu ya tuliyoyafanya hapa duniani. wakati huo miili yetu tunayoitumia kunyanyasa wanyonge itakuwa imeoza mavumbini.

Natumaini kauli yako ya mwisho ndio itakayoleta pumzi ya uhai nafsini mwangu. Nakutakia kazi njema, afya njema na maisha marefu. Mungu akubariki. Wako mtiifu

Mfungwa NO:836'04 JOHNSON NGUZA (PAPII KOCHA)

BAADA YA ROSE NDAUKA KUHUSISHWA KATIKA FUMANIZI...!! HAYA NDIYO MANENO YA MCHUMBA WAKE ROSE KUHUSU SAKATA HILO


 
BAADA ya msanii wa filamu nchini Rose Ndauka kuripotiwa kufumaniwa akiingia gesti na msanii chipukizi wa muziki wa bongo fleva Nassoro Ayoub 'Dogo Nasry' huku akiwa amevaa baibui kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani,  mumewake mtaarajiwa Maliki Bandawe 'Chiwaman' amjia juu msanii huyo kwa madai ya kumchafua mpenzi wake.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Chiwaman aliweka wazi kuwa msanii huyo Nasry ambaye alimuomba Rose aweze kushiriki kwenye video yake, walishindwa kufikia maamuzi kutokana na kiwango cha malipo kuwa madogo, na badala yake msanii huyo alimuomba wapige picha kama ukumbusho.

Alisema kuwa kitendo hicho cha kupiga picha na msanii huyo wakati wapo katika mazungumzo ya awali ya kukubaliana malipo ndizo picha alizotumia msanii huyo na kudai kuwa alikuwa naye nyumba ya wageni kitendo ambacho si cha kweli.

"Hawa wasanii wachanga wanatafuta umaarufu vibaya kwa kuwachafua watu, ilikuwa amemuomba Rose ashiriki kwenye video yake na ndipo walipokutana kwa ajili ya mazungumzo hayo na alikuwa na mdogo wangu sasa hapo masuala ya gesti yametokea wapi" alisema Maliki.

Aliongezea kuwa "kama nilikuwa sijui hicho kitu na kwa jinsi mambo yalivyokuwa ningeweza kumuacha mchumba wangu ninayempenda kwa dhati, ila msanii huyo alichokifanya siyo jambo sahihi, kwani alimuomba apige naye picha na Rose alikubali huku bila kujua nia yake ".

Maliki alisema kuwa huyo msanii anatafuta umaarufu kwa kuchafua majina ya watu wengine, kitu ambacho hakina mashiko kwenye jamii.

'Uchaguzi Zimbabwe ulikuwa huru'Obasanjo


Mkuu wa ujumbe wa uangalizi kutoka Muungano wa Afrika nchini Zimbabwe, Olusegun Obasanjo amesema uchaguzi mkuu wa hapo Jumatano ulikua huru na haki. Matokeo ya awali yanaoyesha Rais Robert Mugabe na chama tawala cha Zanu PF wakiongoza kwa kura nyingi
Chama hicho tayari kimedai ushindi. Msemaji wa chama hicho Rugare Gumbo alisema chama hicho kilitarajiwa kushinda kiasi ya asilimia 70 ya kura hizo
Lakini mpinzani wa Mugabe, Morgan Tsvangirai, amesema uchaguzi huo ni wa uongo na kusema udanganyifu uliofanyika una maana uchaguzi huo haukubaliki.
Waangalizi kutoka Umoja wa Afrika na jumuia ya maendeleo kusini mwa Afrika wanatarajiwa kutoa tamko rasmi hii leo kuhusu uchaguzi huo.
Bw. Obasanjo amesema kulikua na visa kadhaa wakati wa shughuli ya kupiga kura. Hata hivyo amesema visa hivyo haviwezi kutajwa kuwa na uzito wa kubatilisha au kufuta matokeo ya kura.
Msimamo wa Muungano wa Afrika unatofautiana na ule wa kundi la uangalizi la Zimbabwe Election Support Network.
Kundi hilo ambalo ndilo kubwa zaidi linalochunguza kura ya Zimbabwe limekashifu uchaguzi mkuu na kusema ulikuwa na dosari nyingi. Hii ni kwa sababu watu milioni moja walizuiwa kupiga kura.
Huku upande wa Rais Mugabe ulitangaza kushinda uchaguzi na Morgan Tsvangirai akipinga ni dhahiri kwamba Zimbabwe ingali na mgawanyiko mkubwa wa kisiasa.

TANZANIA YAREJESHA KWAO WAKIMBIZI LAKI SITA NA KUFUNGA KAMBI 12 ZA WAKIMBIZI

Dk. Emmanuel Nchimbi Waziri wa mambo ya ndani
dk emmanuel nchimbi
Serikali ya Tanzania imewarejesha kwao kwa hiari wakimbizi wapatao569,018 toka nchi za Maziwa Makuu waliokuwa wamehifadhiwa hapa nchini kutokana na machafuko katika nchi zao.  Kati ya hao 502,358 walitoka nchini Burundi na 66,660, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.  Wakimbizi hawa wamerejeshwa kwao kufuatia zoezi lililoanzishwa rasmi mwaka 2002 kwa wakimbizi toka Burundi na mwaka 2005 kwa wakimbizi toka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRS), baada ya usalama katika nchi zao kuimarika.
Sambamba na mafanikio haya, pia kambi 12 kati ya 13 zilizokuwa zikitumika kuwahifadhi wakimbizi hawa zimefungwa, na hadi sasa ni kambi moja tu ya wakimbizi ya Nyurugusu, wilayani Kasulu mkoani Kigoma ndiyo iliyobakia ikiwahifadhi wakimbizi kutoka DRC (63,728), Burundi (4,153) na nchi nyingine mchanganyiko za Kiafrika (212).
Tanzania inajulikana kimataifa kama nchi mojawapo ambayo imechangia kwa kiasi kikubwa kutoa hifadhi kwa wakimbizi wanaokimbia nchi zao kutokana na machafuko ya kiaiasa ambapo mwaka 1995 idadi yao ilifikia zaidi ya milioni moja.
Lengo la Serikali ni kuona kuwa suala la kuhifadhi wakimbizi hapa nchini linafikia ukomo na juhudi zinaendelea kuona kuwa hata Kambi ya Nyarugusu ambayo ndiyo kambi pekee iliyobakia inafungwa baada ya wakimbizi walio katika kambi hiyo kurejeshwa kwao, pale hali ya usalama nchini DRC itakapokuwa imeimarika.
Kuondoka kwa wakimbizi hawa sasa kunatoa nafasi kwa Serikali na wananchi kutumia kwa shughuli nyingine za kimaendeleo maeneo makubwa yaliyokuwa yanatumika kuhifadhi wakimbizi, lakini pia kunatoa nafasi nzuri ya kuweza kukabiliana na changamoto za kiusalama katika maeneo hayo ambayo yapo katika mikoa ya mpakani mwa nchi.
Serikali inapenda kuishukuru Jumuiya ya Kimataifa kupitia Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), kwa misaada ya hali na mali waliyotoa na wanayoendelea kutoa kusaidia hifadhi ya wakimbizi hapa nchini. Pia Watanzani wote na hasa wale wa mikoa ya Katavi, Kigoma na Kagera kwa ushirikiano waliotoa kwa wakimbizi waliokuwa wamehifadhiwa katika maeneo yao, na nchi za Burundi, Congo kwa ushirikiano wao uliowezesha kuwarejesha raia wao waliokuwa wamehifadhiwa hapa nchini.
Mashirika mengine ambayo pia yalihusika na yanaendelea kutoa huduma za kibinadamu kwa wakimbizi ni pamoja na Shirika la Chakula Duniani (WFP), Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Kuhudumia Watoto (UNICEF), Kamati ya Kimataifa ya Uokozi (IRC), na Shirila la Msalaba Mwekundu Tanzania (TRCS).
Imeandaliwa na Felix Mwagara
KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

HII NDO Dawa ya Ukimwi Iliyopatikana!



GARANIMW1is a herbal preparation that is being used to treat people that have HIV and AIDS. It has strong antiviral properties and therefore also positively affects immune system. The medicine improves the immune system by increasing ones CD4 cell count because viral replication is reduced/halted. The body is then able to fight opportunistic infections that come due to thecompromised immunity. The viral load is reduced to undetectable levels and people have tested non reactive to the HIV tests using both anti body and HIV DNA/ PCR tests. As Garanimw1 is available in powder form, it is taken through porridge made from maize flour with no sugar or salt, one tea teaspoon per day, once a day for three consecutive days, repeated after a period of two weeks from the same pack. Some have become totally cured after taking only one pack while others may need to repeat the dose at 1 month intervals.DISEASES

Frequent and nonstop headaches, chest pains and breathlessness, chronic undefined coughs, skin rashes, other skin conditions, cancer, hair loss, swollen lymph nodes, painful legs, asthma, unexplained weight loss, numbness in the legs and other body parts, hormonal imbalances, general body weaknesses and pains, chronic wounds, diabetes, high blood pressure, loss of memory, cancerous growths, anaemia, skin discolorations and many others. There are many people that have taken the medicine but did not have the HIV virus and have reported success stories on diseases and conditions such as diabetes, high blood pressure, asthma, stomach ulcers, sickle cell, and other abdominal swellings in the body, amenorrhea and others. Some people who had lost their shape due to the effects of ARVs (lipodystrophy) have regained it even while taking the drugs. INTSRUCTIONS
1.The full course of the medicine is three teaspoons of the powder taken over a period of three days, one teaspoon per day for three days – put in porridge with no sugar or salt. The remaining powder should be taken after two weeks in the same manner until it is finished. One should choose time when to take the medcine 2. The porridge should be put in a bowl or cup before adding the medicine and not in a pot. 3.For couples, both should take the medicine and abstain from sex or use condoms correctly and consistently until they go for the HIV test when time is due 4.One can go for test after 12 months. This is the HIV antibody test in which a small amount of blood from a finger prick is tested since antibodies may persist in the blood for several months even after when the disease causing organism has disappeared from the blood stream. 5.HIV DNA PCR test can be done after 10 months which looks into the presence of the actual virus. 6.If one is on ARVs or any other medication they should continue taking the medicine and one will be advised to stop taking the ARVs by a qualified physician when all the above tests are done and are negative 7.The known effects of the medicine is that others may develop increased appetite and thirst therefore food and water should be taken as required. 
 
NOTE: For better and faster results, the dosage should be repeated at 1 month interval for two or more times with condom use at all times although one dose 
 
source:audifacejackson

UNYAMA: POLISI AMCHARANGA MAPANGA MWANAE KISA WIVU WA MAPENZI..picha na tukio hapa (SAMAHANI KWA HIZI PICHA)

(TUNAOMBA RADHI KWA PICHA HIZI.)


MTOTO WA MIAKA 4 DEVOTHA GERLAD ALIYEKATWA MAPANGA NA BABA YAKE,HAPA AKIWA HOSPITALI KWA HUDUMA AYA KWANZA.
WANANCHI WAKIWA NJE YA HOSPITALI YA WILAYA WAKIWA NA SHAUKU YA KUMUONA MTUHUMIWA.

KINA MAMA WALIOGUSWA NA TUKIO WAKIWA NJE YA HOSPITALI KUMUONA MTOTO HUYO. 

AFANDE BWIRE AKIWA HOI WODINI

HAPA AFANDE AKIWA HOI BAADA YA KUFIKISHWA HOSPITALINI..

MADAKTARI WAKIJITAHIDI KUOKOA MAISHA YA MTOTO HUYO.

MADAKTARI WAKIWA KAZINI KUHAKIKISHA WANAOKOA MAISHA YA MTOTO HUYO.
AFANDE BWIRE AKIWA HOI WODINI HUKU AKIWA AMEFUNGWA PINGU.

JITIHADA ZA KUOKOA MAISHA YA MTOTO ZIKIENDELEA

INASIKITISHA SANA JAMANI

MAJUKUMU YA KUOKOA MAISHA YA MTOTO HUYO YAKISONGA KWA KASI.

AFANDE BWIRE AKIWA NA PINGU ZAKE WODINI

MUNGU AMPE AHUENI MTOTO HUYU.

KAHAMA
Mkazi wa kitongoji cha Sango kata ya Nyasubi wilayani Kahama mkoa wa Shinyanga Samson Bwire (54), ameshikiliwa na jeshi la polisi kwa kumcharanga mapanga mtoto wake Devotha Gerald (4) kwa sababu za wivu wa kimapenzi....

Tukio hilo limetokea jana jioni nyumbani kwa Bwire baada ya kuanza kugombana na mke wake Happiness (28) Elias huku akiwa amelewa pombe ambapo, mkewe alikimbia kitu kilichosababisha kumgeukia mtoto Devotha na kuanza kumkata mapanga kichwani.....

Kwa mujibu wa majirani, kelele zilisikika kutoka kwenye mji huo na kwamba walipoenda walimkuta Bwire akichoma nguo za mke wake, na alipowaona aliingia ndani na kuanza kumkata mapanga mtoto huyo huku akiwa amefunga mlango.

Imefafanuliwa kuwa, baada ya kusikia kelele za mtoto, majirani walianza kuvunja milango huku wakiomba msaada kituo cha Polisi na baada ya Polisi kufika walifanikiwa kumnusuru mtoto akiwa amejeruhiwa vibaya sehemu za kichwani.......

Majirani kwa hasira walianza kumpiga Bwire ambaye ni askari polisi mstaafu wa cheo cha koplo kwa nia ya kumuua, hali ambayo imelipa jeshi la Polisi kazi ya ziada kumnusuru na kumpakia kwenye gari kwenda kituoni.

Hata hivyo Wakati gari la Poisi likiwa katika mwendo wa kasi eneo la soko la Mkulima, Bwire ameruka kutoka kwenye gari na kuangukia kwenye Lami kitendo kilichomsababishia majeraha makubwa sehemu za usoni.

Mtoto Devotha na baba yake Bwire wote wamelazwa katika hospitali ya wilaya ya Kahama kwa matibabu huku Bwire akiwa Chini ya Ulinzi mkali wa polisi.

@source:SwahiliTz

Mbunge amwaga machozi mbele ya Waziri Maghembe


Moto
Nyumba ya Mbunge wa Masasi Mjini, Mariam Kasembe (CCM),iliyoteketezwa kwa moto na wananchi katika vurugu zilizotokea Machi, mwaka huu.
 
Mbunge wa Masasi Mjini, Mariam Kasembe (CCM), amemwaga machozi mbele ya Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe, baada ya kutembele nyumba yake iliyoteketezwa kwa moto na wananchi katika vurugu zilizotokea Machi, mwaka huu.
Tukio hilo lilitokea juzi wakati Waziri Profesa Maghembe kutembelea maeneo mbalimbali ya serikali yaliyoharibiwa na wananchi katika vurugu hizo na kujionea uharibifu mkubwa.
Baada ua Waziri Maghembe kufika mahali ilipokuwapo nyumba ya mbunge huyo, alishuhudia pia uharibifu mkubwa uliofanywa na wananchi hao.
“Kutokana na hali hii, mpaka sasa familia yangu haina mahali pa kuishi. Tumeendelea kuishi kwenye kontena kwa zaidi ya miezi sita sasa,” Mbunge Kasembe alimweleza Waziri Maghembe huku akibubujikwa machozi.
“Hali ni mbaya sana, uharibifu ni mkubwa, lakini tusonge mbele na tusikubali uharibifu kama huu kutokea tena,” alisema Profesa Maghembe.
Aidha, Waziri Maghembe aliuagiza uongozi wa Halmashauri ya Masasi kuangalia namna ya kumsaidia mbunge huyo.

JAMES CAMERON AMETANGAZA KUTOA AVATAR 2,3 NA 4.



Director mkali kwenye movie industry “James Camerom” ametangaza kwamba kutakuwa na avatar 2, 3 na 4.
James Cameron amejivulia umaarufu mkubwa kenye soko la movie baada ya kufanya blockbuster kama Titanic na Avatar.
Avatar 2 inatarajiwa kutoka December 2016, wakati Avatar 3 itatoka December 2017 na Avatar 4 itatoka December 2018.
Avatar ndio movie inayoongoza kwa kuingiza hela nyingi na kufikia $2.8 billion gross.

hii ndio official trailer ya Avatar 1

UTURUKI YASAINI HATI YA USHIRIKIAN​O


Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali, Said Mwema (kushoto) pamoja na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Uturuki, Zeki Catalakaya (katikati) wakisaini hati ya ushirikiano wa kuchunguza matukio ya uhalifu kati ya Tanzania na Uturuki. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwamini Malemi akilishuhudia tukio hilolililofanyika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, jijini Dar es Salaam
PIX 3 5b3dd
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Uturuki, Zeki Catalakaya (kulia) akimkabidhi ufunguo wa gari la kuchunguza matukio ya uhalifu, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwamini Malemi. Tukio hilo la makabidhiano lilifanyika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, jijini Dar es Salaam leo. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

BAADA YA KUFUNGUA KAMPUNI KUBWA AFRICA SWAHILI MEDIA MAREKANI MPIGANAJI DAVIS MOSHA “THE CEO” AMUITA SUGE KNIGHT KWA AJILI YA PROMO


    Alex Kassuwi akimpokea Mario Hugh knight Jr. aka Suge Knight alipokuwa anawasili kuitikia mwito wa “THE CEO” Davis Mosha. Ambapo walijadiliana jinsi ya kuikuza AFRICA SWAHILI MEDIA nchini Marekani. THE CEO alimuita Suge Knight kutokana na uzoefu wake katika branding na promotion. Suge ni mjasirialiamali na mwekezaji mkubwa, na ni muasisi na alikuwa CEO wa  Black Kapital Records na vilevile ni muasisi mwenza na CEO wa zamani wa Death Row Records. Amewapa mafanikio makubwa wasanii Tupac Shakur, Dr. Dre, Snoop Dogg aka Snoop Lion, Outlawz na Tha Dogg Pound. 
   Suge akiwasili kumuona “THE CEO” Davis Mosha under escort
  Suge Kabla ya kumuona THE CEO alitambulishwa kwanza kwa mtoto wa Davis Mosha, Edgar Mosha. Kulia ni Mayor wa L.A. Bwana Deo Temba.
 Baada ya mazungumzo ya muda mrefu na THE CEO Suge alipata picha ya ukumbusho
  Mayor wa L.A. Deo Temba, Edgar Davis, Suge Knight na THE CEO Mpiganaji Davis Mosha wakiwa pamoja JW Marriott L.A. LIVE
Crew walioambatana na Suge Knight kuja kumuona “THE CEO” Davis Mosha kwa ajili ya Kuikuza AFRICA SWAHILI MEDIA Marekani.
Suge knight alipokuwa akiondoka baada ya kikao na Mpiganaji Davis Mosha THE CEO.
Picha na Africa Swahili Media

Actress Mercy Johnson Bombarded with Movie Scripts




 Actress Mercy Johnson Bombarded with Movie Scripts
Actress Mercy Johnson who’s finally back to work, after delivering her first child in the US, has gotten no less than 20 scripts in the last one month from movie marketers and producers in Nigeria and Ghana.
According to a Nollywood source: "MJ is fully back. In the last one month, she has been bombarded with several scripts from different marketers and producers who want to get her on their movies. She hasn’t decided the ones she will do and the ones she won’t do yet. It is as if they were all waiting for her return."

MJ, as Mercy is fondly called, had taken a leave off movies to focus on her marriage and to deliver her baby daughter, Purity.

Already, since her return to Nollywood, she’s featured in about three productions, including the on-going Tchidi Chikere produced comedy, ‘Dumebi Goes to School’, a sequel to the hilarious ‘Dumebi The Dirty Girl’.
[source: naij.com]

YALIYOJIRI WIKI YA UNYONYESHAJI : Miiko, mila zinazokwamisha unyonyeshaji


Mkazi wa eneo la  Losikito Paulina Richard akimnyonyesha mwanaye Magreth Richarde.
  • Anaeleza pindi anapokuwa mjamzito hapati vyakula vinavyohitajika kama lishe hivyo analazimika kutumia muda mwingi kufanya vibarua vya kumwingizia kipato, hivyo kutokana na uhaba wa fedha hulazimika kwa siku kupata mlo mmoja.

Wanaume wengine hukimbia wenza baada ya kuwapa mimba
Arumeru. Hali ngumu ya maisha ni  chanzo cha lishe duni kwa mama mjamzito hata mtoto anayetarajiwa kuzaliwa kwa kuwa wengi wao hutumia muda mwingi kujitafutia kipato.
Imekuwa ni jambo la kawaida kwa jamii ya Kimasai hasa wanaume kuwaacha wanawake zao nyumbani huku wakiwaachia majukumu yote wanawake hao wakihangaika kutafuta maisha ili waweze  kuendesha maisha inayomzunguuka.
Mama mjamzito anatakiwa ale chakula kwa siku mara nne asubuhi apate kifungua kinywa na kuanzia saa 3 hadi saa 4 asubuhi anatakiwa apike uji ambao ni lishe wenye mchanganyiko kama  mahindi, mtama mweupe na karanga ambao akinywa utamjenga mtoto aliye tumboni.
Vyakula hivyo vitamsaidia kutengeneza virutubisho muhimu katika maziwa ambayo anatarajiwa kunyonya mtoto atakayezaliwa.
Hivyo,  mtoto anapozaliwa zaidi ya saa moja anyonye maziwa ya mama yake kwanza ambayo yana virutubisho vyote vya kumlinda mtoto huyo.
 Hata hivyo, hali ni tofauti kwa jamii hiyo ya Kimasai ambako asilimia kubwa ya wanaume wakishawapa mimba wake zao, wengi husafiri na kwenda nje ya mkoa wao kutafuta maisha au hata kuoa mke mwingine .
Neema Sanare,  mkazi wa  eneo la Losikito Kata ya Mwandeti Wilaya ya Arumeru Magharibi mkoani Arusha anaeleza kuwa yeye ni mjamzito kwa sasa ana mtoto mwenye umri wa miaka mitatu lakini pindi anapokuwa mjamzito hadi kujifungua mume wake huwa anaondoka kwenda kwa mke mwingine.
Anaeleza pindi anapokuwa mjamzito hapati vyakula vinavyohitajika kama lishe hivyo analazimika kutumia muda mwingi kufanya vibarua vya kumwingizia kipato, hivyo kutokana na uhaba wa fedha hulazimika kwa siku kupata mlo mmoja.
Sanare anasimulia akiwa na hali hiyo au analea mtoto, mume wake huwa hamjali na anahamia kwa mwanamke mwingine au anasafiri kwenda Kenya kutafuta maisha.
“Kama hivi nina wakati mgumu ni kawaida yake nikishakuwa mjamzito hadi najifungua, mwanaume haonekani hadi mtoto atakapofikia umri wa miaka mitatu.
Anasema alipojifungua mtoto wake wa kwanza mume wake aliondoka na kumwacha akiwa na mama  mkwe  ambaye alikuwa anamtunza, lakini mtoto alipofika miezi minne alilazimika kufanya shughuli ya kumpatia kipato ili aweze kuishi.

MWANAMKE MWINGINE WA KITANZANIA AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA ZIMBABWE


A 34–year–old Tanzanian woman was last week arrested at the Harare International Airport after she was found in possession of an illicit drug with a street value of $45 000 upon arrival from India.

SENIOR REPORTER
Demu mwingine wa Ktz anaeishi South Africa kwa Jina la Jackline Mollel akamatwa na madawa ya kulevya nchini Zimbabwe.........

Duh,,,,, hivi hii kitu ya madawa imeingia kama fashion ya nguo  eeeh???


Hivi how desparate do you have to be to do this???? AU Niseme how stupid does one need to be kufanya hii kitu??

Soma kilichoandikwa na Website Maarufu Zimbabwe hapa chini:
A 34–year–old Tanzanian woman was last week arrested at the Harare International Airport after she was found in possession of an illicit drug with a street value of $45 000 upon arrival from India.
SENIOR REPORTER
Mollel Jackline Richard, who stays in South Africa, was not asked to plead when she appeared before Harare magistrate Donald Ndirowei yesterday.
She was remanded in custody to July 27.
Richard was allegedly found in possession of 15kg of ephedrine which stimulates the heart and nervous system. It is often found in herbal and diet pills.
The State alleged that Richard arrived at Harare International Airport aboard an Emirates flight from India.
The alleged drug pusher produced her passport at the immigration desk at the airport where an alert officer tipped CID Drugs detectives that Richard had a visa for India which is a known source for illicit drugs.
The court heard that Richard was taken for interviewing and during a search conducted on her by detectives they recovered 30 khaki envelopes containing a whitish substance which was wrapped with fabric sheets inside a maroon bag.
Tests were conducted on the substance and revealed that it was ephedrine. The drug was then taken for recording and weighing.

Tume: Hakuna gharama kuendesha Serikali tatu


Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Humphrey Polepole akizungumza jambo.

Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya, imewabeza watu, hususan wanasiasa wanaosimama majukwaani kueleza Muundo wa Muungano wa Serikali tatu utaongeza gharama za kiuendeshaji kuwa ni uongo na sababu hizo hazina tija.
Mjumbe wa Tume hiyo, Humphrey Polepole alisema hayo jana wakati wa mkutano wa kuijadili Rasimu ya Mabadiliko ya Katiba Mpya mbele wa Wajumbe wa Baraza la Wilaya ya Nanyumbu Mkoani Mtwara.
Alisema Muundo wa Serikali tatu hauna gharama zozote kwani chanzo cha mapato cha kuongoza Serikali ya Muungano kuwa tayari kimebainishwa.
Polepole alisema gharama za kuongoza Serikali hiyo zitatokana na Kodi ya Ushuru wa Bidhaa ambapo jumla yake zinazokusanywa si chini ya  Sh1 trilioni.
 “Mpaka sasa Serikali ya Muungano inakusanya zaidi ya Sh3 trilioni hivyo kama itatumika  Sh1 trilioni na zitakazobaki zitaelekezwa katika shuguli zingine, fedha zitakuwepo,” alisema Polepole na kuongeza:
 “Nashangaa wanasiasa wanaosimama majukwaani kueleza wananchi kuwa kutakuwa na mzigo wa gharama, hii si kweli kwani Tume tumekwisha bainisha chanzo chake cha mapato na hao wanaozungumza hayo hawafuatilii mchakato kwa umakini.”
 Alisema uchambuzi walioufanya juu ya kodi inayokusanywa mwaka 2003/04 zilikusanywa jumla ya Sh500 bilioni na mwaka 2011/12 zilikusanywa Sh1 trilioni ambapo kila mwaka mapato hayo yanaongezeka.
 “Uzoefu unaonyesha kila mwaka mapato yanaongezeka hivyo uwepo wa Muungano wa Serikali tatu ni dhahiri hautaathiri kitu chochote na utasaidia kutatua kero zilizopo zinazojitokeza kila mwaka kila kukicha,” alisema Polepole
 Polepole aliwataka Wananchi kutokuwa na shaka na mapendekezo hayo ya Tume juu ya Muundo wa Muungano kuwa wa Serikali tatu kwani utapunguza malalamiko ya muda mrefu yaliyopo.
 “Hivi sasa kuna kero zaidi ya 47 na kwa Muungano huu uliopo hautamaliza na wala hauwezi kuyafanyia kazi lakini kutokana na mapendekezo ya Tume ya Serikali tatu ninahakika yatapungua na kila upande kutokuwa na  malalamiko,” alisema Polepole.
Polepole amesisitiza kwa kuwaomba wananchi kuendelea kutoa maoni katika hali ya kutoshinikizwa kwa namna yoyote.
“Kila mtu anapaswa kuwa huru kutoa maoni yake bila kuogopa chochote. Lengo la uwepo wa katiba mpya ni kujua hitaji hasa la wananchi ni nini na kwamba katika kutoa maoni wananchi wanapaswa kufanya hivyo bila woga,” alisisitiza Polepole.
chanzo;mwananchi.

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...