facebook likes

Saturday, July 20, 2013

Okwi, Patrick Ochan waomba kurudi Simba

PATRICK Ochan na Emmanuel Okwi wamefanya uamuzi wa kushangaza baada ya wote wawili kuomba kurudi kuichezea Simba ya jijini Dar es Salaam.
Ochan, kiungo aliyeuzwa na Simba kwenda TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa kiasi cha dola 100,000 
anataka kurudi Msimbazi haraka iwezekanavyo kwa uhamisho wa mkopo baada ya kuchoshwa na maisha ya Lubumbashi.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na Mwanaspoti, Ochan mwenye umri wa miaka 27, ameonyeshwa kukerwa na lundo la wachezaji mahiri na wasio mahiri ndani ya TP Mazembe ambalo limesababisha akose namba ya kudumu klabu hapo.
“Nataka kurudi Simba kwa mkopo, nimechoshwa na maisha ya Mazembe. Tajiri (Moise Katumbi) anarundika wachezaji wengi hapa na nafasi ya kucheza imekuwa ngumu. Waambie watu wa Simba nataka kurudi klabuni kwangu kwa mkopo. Mwambie Kaburu (Geofrey-aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Simba) nataka kurudi Simba,” alisema Ochan.
Ochan amekiri kwamba mara kadhaa amejaribu kuihama Mazembe ikiwemo kutaka kutimkia Afrika Kusini kuichezea timu ya Golden Arrows, lakini Katumbi ametia ngumu.
“Kuhama kwa mkopo inawezekana. Nitazungumza na viongozi huku nadhani inawezekana kabisa kwa sababu watataka nipate muda wa kucheza. Baada ya wiki mbili nitakuja Uganda. Kwa kweli nataka kurudi zangu Simba,” alisema Ochan ambaye aliuzwa pamoja na Mbwana Samata wakitokea Simba.
Katika hatua nyingine, Emmanuel Okwi naye amempigia simu mmoja ya viongozi wa Simba na kuomba arudi Msimbazi.
Okwi, ambaye yupo jijini Kampala akiwa amesusa kwenda Etoile du Sahel kwa mwezi moja sasa, ameomba kurudi Simba kwa madai kuwa amekuwa hapewi nafasi ya kucheza, lakini mbaya zaidi amekuwa halipwi mshahara na hajamaliziwa fedha zake za kusaini mkataba wa miaka mitatu.
“Ni kweli amepiga simu kuomba tumrudishe Simba, lakini tukifanya hivyo tutakosa Sh 480 milioni ambazo tunawadai Etoile,”alisema kiongozi mmoja wa Simba. Kiongozi huyo alisema kinachoweza kufanyika ni klabu hiyo ya Tunisia angalau iwalipe Sh 300 milioni halafu Okwi aje Simba kucheza kwa mkopo.
Mwanaspoti ilimtafuta Okwi kwa simu jana Ijumaa, lakini simu yake ya mkononi ilikuwa inaita bila kupokewa.
source mwanaspoti

ANGALIA PICHA KANYE WEST AKIMPIGA PAPARAZI



Kanye was on his way out of the airport when he went ballistic, attacking a member of the paparazzi at LAX.......

Angalia PICHA mh,MWIGURU NCHEMBA AKIWA NA FAMILIA YAKE NYUMBANI KWAKE


BREAKING Newzzzz....MSANII WA MAIGIZO MR.BOMBA ALIYE TAMBA SANA NA MAIGIZO MBALIMBALI ITV AFARIKI DUNIA


Leo katika pita pita zangu kwenye ukurasa wa FB wa msanii wa bongo muvie Batuli, nimekutana na habari hii ya majonzi ya kuondokewa na msanii mahiri wa maigizo na bongo muvi hapa nchini, Batuli ameandika maneno haya hapa chini
R.I.P baba yetu Mr Bomba Mwenyezi Mungu aiweke roho yako mahala pema peponi "Amin"

Rais Kikwete akutana na Professa Lipumba ikulu Jijini Dar es Salaam

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete jana alikutana na Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF)Profesa Ibrahim Lipumba na kufanya naye mazungumzo ikulu jijini Dar es Salaam.Mazungumzo hayo yalihusu masuala mbalimbali ya siasa na uchumi nchini.Pichani Rais Kikwete akiwa na Professa Lipumba katika nyakati tofauti  ikulu jijini Dar es Salaam
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF)Profesa Ibrahim Lipumba 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimsindikiza Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF)Profesa Ibrahim Lipumba baada ya mazungumzo yao

MR. NICE APATA SHAVU JINGINE NCHINI KENYA BAADA YA KUTEMWA NA GRANDPA



Ikiwa ni zaidi ya mwezi mmoja toka staa wa Bongo Luca Mkenda aka Mr Nice apoteze nafasi ya kufanya kazi na label ya GrandPa ya Kenya kwa shutuma za uvivu, kushindwa kutoa ushirikiano na ukiukaji wa mkataba hatimaye mlango mwingine umefunguka kwa nyota huyo wa ‘Kikulacho’.



Mr Nice ambaye bado yuko Kenya anatarajia kujiunga na label nyingine nchini humo ‘Candy Records’ ambayo ina miezi michache toka ianzishwe. 


Kwa mujibu wa CEO wa label hiyo John Kariuki aliyekuwa akizungumza katika ufunguzi rasmi wa label hiyo jijini Nairobi, alisema wako katika hatua za mwisho kukamilisha mpango wa Mr Nice kusain mkataba nao kama ilivyoripotiwa na Niaje.



Label hiyo tayari imesha wasain wasanii kadhaa wa Afrika Mashariki akiwemo hit maker wa ‘Ulofa’ Top C wa Tanzania, pamoja na wengine kutoka Kenya.

MMILIKI WA HOME SHOPPING CENTRE AMWAGIWA TINDIKALI



Taarifa za awali zinadai kwamba Mfanyabiashara Said Mohamed Saad ambaye ni Mmiliki wa Home Shopping Centre (Dar), amwagiwa tindikali  saa mbili  ya usiku  huu maeneo ya Msasani City Mall ....

Taarifa  hizo  zinadai  kwamba  mtuhumiwa  aliyefanya kitendo hicho alitoka mbio, mlinzi akamkimbiza lakini bahati mbaya akateleza na kuanguka na jamaa akawahi pikipiki na kutoweka eneo la tukio

BAADA YA JANUARI MAKAMBA KUDAI KUWA MNYIKA NI "MNAFIKI".....ZITTO KABWE NAYE AMEAMUA KUINGILIA KATI MZOZO HUO


Hizi  ni  tweets  za  viongozi  wetu  wakitupiana  lawama  kuhusu  swala  la  kodi  ya  line  kiasi  cha  kuitana  "MNAFIKI"....
 January Makamba on Mnyika acha unafiki July 19 2013


HIKI NDO KICHAPO WANACHOPEWA WAASI WA M23 NA JESHI LA KONGO ( FARDC )


 Goma -DRC.
WAKATI mapigano yakizidi kuwa makali kati ya wanajeshi wa DR Congo (FARDC) na kundi la waasi wa M23, wanajeshi wa DRC wako hatarani kushitakiwa kwa tuhuma za kuwatesa waasi na kunajisi maiti zao.
 
Wanajeshi hao wanatuhumiwa kwa kosa la kukiuka haki za binadamu na sheria za Umoja wa Matifa (UN) inayokataza ukiukwaji wa haki za binadamu huku ukikataza watuhumiwa na mateka wa kivita kufanyiwa vitendo vyovyote vinavyo ashiria kukiuka haki zabinadamu badala yake mateka wote wanatakiwa kushtakiwa kwa muujibu wa sheria.

 Maiti ya muasi wa M23 ikinajisiwa na Askari wa Congo,baada ya kukamatwa, kuteswa hadi kufa katika mapigakano yanayoendelea maeneo ya Kivu na Goma nchini Congo.

Msemaji wa Katibu Mkuu wa UN Ban Ki-moon alisema kwamba, Umoja huo umeonyesha wasiwasi kuhusu taarifa ya kutokutendewa haki kwa wafungwa wa M23 na kunajisiwa kwa maiti ya wapiganaji wa M23 baada ya kukamatwa na vikosi vya silaha.

Alisema watuhumiwa wa M23 walifanyiwa vitendo vibaya na askari wa DRC mbele ya raia bila ya kuzingatia Sera ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu na kwamba watuhumiwa waliohusika katika matukio hayo watafanyiwa uchunguzi wa kina.

Wanajeshi wa DRC wakiinajisi maiiti ya muasi wa M23 baada ya kukamatwa na kupigwa hadi kufa mbele ya raia

Wanajeshi wa DRC wakiendeleza mateso makali kwa waasi wa kundi la M23 mpaka kifo kinapowafika wakiwa uraiani


Wanajeshi wa DRC wakiwa wamemfunga mpiganaji wa kundi la M23 nyuma ya gari na kumpitisha mitaani.


 Wanajeshi wa Congo wakimfunga askari wa kundi la M23 mbele ya raia baada ya kukamatwa

 
 Wanajeshi wa DRC wakimtembeza muasi wa kundi la M23 mitaani baada ya kukamatwa.

Credit: Habari mpya

PICHA ZA USHUHUDA WA WANACHAMA 5 WA CUF WAKIELEZA JINSI WALIVYOTESWA NA ASKARI HUKO MTWARA


 Baadhi ya Viongozi wa Chama cha Wananchi (CUF) kutoka (kulia) ni, Mwenyekiti wa Vijana Wilaya ya Mtwara Mjini, Ismaili Njalu. Katibu wa Wilaya ya Mtwara mjini, Said Kulanga na Mwenyekiti wa Wilaya ya Mtwara mjini, Salum Mohamed wakiwaonesha waandishi wa habari majelaha waliyoyapata baada ya kupigwa na Wanajeshi wa Wananchi (JWTZ) katika mkutano uliofanyika Makao Makuu ya Chama hicho Dar es Salaam.

--------------
CHAMA cha Wananchi (CUF) kinaandaa utaratibu wa kufungua kesi mahakamani dhidi ya ukiukwaji wa haki za binadamu uliofanywa na Wanajeshi wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kwa watendaji wa chama hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Naibu Mkurugenzi Mipango, Uchaguzi wa Bunge Shaweji Mketo,kwa niaba ya wanachama wenzake alisema, bado wanawasiliana na wanasheria, taasisi za haki za binadamu na mamlaka nyingine ili kupata mwongozo waweze kufungua kesi hiyo.

Mketo na wenzake watano, ni miongoni mwa watu walioonja joto ya mateso ya siku 28 kutoka kwa askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), ambao wameweka kambi Mtwara kudhibiti machafuko yanayotokana na madai ya kuzuia bomba la gesi asilia lisijengwe Dar es Salaam.

Mbali na Mketo wengine ni Mwenyekiti wa Vijana Mtwara mjini Salum Mohamed, Mwenyekiti wa Mtwara mjini Salum Mohamed, Mwenyekiti wa Wilaya Mtwara vijijini Ismail Jamal,Katibu wa Wilaya Mtwara mjini Said Kulaga na dereva wa CUF makao makuu Kashinde Juma.


Naibu Mkurugenzi Uchaguzi na Mipango wa CUF, Shaweji Mketo akifafanua jambo kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu kuteswa kwa wanachama watano wa chama hicho na askari wa JWTZ mkoani Mtwara. 
 -----
Akisimulia mkasa huo uliompata yeye na wenzake alisema wakiwa njiani walikutana na gari mbili za jeshi kubwa na ndogo zikiwa njia panda ya newala na mtwara mjini,na kuwasimamisha huku walitokea askari wapatao 50 vichakani na kuanza kuwapiga huku wakiwasachi mifukoni.

“Askari wa JWTZ walikuwa 50 walitusachi na kuchukua fedha zangu shilingi 85,000 na nilipoanza kuzuia fedha hizo wasizichukue ndipo walipoanza kunipiga kweli wakanivua viatu vyangu nilivyowahi kununua nje ya nchi wakavichukua na mimi kuniachia vyao vya jeshi hivi hapa ,”alieleza Mketo.

Alisema walikuwa wakipigwa na fimbo, kumwagiwa maji yaliyokuwa yamewekwa barafu na pilipili jambo ambalo liliwafanya waendelee kupata maumivu makali sana.

Mketo alisema hata hivyo kuteswa kwao ni ishara kuwa Mtwara bado inanuka damu na hakuna usalama huku wananchi wengi wakihofiwa kufariki dunia.

Hata hivyo alisema wakati wakiendelea kuwatesa alisikika mwanajeshi mmoja akisema wao wapo pale kwa ajili ya kutekeleza amri ya Waziri Mkuu aliyoitoa Bungeni kwamba wananchi watakaokaidi amri ya serikali wanatakiwa kupigwa.

Kiongozi huyo ambaye aliongea kwa masikitiko makubwa huku akiwataka wenzake kuonesha majereha kwa wanahabari alisema kuwa licha ya kuwaambia wanajeshi waliokuwa wakiwatesa kuwa amefanyiwa upasuaji mkubwa wasimpige eneo hilo hawakujali kwani waliendelea kumchapa na bakora katika eneo la mshono hadi lilipogeuka rangi na kuwa nyeusi.

Alisema kiongozi mmoja ambaye ni Mwenyekiti wa Mtwara mjini Salum Mohamed aliambiwa azivute ndevu zake kwa kutumia mikono na alifanya hivyo hadi haapo zilipoanza kuvuja damu ndipo wakamwambia walichokuwa wanakihitaji.

Mketo alisema vitendo hivyo ni vya kinyama na kwamba haviwezi kuvumilika hivyo serikali inatakiwa kuviangalia utendaji kazi wa vyombo vya dola kwani ni kulinda raia na si kutesa.

Hata hivyo aliilaumu serikali kwa kuvifungia vyombo vya habari mkoani humo kwa kigezo cha kwamba vinawashawishi wananchi kuandamana jambo ambalo si kweli.

MUME AZIMIA BAADA YA MKE WAKE KUNASWA AKIJIUZA


Mume na mke wakiongea

Seleman Yasin (78), mkazi wa Mtaa wa Mtamba, Msasani jijini Dar es Salaam, juzi Alhamisi alizimia  baada ya kupata taarifa za mkewe, Saida Abdalah ‘Mama Hamisi’ (21), kunaswa kwa tuhuma za ukahaba na kupandishwa kizimbani kwenye Mahakama ya Jiji.

Imedaiwa mahakamani hapo kuwa Mama Hamisi alinaswa kwenye msako wa machangudoa uliofanyika usiku wa kuamkia juzi maeneo ya Buguruni.



Akiwa kizimbani, Mama Hamisi alisomewa shitaka la kujiuza na mwendesha mashitaka wa mahakama hiyo, Richard Magodi mbele ya Hakimu Timoth Lyon.


Baada ya kusomewa shitaka lake, Mama Hamisi na makahaba wengine 13, walikana kufanya biashara hiyo kesi ikaahirishwa hadi Julai 31, mwaka huu.

 mume akichambua nguo za mkewe

Hakimu Lyon aliwaambia washitakiwa kuwa dhamana iko wazi ndipo akatokea mume wa Saida ‘Baba Hamisi’ na kujitambulisha kisha kuanza kuhangaikia dhamana ya mkewe ambaye wakati huo tayari alikuwa nyuma ya nondo.
 

“Yaani we Mama Hamisi kila siku unanidanganya unauza ubwabwa, Buguruni kumbe ubwabwa wenyewe ndio huo! Akafyatua tusi,” Baba Hamisi.

“Kila siku mimi nalala nyumbani na watoto wewe unarudi alfajiri unanidanganya unauza ubwabwa!
 

“Mimi machale yalishawahi kunicheza kipindi fulani sema nilikuwa nakuvizia lakini leo Mungu kanionesha ,” alisema Baba Hamisi.
 

Licha ya kupandwa na jazba lakini mtu chake, Baba Hamisi alituliza jazba na kutaka kumchomoa kipenzi chake kwa dhamana lakini alishindwa kutimiza masharti.

Kwa kuwa Baba Hamisi alikuwa na safari ya muhimu ya mkoani ikabidi aondoke na kumuachia nguo za sikukuu alizonunua kwa ajili ya mtoto wao, Hamisi.


Akizungumza na mwandishi  wetu, Baba Hamisi alisema yeye hakuwa akifahamu kama mkewe anajiuza hivyo tukio hilo lilisababisha apigwe na butwaa.

CHRISTOPHER GEORGE YOHANA NI ASKARI WA TANZANIA ALIYETEKWA NA WAASI WA M23



Waasi wa M23 wa DR Congo, wanadai kuwa wamemkamata askari wa Tanzania anayeitwa Christopher George Yohana, wakati akishirikiana na waasi wa Rwanda (FDLR) wanaodaiwa kuhusika na mauaji ya maelfu ya Watusi mwaka 1994.

Waasi hao wa M23 wameweka picha ya passport ya mateka huyo kwenye mitandao ya kijamii ya Facebook na Twitter. 



Kwa mujibu wa chimpreports.com, M23 wameripoti kumkamata askari huyo akiwa na bunduki aina ya AK47 yenye serial number 1372. Ifuatayo ni kauli ya M23 waliyoweka Facebook ikiambatana na picha hiyo:


“leo Fdlr zikiongozwa na askari toka Tanzania zilivamiya Positions zetu pale Kinyadonyi Na Nkwenda huko Rutshuru. Zilikuta Vijana wanazisubiri, walizicapa na kuzikimbiza alafu zikaaca Askari wa Tanzania Nyuma tukamunasa, ivi tuko naye tuko na mupa cayi na mukate anywe. 



Serikali ya tanzania isiwe na hofu hatutamufanya kitu, tutamucunga muzuri. sisi hatuko kama wale wa criminals wa FARDC ambao wanatukanaka hata maiti, na wenye Wanabakaka watoto wa myaka sita, sisi ni jeshi la Mungu. Kesho mutaona Video yake, Cliquer apa uone passport ya ule askari ya tanzania ambaye tulikamata”

christopher-george-yohana
Na hapa chini ndicho walichopost Twitter: m23-tanzania-twitter


BBA: MSHIRIKI WA TANZANIA ( NANDO) HUENDA AKASHITAKIWA KWA KOSA LA KUMDHALILISHA MSHIRIKI WA KIKE TOKA GHANA



Mshiriki wa pekee katika Jumba la BBA The Chase , Selly kutoka nchini Ghana, amesema ya kwamba yupo mbioni kumfungulia mashtaka mshiriki kutoka nchini Tanzania Nando kwa kitendo cha kumdhalilisha na kumsingizia amemuambukiza Ugonjwa wa Zinaa.

Baada ya kutolewa katika jumba hilo wiki iliyopita, Selly ameshauriwa na mama yake na tayari wamewasiliana na Waandaji wa Shindano hilo. " Nimepima  sijakutwa na maambukizi ya aina yoyote ya Magonjwa ya Zinaa wala sina historia hiyo" Alisema Selly.

" Mimi na Nando hatukufanya Mapenzi zaidi ya kucheza tu Kitandani, nashangaa hata kwa kiasi gani mambo yamekuwa hivi" Aliongeza Mrembo huyo.

"WANAUME WALIO MSAIDIA SAJUKI WAMENIGEUKIA NA KUNITAKA KIMAPENZI"-WASTARA JUMA



Wastara Juma amefunguka kuwa wanaume wengi waliokuwa wakimsaidia wakati mumewe Juma Kilowoko ‘Sajuki’ akiwa mgonjwa wanamgeuka na sasa wanamtaka kimapenzi. 
 
Akizungumza kupitia Kipindi cha Take-One katika Runinga ya Clouds chini ya Zamaradi Mketema, Wastara alisema baadhi ya watu ambao walikuwa karibu naye wakati Sajuki anaumwa sasa hivi wamegeuka na kumtaka kimapenzi, jambo ambalo linamuumiza na kumshangaza mno.

Bishosti huyo alisema kuwa tofauti na wanaume hao ambao walikuwa wakimpa sapoti kipindi hicho, bado wapo wengine kibao kutoka nje na ndani ya nchi ambao wanatuma maombi kwake lakini anawaona wote ni matapeli na wanamtamani tu hivyo hayupo tayari kuingia kwenye uhusiano wa aina hiyo.

“Kweli ninaumia sana kwa sababu ninakaa na kujiuliza hawa wanaume walikuwa wanasubiri mume wangu afariki dunia ndiyo wanitongoze?
 

“Kusema kweli inanishangaza, hata watu ambao sikuwadhania kabisa eti nao wananitaka, watu wajue kwa sasa sipo tayari kuwa na mwanaume.
 

“Sitaki kukurupuka kwa sababu naweza nikaingia kwenye shimo la taka kwani jamii itanikimbia kutokana na kunuka, natamani kumpata mwanaume anayefanana na mume wangu kitabia.

“Uvumilivu wangu na uzuri ulitokana na kutunzwa siyo aje mtu anayetaka nikavumilie shida, hilo sitaki litokee, namuomba Mungu sana,” alisema Wastara.

soource:mpekuzi

Picha 6! rapper Mabeste kapata Babyboy..


babyboyword1 7 6 5 4 3 2source:millardayo

Walichoandika Big Brother Africa “The Chase” kuhusu DJ PQ.


DJPQ_BB_74d1aab9-1a24-4e1d-bbad-f477f8add475_151319161547890
Dj kutoka Clouds Media Group ndiyo atakuwa Dj wa kwanza kuwarusha washiriki wa Big Brother waliochanganyika kutoka Ruby na Diamond. Mtandao official wa Big brother the Chase ambayo unaiona pekee kupitia Dstv, wameendelea kuandika kwamba Dj PQ jina lake linatokana na jina lake la kwanza Peter na Q ni quick kutokana na kasi yake anapokuwa kazini.
Usikose kuona jinsi Dj PQ anavyoingia kwenye list ya madj waliowarusha washiriki wa Big brother tangu ianze season ya mwaka huu. Dj PQ ambaye alianza kupata fans wengi mwaka 1998 baada ya kushinda Dj competition na kupewa crown ya Smart Boy Dj, leo usiku mida ya saa tano kwa saa za Tanzania atakuwa anawarusha washiriki wa Big brother.

Unaionaje hii…shindano la kupunguza uzito na mshindi kupata dhahabu yenye thamani zaidi ya millioni 8


To match feature GOLD-FIXING/
Kutokana na hali ya watu kunenepa ovyo kwasababu ya aina maisha wanayoishi hasa kwenye vyakula wanavyokula. Halmashauri ya
jiji kubwa duniani “Dubai”, limenzisha kampeni waliyoipa jina la “Your Weight in Gold”. Unaambiwa kwa kila kilo moja utakayopunguza unapata 1gm ya pure gold.
Mchakato huo unahusisha watu watakao punguza kilo zaidi ya mbili ndani ya siku 30. Lakini kwa watu watatu watakao punguza zaidi uzito wao, watapata nafasi ya kushinda kiasi cha dhahabu chenye thamani zaidi ya millioni 8 (Dh20,000). Mtu wangu wa nguvu hili shindano lingekuwa hapa Dar mambo yangekuwaje?, watu wangu wauza chips na wauzaji wengine wa vyakula soko lingepungua huku watu wakijitahidi kuzipa hizo dhahabu kwa kupunguza kura na kufanya mazoezi yakutosha.

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...