facebook likes

Wednesday, July 10, 2013

WAAMUZI WALIOPANGWA KUCHEZESHA MECHI YA STARS VS UGANDA WAFELI MTIHANI WA WAAMUZI - WABADILISHWA



Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limefanya mabadiliko ya mwamuzi wa mechi ya mchujo kusaka tiketi ya Fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ligi ya Ndani (CHAN) kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Uganda (The Cranes) itakayochezwa Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mwamuzi aliyeondolewa kutokana na sababu za kiufundi ni Jean Claude Birumushahu aliyekuwa mwamuzi msaidizi namba moja. Nafasi yake sasa inachukuliwa na Herve Kakunze pia kutoka Burundi.

CAF imemuondoa mwamuzi huyo baada ya kufeli katika mtihani wa waamuzi (Cooper Test) kwa waamuzi wa Burundi wanaotambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) uliofanyika nchini humo siku tatu zilizopita.

Waamuzi hao na Kamishna wa mechi hiyo Gebreyesus Tesfaye kutoka Eritrea wanatarajiwa kuwasili nchini kesho (Julai 11 mwaka huu) kwa ndege za Kenya Airways na EgyptAir kwa muda tofauti.

Nayo Uganda Cranes inatarajiwa kuwasili nchini kesho (Julai 11 mwaka huu) na itafikia hoteli ya Sapphire. Shirikisho la Mpira wa Miguu Uganda (FUFA) bado halijatuma taarifa rasmi juu ya ujio wa timu hiyo.

Wakati huo huo, makocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen na wa Uganda, Milutin Micho pamoja na manahodha wao watakuwa na mkutano na Waandishi wa Habari utakaofanyika keshokutwa (Julai 12 mwaka huu) saa 5 asubuhi kwenye ofisi za TFF kuzungumzia mechi ya Jumamosi.

FRIENDS, POLISI KUCHEZA MECHI YA RCL JUMAPILI
Mechi ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) kati ya Friends Rangers ya Dar es Salaam na Polisi Jamii ya Mara iliyokuwa ichezwe Jumamosi (Julai 13 mwaka huu) imesogezwa mbele kwa siku moja.
Timu hizo sasa zitacheza Jumapili (Julai 14 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Azam ulioko Chamazi. Polisi Jamii ilishinda bao 1-0 mechi ya kwanza iliyochezwa Julai 6 mwaka huu Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma.

Refa Hans Mabena kutoka Tanga ndiye atakayechezesha mechi akisaidiwa na E. Mkumbukwa na Hajj Mwalukuta wote kutoka Tanga. Mwamuzi wa akiba (fourth official) ni Kessy Ngao wa Dar es Salaam.

Mechi kati ya Stand United FC ya Shinyanga na Kimondo SC ya Mbeya itachezwa Jumamosi (Julai 13 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga. Mwamuzi atakuwa Daniel Warioba kutoka Mwanza. Kimondo SC ilishinda mechi ya kwanza bao 1-0.

KALI YA LEO: TIMU KUANDIKA MAJINA YA AKAUNTI RASMI ZA TWITTER ZA WACHEZAJI KWENYE JEZI ZAO




Klabu ya soka ya nchini Ubelgiji Zulte Waregem imetoa taarifa kwamba majina ya akaunti rasmi za mtandao wa Twitter za wachezaji wa timu hiyo zitakuwa zikiwekwa kwenye jezi zao kuanzia msimu ujao wa ligi unaotarajiwa kuanza hivi karibuni. 
Klabu hiyo imetoa tangazo hilo wakati ikitambulisha jezi mpya kwa ajili ya msimu wa 2013-14. Majina ya akaunti rasmi za Twitter za wachezaji yataandikwa kwenye kaptura. 
Zulte Waregem ilimaliza nafasi ya pili katika ligi ya msimu uliopita, nyuma ya mabingwa Anderlecht. Nafasi hiyo iliwatosha kuwapa nafasi ya kushiriki katika michuano ya mabingwa wa ulaya msimu ujao 

NIGERIA WATIA AIBU KWA KUPANGA MATOKEO: VILABU VINNE VYAFUNGIWA KWA KUFUNGA MABAO 146 KATIKA MECHI MBILI - WAWEKA REKODI YA DUNIA


Vilabu vinne ambavyo vilihusika na njama ya kupanga matokeo ya mechi vimepigwa marufuku nchini Nigeria.
Katika mechi moja klabu moja iliilaza nyingine magoli 79-0 na magoli 67-0 katika mechi ya pili.
Jumla ya magoli 146 yalifungwa katika mechi hizo mbili, idadi ambayo inaingia katika vitabu vya kumbukumbu kama mechi iliyokuwa na idadi kubwa zaidi ya magoli duniani.
Klabu ya Plateau United Feeders iliilaza timu ya Akurba kwa mabao 79-0 wakati timu ya Polisi ya Machine FC kwa upande wake ikailaza Bubayaro magoli 67-0.
Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya shirikisho la mchezo wa soka nchini Nigeria, Muke Umeh amesema ufisadi na ulaghahi wa kiwango hicho hakiwezi kukubalika katika soka ya sasa.
Umeh ametangaza kuwa baada ya mkutano wa kamati hiyo, ilibainika wazi kuwa vilabu hivyo vina kesi ya kujibu na hivyo vyote vinne vimepigwa marafuku ya kushiriki katika mecho yoyote, hadi uchunguzi utakapokamilika.
Kabla ya mechi hiyo vilabu vya Plateau United Feeders na Police Machine vilikuwa na alama sawa na vilikuwa vikipania kupandishwa daraja hadi ligi daraja ya pili.
Feeders ilipata magoli 72, katika kipindi cha pili ili hali Machine nao wameripotiwa kufunga magoli 61 katika kipindi cha mechi yao.
Kufuatia matokeo hayo Plateau ilimaliza ya kwanza kwenye msimamo wa ligi na idadi kubwa ya magoli ikifuatwa na timu hiyo ya polisi.
''Tutachunguza sakata hii na kuwachukulia hatua kali wote waliohusika'' Alisema Ummeh.
Mkurugenzi wa michezo na mashindano wa Shirikisho la mchezo wa soka nchini Nigeria, Dkt. Mohamed Sanusi, amekariri tangazo lililotolewa na mwenyekiti wa kamati ya maandalizi kuwa waliohusika wataadhibiwa vikali.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na NFF, vilabu vilivyohusika, wachezaji,, maafisa wa kiufundi wa timu na wasimamizi wa mechi hiyo watakaopatikana kuhusika kwa njia moja au nyingine, katika kashfa hiyo ambayo imetajwa kuwa mbaya zaidi katika historia ya soka nchini Nigeria watachukulia hatua kali za kisheria.

Mfahamu Mkenya anayekaribia kuweka Historia kwenye English Premier League.

Victor+Wanyama+at+homeMchezaji wa kimataifa toka Kenya anayecheza nafasi ya kiungo cha kati Victor Mugubi Wanyama anatarajiwa kuweka historia ya kuwa mchezaji wa kwanza toka Nchi ya Kenya kucheza kwenye ligi kuu ya England baada ya klabu yake ya Glasgow Celtics kukubali ofa ya paundi milioni 12 toka kwa klabu ya Southampton kwa ajili ya mchezaji huyo.
Wanyama ambaye amekuwa akitafutwa na klabu kadhaa kubwa zikiwemo Manchester United , Liverpool na Arsenal amekuwa akicheza kwenye kiwango cha juu hali ambayo imemfanya kuwa moja ya wachezaji waliotajwa sana kwenye dirisha la usajili mwaka huu .
Celtics imefikia makubaliano ya kumuuza Wanyama kwenda Southampton ambapo dili la kusajiliwa kwa mchezaji huyo litakamilika mara atakapopimwa afya yake pamoja na kukubaliana baadhi ya masuala binafsi kwenye mkataba wake.
VictorWanyama
Wanyama ni mdogo wa mchezaji mwingine toka Kenya McDonald Mariga  anayecheza soka lake nchini Italia Kwenye klabu ya Parma na amewahi kuzichezea Inter Milan pamoja na Real Sociedad ya Hispania . Endapo usajili huo utakamilika Itakuwa historia nyingine kwa familia ya Mariga ambayo iliweka Historia pale McDonald alipocheza mchezo wa fainali ya ligi ya mabingwa mwaka 2010 ambapo alikuwa mchezaji wa kwanza toka Kenya na Afrika Mashariki kwa kizazi cha sasa kucheza fainali na kuvaa medali ya michuano hiyo .
Southampton itamnunua Wanyama kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 12.5 ada ambayo itamfanya Wanyama kushikilia rekodi nyingine ya kuwa mchezaji ghali kuliko wote kwenye ligi kuu ya soka ya Scotland na klabu ya Celtic.
Victor-Wanyama-scores-for-Celtic-against-Dundee-1341816

Umesikia kilichofanywa na Steve R’n'B na Mr Blue kwenye single yao ya pili kushirikiana? isikilize hapa


1


Ni uhakika kwamba baada ya kufanya ile hit ya ‘Tabasamu’ ukiambiwa leo wamefanya tena single nyingine Steve R’n'B NA Mr Blue lazima ushawishike kuisikiliza, kujua kimefanywa nini ndani…. karibu uisikilize hapa chini..

Salam za Ramadhan kutoka kwa watu mashuhuri hapa Tanzania

Ramadan_Kareem_5_by_SEiFO92
Mwezi wa Ramadhan umeanza leo watu wangu wa nguvu, kutoka jovinbachwa.blogspot.com nawatakia mfungo mwema na wenye baraka tele. Nakupa nafasi ya kusoma salaam za Ramadhan kutoka kwa watu mashuhuri hapa Tanzania.
faraja nyarandu
kitenge
lulu
mwamvita

salama

PICHA:: HUU NDIYO UWANJA WA NDEGE ALIPOKAMATWA AGNESS MASOGANGE NA MWENZIE


International-Airport-Cape-Town-OR-Tambo
JNB
SOUTH AFRICA CHANGING NAMES
O-R-Tambo-International-Airport

Hii ndio TV inayouzwa milioni 24 dukani Dar es salaam

.
.
Kwenye duka la wakala wa Samsung Mlimani City Dar es salaam unaambiwa moja kati ya TV zenye gharama kubwa kuwahi kununuliwa ni hii kubwa kabisa ya sasa hivi ambayo ina inch 75, bei yake ni milioni 24….. kwa teknolojia yake unaweza kuwa unaangalia chochote kwa kutumia miwani za 3D.
Pia ina smart content, una create account na kupata applications kibao, ni tv ambayo unaweza ku-update yani kama Samsung wakileta teknolojia nyingine kwenye Tv hutatakiwa kununua Tv nyingine bali unatakiwa kununua kadi na ku-update hiyo teknolojia mpya.
Tv ya bei ndogo kuliko zote kwa Samsung sasa hivi ni inch 19 inayouzwa laki nne na nusu ambapo Tv zinazonunuliwa na Watanzania wengi ni za inch 32, 26, 40, na 46 ambayo ni smart TV unayoweza kuitumia pia kwa kutumia Internet.
.
.
.
Hii ndio TV kubwa kuliko zote za Samsung ambayo ina inch 75, yani bei yake ya milioni 24 ni pesa ambayo kama una kipato cha shilingi elfu 30 kwa siku, kuweza kuinunua inabidi usile wala kunywa au kufanya chochote kwenye hiyo elfu 30, uikusanye kwa siku mia nane (800)
.
.
Baada ya kukupa hiyo info kutoka Dar es salaam, kwa sasa zichukue hizi info nyingine kuhusu historia ya TV duniani…
1. Mwaka 1926 J.L BAIRD alitengeneza TV ya kwanza ambayo uwezo wake wa kuonyesha ulikua wa kiwango cha mistari 30 tofauti na TV za sasa zenye mistari mpaka 1080 ambayo ni high definition.
2.TV ya Panasonic ya Inch 150 ndio TV kubwa kuliko zote kwa sasa ambayo gharama yake ni dola laki moja za Kimarekani sasa hivi, pesa ambayo kibongobongo ni zaidi ya milioni 150.
3.Tangazo la kwanza kwenye TV liliruka hewani kwa mara ya kwanza siku ya kwanza ya July mwaka 1941 na lilihusu mechi ya mpira wa Baseball Marekani kati ya B. DODGERS NA PHILADELPHIA PHILLIES na lilikua la sekunde 20, gharama yake wakati huo ilikua dola 9 za Kimarekani ambayo kwa bongo ni zaidi ya shilingi elfu 10.
4.Kwa Marekani, watoto mpaka kufikia umri wa miaka 14 wanakua wameshuhudia matukio elfu kumi na moja ya mauaji kupitia TV.
5. Kipindi cha miaka ya 1950 kilifahamika kama zama za dhahabu kwa Televisheni, ni wakati ambapo matangazo ya kwanza ya rangi yaliruka, kabla ya hapo yalikua yanaruka ambayo ni black and white.
6.Remote ambazo hutumika kubadilishia channel na vitu vingine kwenye TV zilianza kutumika kwenye miaka ya 1980.
7. Matukio yaliyoweka rekodi ya kutazamwa sana kwenye TV ni michezo ya Olympic na michuano ya FIFA ya kombe la dunia.
8. Mwishoni mwa vita kuu ya pili ya dunia, Televisheni iligeuka kuwa rahisi kwenye umiliki kwa yeyote anaeweza kumudu gharama za kuinunua.

Hii ndio picha ya kwanza ya Amber Rose na Wiz Khalifa baada ya kufunga ndoa.

.

.
Mastaa Amber Rose na rapper Wiz Khalifa wamefunga ndoa rasmi jana July 8 2013 na sasa ni Mr.  and Mrs. Thomaz ambapo muda mfupi baada ya ndoa Amber alitweet “Yay me and my baby are officially married!!!” na kuweka hiyo picha instagram iliyokua na maneno yanasema 

 “Happily ever after.”

TWEETS ZA AMBER & WIZ KHALIFA ZATHIBITISHA WAWILI HAO KUFUNGA NDOA


Usiku wa kuamkia leo tarehe 9/7/2013 majira ya saa 8 usiku
 kwa majira ya saa za afrika mashariki
niliona kupitia mtandao wa facebook,msanii
wa hip-hop Wiz khalifa akiandika kupitia page yake ya facebook iliyokuwa
verified  kuwa
 yeye na mama watoto wake mwanamitindo
Amber Rose wamefunga ndoa tarehe 8/7/2013....!!
Katika hali ya kuwaacha mashabiki zao katika sintoamini leo
 majira ya mchana walirudia tena  majira ya saa nane kwa muda
wa saa za afrika mashariki wawili
hao walipost kwa upande huu,alianza Amber Rose mama wa mtoto mmoja
 aliyezaa na Rapper huyo kuandika
kupitia mtandao wake wa Twitter na Instagram kuwa
 amefunga ndoa na Mpenzi wake huyo
baba wa mtoto wake....

Zicheki Tweets hizi za Mastaa hawa ambao ndoa yao imekuwa ya
 ghafla ghafla tofauti na ilivyotegemewa
kama mastaa wengine ujipanga na kualika watu maarufu kusherekea
siku nzuri na muhimu ya maisha ya
mwanadamu....!!

ZITTO KABWE AWATAKA WANANCHI WAGOME KUILIPA KODI YA SIMU YA SH. 1000.....AMEDAI KUWA KODI HIYO ILIPITISHWA KINYEMELA



Sakata  la  kodi  ya  line  ya  simu  limeendelea  kuwakuna wanasiasa  wetu  ambao  wamekuwa  wakifunguka  kwa  nyakati  mbalimbali  kupitia mitandao  ya  kijamii....

Baada  ya  January  Makamba, Zitto  kabwe  naye  amefunguka  na  kudai  kuwa  kodi  hiyo  ni  batili  na  ilipitishwa  kinyemela  kwa  sababu  ilikuwa  imeshaondolewa....

Huu  ni  ujumbe  wake  aliouweka  katika  account  yake  ya  facebook:

Baada ya  kauli  hiyo,Zitto  Kabwe  aliandamwa  na  maswali  mengi  sana  toka  kwa  wananchi  wakidai  kuwa  "Makamba  alisema  tuwalaumu  ninyi  maana  ninyi  wabunge  ndo  mlibariki  kodi  hii"

Zitto  naye  alishindwa  kulijibu  swali  hilo  na  kuwataka  wananchi  "wachukue  simu  zao, wawapigie  wabunge  wao  wawaulize  ni  kwa  nini  walipitisha  kodi  hii"

 "Anasema  hiyo  kwa  sababu  wabunge  ndio waliopitisha.Wabunge  ndio  wawakilishi  wa  wananchi.Jambo likipita bungeni hao ndio wa kwanza kulaumiwa.Yupo sahihi kabisa.Mpigie mbunge wako simu muulize kwa nini  alikubali au  hakupinga kodi hii"..Hili  ni  jibu  za  Zitto Kabwe

JAMIE FOXX AWA MTU WA KWANZA KUFANYIWA INTERVIEW NA OPRAH KWENYE KITUO KIPYA CHA OWN


Ni muda mrefu toka mwanamama Oprah Winfrey kuachana na
Tv Talk show na kuamua kufungua
kituo cha Televisheni kiendacho kwa jina la 'OWN' kinachorusha
matangazo ya aina mbalimbali
Mwanzoni mwa mwaka huu....
Tokea kituo hicho kianze kufanya kazi hizo akikuwahi
kurusha inrterview na mtu yoyote maarufu
duniani kama ilivyokuwa kwenye kipindi cha Oprah...
Lakini jana usiku wa tarehe 8/7/2013,ilikuwa Exclusive
Interview ya kituo hicho
na usiku huo ilikuwa Interview na JAMIE FOX mwigizaji
maarufu na msanii wa kuimba mkubwa marekani...!!
Katika Mahojiano hayo yaliusisha maisha yake ya ndani na
muziki anaofanya,na sanaa ya uigizaji na pamoja na
skendo iliyomkumbaa hivi karibuni ya kutembea na mke wa
mchezaji kikapu wa marekani
Kelvin Durant....
Pia aliweza kuzungumizia mafanikio yake aliyopata ndani ya mwaka jaa
hadi mwaka huu kwenye televisheni ya 'OWN'

Jamie Fox ndie mtu maarufu wa kwanza kufanyiwa mahojiano
 kwenye kituo hicho cha
mwanamama mwenye pesa zaidi kuliko wote dunia...

"NITAENDELEA KUPAMBANA NA WABISHI WASIOTAKA KUHAMA ILI KUPISHA MIRADI YA UJENZI"...MAGUFULI


WAZIRI wa Ujenzi, Dk. John Magufuli ameapa kupambana kwa kuwabomolea au kuwakomesha kwa njia nyingine, watu waliogoma kuhama kwa ajili ya kupisha miradi mbalimbali ya ujenzi inayotekelezwa na wizara yake.

Katika hilo, tayari amekwishatangaza uamuzi mzito wa kuruhusu kampuni ya ujenzi ya Jaspal Singh, kujenga barabara kwa kiwango cha lami kwa kuzizunguka nyumba za wakazi waliogoma kuhama na kukimbilia mahakamani akiamini kuwa wataondolewa kwa kugongwa na malori yatakayokuwa yakipita baada ya barabara hiyo kukamilika.

Pamoja na hilo, Dk. Magufuli amesema atazibomoa bila kulipa fidia nyumba za wananchi nane waliokataa kufanyiwa tathmini ili kupisha mradi wa ujenzi wa daraja la Kigamboni, endapo hawatabadili msimamo wao huo.

Uamuzi huo aliutangaza jana baada ya kufanya ziara ya kutembelea miradi mbalimbali katika Jiji la Dar es Salaam, ambapo alibaini kuwa miradi mingi inakwamishwa na wananchi wa maeneo husika.

Akiwa katika mradi wa ujenzi wa barabara ya Kigogo hadi Jangwani yenye kilomita 2.7, alishangazwa kuona mradi umesimama huku vifaa vikionekana kuwa na kutu kitendo ambacho kilimlazimisha ahoji.

Mhandisi Mshauri wa mradi huo, Mussa Ali pamoja na Mkandarasi Jaspal Hungh, walimueleza Magufuli kwamba kuna wananchi wenye nyumba 16 wamechukua fidia na kufungua kesi mahakamani kwa kudai kiasi walichopewa ni kidogo.

Aliongeza kuwa kesi hiyo imechukua zaidi ya miaka miwili bila kutolewa hukumu na kusababisha mradi kukwama.

TAMKO LA KIGOGO

Akizungumzia hilo Magufuli alisema: “Naomba tusiingilie mahakama lakini naagiza kuanzia leo (jana), anzeni kujenga barabara ya lami kwa kuzizungushia lami nyumba hizo na kuruhusu gari zipite, nadhani haitapita wiki kabla hazijagongwa na malori ya mchanga, sitaki kusikia Serikali inadaiwa fidia ya ucheleweshaji wa mradi.

“Pia naagiza kwamba mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki kwamba meneja wa mradi fungua kesi dhidi ya wananchi hao waliochukua fedha za fidia na kwenda mahakamani, huo ni wizi.

“Serikali ikishinda kesi ya madai yao ya fidia ndogo, wao ndio watawajibika kujenga sehemu ya nyumba zao, hatuwezi kuchezea fedha kwani kuwafidia Sh bilioni 3.8 ambapo mradi wenyewe unagharimu Sh bilioni 7.6.

“Kuna mazoea yameibuka ya watu kuchezea Serikali na mahakama, sasa nasema katika miradi ya wizara yangu nitapambana nao watu wenye kiburi cha kuchezea vyombo hivyo,” alisema.

DARAJA L A KIGAMBONI

Awali akitembelea eneo la Kigamboni uliko mradi wa daraja la Kigamboni, Magufuli aliwataka wananchi nane waliokataa kufanyiwa tathmini ya nyumba zao ili kupisha mradi huo, kubadili msimamo wao haraka kabla ya Serikali haijazibomoa nyumba hizo kwa nguvu tena bila kulipwa.

Jumla ya watu 121 walitakiwa kuhama kupisha mradi huo ambapo kati yao 113 walikubali kufanyiwa tathmini na kulipwa jumla ya Sh bilioni 11.7, lakini nane walikataa.

“Nasema Serikali ikiamua kufanya ukorofi utakuwa mkubwa kuliko msimamo wako, sasa nasema hao waliokataa kufidiwa naomba wasiambulie patupu kabla hatua hazijachukuliwa, wakubali kuchukua kiasi kitakachothaminiwa haraka, sisi tukija tutabomoa na hatukulipi na mradi utaendelea.

“Naomba daraja hili likamilike na kukabidhiwa kwa Rais Jakaya Kikwete Januari 31, 2015 na kulifungua, sitaki kuona linafunguliwa na rais mwingine ambaye anaweza kusema yeye ndiye aliyejenga wakati ni uongo, aliyeweka jiwe la msingi ndiye atakayefungua,” alisema.

Mradi wa daraja la Kigamboni unagharimu Sh bilioni 214 na kati hizo asilimia 40 zinatolewa na Serikali wakati Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), unachangia asilimia 60.

Mbali na hilo, Dk. Magufuli ameagiza kuondolewa haraka wakazi wa eneo la Davis Corner, Temeke ambao licha ya kulipwa fidia ili kupisha ujenzi wa barabara ya Jet Corner hadi Temeke, wameshindwa kuhama mpaka sasa na badala yake kutumia fedha hizo kuendeleza ujenzi na kudai malipo mengine.

Magufuli alishangazwa kuona wananchi hao ambao wamegoma hadi sasa wamelipwa fidia Sh 15.8 huku mradi wenyewe ukiwa Sh bilioni 12 na barabara ikiwa haijakamilika.

Mradi wa mabasi ya kasi

Akikagua mradi wa mabasi yaendayo kasi jijini Dar es Salaam (DARTS), Magufuli alifurahishwa na kasi pamoja na kiwango cha ujenzi wa mradi huo, ambao utapunguza msongamano wa magari.

Meneja wa mradi wa Darts, Baraka Ally alimweleza Dk. Magufuli kwamba mradi unaendelea vizuri na utakamilika kwa wakati uliopangwa.

Hata hivyo alisema changamoto kubwa inayoukabili mradi huo ni uvamizi wa wafanyabishara ambao wamekuwa wakiweka biashara zao barabarani huku wenye teksi na magari mengine wakiegesha eneo la mradi.

Vile vile alisema kuwa kuna hatari kubwa ya Jiji la Dar es Salaam kukumbwa na harufu kali kutokana na wakazi wanaoishi karibu na barabara kujiunganishia kinyemela mabomba ya maji machafu na mifereji ya mvua.

Magufuli aliagiza watu wote wanaokwamisha mradi huo kuchukuliwa hatua kali, ikiwa ni pamoja na halmashauri kuwajibika katika hilo.


MTANZANIA

Pichaz na Video za yaliyomkuta Rihanna akiwa beach na jinsi alivyolewa hadi kushindwa kutembea


1464899-rihanna-lakers-game-photos-of-the-week-617-409
Bad girl RiRi alikuwa Poland siku kadhaa zilizopita na kilichotokea huko kimekuwa headline kama kawaida yani, alikuwa kwenye moja ya concert zake Ulaya lakini katika siku kadhaa alizokuwa Poland alitumia muda wake pia kwenye beach kupunga upepo lakini kituko cha kwanza kilichomkuta ni pale alipokwenda beach na kujikuta anazungukwa na watu kama Simba akiwa Zoo.
Watu wengi walikuwa wamezunguka kumuangalia Rihanna akiwa Beach…. yani tengeneza picha wewe unakwenda beach alafu watu kama hivi wanakuzingira kukuangalia tu umepumzika….
ifwt_rihanna4
Watu wakimshangaa Rihanna akiwa Beach
ifwt_rihanna-1
Tweet ya Rihanna akizungumzia yaliyomkuta Beach
Siku nyingine Rihanna akiwa hukohuko Poland bata likahamia kwenye concert na inadaiwa kwamba alitoka kwenye club hiyo akiwa amelewa kiasi cha kushindwa hata kutembea, cheki hii video hapa chini inayomuonyesha Rihanna akijaribu kutembea lakini anashindwa hadi anasaidiwa na msaidizi wake…..
Siku nyingine Rihanna akiwa hukohuko Poland bata likahamia kwenye concert na inadaiwa kwamba alitoka kwenye club hiyo akiwa amelewa kiasi cha kushindwa hata kutembea, cheki hii video hapa chini inayomuonyesha Rihanna akijaribu kutembea lakini anashindwa hadi anasaidiwa na msaidizi wake…..

rihanna-sopot-poland-jacquie-aiche-body-chain-fleet-ilya-visor-rihanna-for-river-island-skirt-mikoh-mundata-top-miu-miu-sandals
Rihanna akiondoka Beach baada ya mambo kuwa magumu

Matatu za Kenya a.k.a daladala zimekuja na ubunifu wa huduma mpya aisee


Nairobi - Kenya - East Africa
Ukiwa kwenye jiji la Nairobi na ukaona magari yamechorwa rangi tofauti na graffiti, basi hizo ni daladala zao jijini Nairobi maarufu kama Matatu ambapo sasa hivi wamiliki wake wamekuja na ubunifu mpya ambao unawasaidia katika kufanya biashara zaidi na kuvutia wateja wengi sana.
Mtu wangu wa nguvu najua internet ni moja kati ya huduma unazotumia kila  siku na imekuwa inatumika kama kivutio cha biashara pia kwenye sehemu kadhaa ya biashara kama kwenye migahawa, Bar au Night club kwenye nchi zilizoendelea utakutana na internet ya bure kupitia WiFi. Basi wenzetu wa 254 Kenya wameanza kupiga hatua mbele kwenye kitu hiki baada ya matatu zao kuanza kutoa free internet kwa kutumia WiFi. fikiria na foleni hizi zilizopo Dar kama daladala zingekua na internet ya bure ndani yake watu wasingeuona ukali wa foleni kabisa… bila kusahau uhakika wa kufanya biashara ungeongezeka kwa sababu watu wengine wangechagua daladala zenye internet yenye speed. ukiwa katika jiji la Nairobi na simu yako ikiwa ina support WiFi, ukipanda matatu ni kama upo nyumbani au kazini. abiri wengi hivi sasa hutumia muda wa asubuhi kuelekea ofisini huku wakiangalia habari mbalimbali kwenye simu zao na kupitia mitandao ya kijamii..
Hivi sasa makonda wa matatuu wanaita abiria kwa kuongezea kionjo cha internet ya bure ipo, kwa mfano hata Dar kungekua na hiyo huduma ungemsikia konda tu anasema “Kariakoo Sokoni hiyoo mia nne na internet yenye kasi bureee”

Chidy Benz azuia kutoka kwa video ya ngoma aliyoshirikishwa


972201_584553924917440_1798184707_n
Hivi karibuni  msanii Baghdad ambaye alikuwa na umbo kubwa sana na kupungua ghafla, alitoa ngoma yake mpya akishirikiana na wasanii wawili ambao inasemekana kwamba hawana mahusiano mazuri. Wasanii hao ni Chidy Benz na Ney wa Mitego, kwa pamoja walishiriki kwenye ngoma moja ya Baghdad bila kujua kama wapo kwenye ngoma moja. Baadaye kutokana na  ratiba zao tofauti wakafanya video siku tofauti na katika location tofauti lakini kwa ajili ya ngoma moja hiyohiyo. Baghdad baada ya kuachia audio yake ambayo ilipata attention baada ya kusikika kwamba Ney wa Mitego na Chidy Benz wapo kwenye ngoma moja.
Habari kutoka kwenye chanzo cha uhakika zinasema kwamba Chidy Benz kutokana na kutokuwa na taarifa juu ya collabo hiyo, amepiga stop kutoka kwa video yake. Source ya story hii inaendelea kuhabarisha kwamba kuna mazungumzo yanafanyika na Chidy Benz kupata njia nzuri ya kuitoa video hiyo baada ya kuweka mambo kadhaa sawa kwenye maongezi hayo.


1044191_580378118668354_1069630180_n
Chidy Benz akiwa Maisha Club ambayo ni location iliyotumika kufanya video hiyo kwenye part ya Chidy.

1044861_580381218668044_2084355953_n
Ney wa mitego akiwa location Mbezi kwenye sehemu ambayo ili-rekodiwa part ya verse yake
Kama ulikuwa haujawahi kusikiliza ngoma yenyewe mtu wangu wa nguvu, chukua nafasi ya kusikiliza hapa

50 cent apata kashfa nzito ya kumtumia mwanaye wa kiume sms zenye lugha chafu.


FilmDistrict With The Cinema Society, L'Oreal Paris & Appleton Estate Host A Screening Of "Parker" - Inside Arrivals
Msanii Curtis Jackson maarufu kama 50 cent wa crew ya G unit hawezi kusahau siku kadhaa zilizopita baada ya kuandamwa na mambo mengi mabaya na bado yameendelea kumkuta. Wiki iliyopita ilisemekana kwamba 50 cent amekamatwa na polisi kwa kosa la kumshambulia mwanamke ambaye amemzalia mtoto wa pili japokuwa 50 cent hakuwahi kusema kwamba ana mtoto wa pili. Lakini 50 cent alijibu kupitia instagram kwa kutumia neno “am not in jail am in” na kumalizia eneo alipo kwa mfano am not in jail am in my living room kama ulivyosoma kwenye stori iliyopita ya 50 cent hapahapa.

Baada ya kashfa hiyo ya kumshambulia baby mama wake, 50 cent alitoswa kufanya show ya MLB. Mambo yanazidi kumuendea mrama 50 cent, hivi sasa kwenye internet habari kubwa ni kuhusu msanii huyu kumtumia sms zenye lugha chafu mtoto wake wa kiume ambaye ana miaka 16 tu. Hivi sasa  Marquise ambaye ndiyo mtoto wa 50 cent anaishi na mama yake na wakati anachat na baba yake ambaye alimtupia maneno machafu sana alikuwa nyumbani kwa mama yake.
Baada ya hizi screen shot za maneno ambayo msanii huyu alimtumia mwanaye na baadaye zikavuja kwenye internet, 50 cent aliingia kwenye ukurasa wake wa twitter na kuandika kwamba aliyekuwa anajibu hizo sms ni mama yake  Marquise ndiyo alikuwa anajibu na siyo mtoto huyo. Hakuishia hapo lakini aliendelea na kusema kwamba baada ya maongezi yale,  ameamua kwamba Marquise sio mtoto wake tena na anamtoa kwenye list ya watu atakao wapa urithi wake. 50 cent akazidi kungezea kwamba anahitaji kufanya DNA test kuhakikisha kama huyu mtoto ni mwanaye kweli au la, kwasababu anawasiwasi kama mama yake Marquise alim-cheat kipindi hicho wanapata huyu mtoto.
Baadhi ya mitandao imehoji kuhusu haya maneno machafu ambayo 50 cent ameyatuma kwa mtoto mdogo wa miaka 16 tu, pia kwa nini amemtoa kwenye list ya urithi wake kisa ameonyesha kutokuwa na heshima kwa baba yake wakati baadaye 50 cent ame-tweet kwamba  aliyekuwa anajibu ni mama yake na sio Marquise. So hakuna sababu ya kumfuta  Marquise kwenye list ya watu watakaopata urithi kwa kumkosea heshima baba yake ikiwa aliyekuwa anajibu zile sms ni mama yake.
article-2358210-1AB6BE19000005DC-772_634x940
Marquise na mama yake

Hizi ndiyo screen shoots za sms alizotuma 50 cent kwenda kwa mtoto wake ambazo hadi sasa 50 cent hajakataa kama sio sms zake bali alichokisema ni kwamba aliyekuwa anajibu hizi sms ni mama yake Marquise akitumia simu ya Marquise screen-shot-2013-07-08-at-9-40-58-am 1 2 3 4 5 6 7 8 9

50textbbbb

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...