facebook likes

Wednesday, July 3, 2013

Idadi ya Mercedes benz zilizonunuliwa na viongozi Kenya ndani ya mwezi mmoja mazee

.

Mercedes Benz
Hii ni moja kati ya stori kubwa za Kenya nilizozipata hivi karibuni, japo nimechelewa kuiweka hapa kutokana na millardayo.com kuchelewa kurudi kwenye utaratibu wake wa kawaida… ni moja ya headlines kubwa nilizopenda na watu wangu wajue.
Mtandao wa Jambo umeripoti kwamba baadhi ya Makatibu wakuu wa Wizara na wajumbe wa kamati mbalimbali za katiba nchini Kenya, wamekiuka mpango wa Serikali kupunguza matumizi kwa kununua magari ya kifahari yakiwemo ya aina ya Limosine jambo ambalo limefanya Hazina kuwapa Onyo zito.
.
.
Taifa la Kenya lilipata taarifa kwamba viongozi kadhaa wa juu wamenunua magari 30 aina ya Mercedez Benz ndani ya mwezi mmoja ambapo wengine wamedaiwa kujichukulia magari ya ulinzi kinyume na taratibu.
Unaambiwa katibu mkuu wa Hazina Henry Rotich jumapili iliyopita aliliambia gazeti la The Daily Nation kwamba taifa halitavumilia matumizi ya anasa na ufisadi ambapo Wizara yake haijapitisha matumizi ya magari ya kifahari.

VITUKO ZIARA YA OBAMA : kwa mara ya kwanza ndio nimeiona hii duniani aisee

.
















Huku tunakoishi uswahilini wengi wetu huwa hata majumba ya Cinema wanakolipia elfu kumi kutazama movie huwa hatuyafahamu au hatujawahi kwenda kabisa…. hivyo kuna kautaratibu ketu ka kuchangisha hizi mia mia na mia mbili kwa ajili ya kuingia ‘vibanda umiza’ ambavyo huwa vinatutoza hizo senti kwa ajili ya kutazama movie zilizotafsiriwa pamoja na mpira…. yani kutazama hivyo vitu viwili sehemu kama hizo ni kawaida kabisa.
Sasa bwana kwenye eneo la Kisarawe ambalo liko kwenye mkoa wa Pwani, kuna mjanja mmoja alitumia akili ya ziada kujua kwamba sio kila mmoja anaweza kwenda town kusubiria kuona msafara wa Rais Obama, hivyo akaamua kuchangisha hizo mia mia kwa kila anaetaka kutazama ujio wa Rais Barack Obama Tanzania ambao ulikua unaonyeshwa moja kwa moja na vituo mbalimbali vya TV ikiwemo ya Taifa TBC1 na Clouds TV.
Uhakika wa kuzikusanya hizo mia mia ulikuwepo sana kwa sababu kwanza Kisarawe sio kila Mwananchi anamiliki TV au nyumba yake ina umeme hivyo ni lazima tu kama angekua na shilingi 100 angejikusanya kwenye kibanda umiza kucheki hilo movie la Obama kwenye ardhi ya Tanzania.
.
Hii ni ndege ya Rais Obama kwa juu wakati akiwa anatua Dar es salaam.
.
.

Umeshawahi kumsikia akiongea mtu alietajwa kufa akafufuka? #Msukule




..
Hekaheka ni kipengele ndani ya show ya Leo Tena Clouds FM ambacho huwa kinadili na mikasa ya mitaani na ya ndani kabisa… leo July 3 mtangazaji Dina Marios amefanya mahojiano mafupi na Mtanzania ambae amewahi kuchukuliwa kama msukule, ni zile imani za kishirikina ambapo mtu anatangazwa kafariki lakini sio kweli….. huyu jamaa alishawahi kutangazwa amekufa, msiba ukafanyika kabisa nyumbani.




MAMA WA MIAKA 52 AKAMATWA KWENYE CHUMBA CHA MTIHANI AKIMFANYIA MTIHANI BINTI YAKE


Mwanamke mmoja mfaransa (52) amejikuta mikononi mwa polisi wa jiji la Paris katikati ya mwezi june, baada ya kukamatwa kwenye chumba cha mtihani akimfanyia mtihani wa Kiingereza mwanae mwenye umri wa miaka 19, huku akijiweka kisichana zaidi wasimshutukie.

Ripoti kutoka nchini humo zinasema mwanamke huyo aliyejulikana kwa jina la Caroline D aliingia kwenye chumba cha mtihani akiwa amevaa skin jeans na viatu aina ya Converse ili aonekane kama mwanae.

Lakini jicho makini la msimamizi wa mtihani lilimnasa mama huyo kwa kuwa msimamizi alikua tayari alishamuona mwanae wakati anafanya mtihani wa Philosophy, kwa hiyo akamshtukia mama huyo kwa muonekano wake na sura yake ya kiutu uzima.

Msemaji wa Polisi wa Paris alisema mwanamke huyo alikiri makosa yake ya udanganyifu na kusema kuwa kiukweli yeye alikuwa anaweza zaidi Kiingereza zaidi ya mwanae.

Mwanamke huyo anakabiriwa na mashtaka ya udanganyifu na anaweza kulipa fine isiyopungua £7,000.

Lakini pia binti yake anaweza kupata msala wa kuzuiwa kufanya mtihani wowote wa kitaifa kwa muda wa miaka mitano. 

LeoT

JACOB STEVEN 'JB' AJIFUA KUMCHACHAFYA IDD AZZAN KATIKA USIKU WA MATUMAINI J'PILI HII



Jacob Steven 'JB' akijifua kwa ajili ya mpambano wake na Idd Azzan utakaofanyika katika Tamasha la Usiku wa Matumaini 2013.
Jb akipiga pushapu kadhaa wakati wa maandalizi hayo.
JB akiwa tayari kumkabili Idd Azzan.
MSANII nguli wa Filamu nchini, Jacob Steven 'JB' akifanya mazoezi ndani ya The Atriums Hotel kwa ajili ya maandalizi ya mpambano wa ndondi kati yake na Mbunge wa Kinondoni, Idd Azzan utakaofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Julai 7 mwaka huu katika Tamasha la Usiku wa Matumaini.

CPwaa signed with Universal Music





The Tanzanian International Bongoflava Artist has signed a licensing deal with one of the world biggest and top Music labels "Universal Music, South Africa". His content will be distributed through the Kleek, a mobile streaming service available on all Samsung smart phone in Ghana, Angola, Kenya, South Africa and Nigeria. CPwaa is one of the A-List Artists signed by Universal Music from East Africa for its Kleek continental platform.

On March 13, 2013 Universal Music Group, in partnership with Samsung, as well as African and international music labels and publishers, has launched a pan-African mobile music streaming service called the Kleek.  Designed and built specifically for Africa, the Kleek will bring music lovers closer to their favorite artists, while also providing artists with valuable access to a wider pan-African audience.

This new deal will make CPwaa not only to gain more revenues from his music but also a worldwide exposure and global outreach through the Kleek.

WADUNGUAJI"SNIPPER" WA OBAMA WALIVYOKUWA VIVUTIO KWENYE MAGHOROFA YA POSTA, WENGINE KIBAO WALIKUWA KIGAMBONI LAKINI WALIKUWA WANAONA KILA KINACHOENDELEA MJI MZIMA!

 
Mmoja wa Wadunguaji ambae alionekana kwenye maghorofa ya Posta juu akiimalisha usalama.
 Madunguaji ambae alionekana kwenye vichaka huko Kigamboni akiimaRisha usalama kwa kutumia viona mbali ambavyo vilimuwezesha kuona kila kitu hasa maeneo ya Ikulu.

 Hii ni silaha maalum kwa ajili ya kudungua mtu mwenye umbali mrefu kupita maelezo ambapo inadaiwa uwezo wa kumtungua adui aliyekuwa kwenye umbali kati ya Mwenge na Kariakoo.
 Kazi ilikuwa moja tu kuseti mitambo kama Magaidi wangethubutu kufanya fyoko basi shughuli wangeiona kudadeki!!


 Mdunguaji huyu ambae nae alikuwa tayari kwa lolote kama ingetokea ambushi yoyote.

Hiyo ndo darubini iliyopo kwenye bunduki ya kudungulia ambayo humsaidia mtumiani kumlenga adui na huwa haikosei ikifyatuliwa inamfikia mlengwa.

Kama hukubahatika kuona watu hawa ambao mara kadhaa tumekuwa tukiwaona kwenye sinema za waigizaji maalum wa Kimarekani kama vile Bruce Wills nk utakuwa umekosa uhondo wa aina yake kwani walikuwa vivutio vikubwa sana kwenye Jiji la Dar pamoja na viunga vyake.
blog hii ambayo ilikuwa imemwaga waanahabari wake waliobobea kufanya habari za uchunguzi walibahatika kuwanasa wadunguaji hao" Snipper" wakiwa wamejiachia kwenye majengo marefu wakiimarisha usalama.

Habari zaidi zilieleza kuwa wadunguaji hao hawakuwa Posta peke yake bali kwenye mji mzima wa Dar ambapo Maghorofa yote ya Kariakoo yalijaa wao huku Kigamboni ndo wakiwa wale wenyewe wa kivita kabisa hali ilizusha hofu na mashaka tele kwa wananchi waliwaona.
Hata hivyo kifaa  kilichofungwa kwenye bunduki hizo ambacho humuwezesha mtumiaji kumlenga vyema mlengwa wake na inasemekana vinauwezo wa kufika kilomota kumi umbali wa kutoka Mwenge na Kariakoo.
Habari zaidi zilieleza kuwa wadunguaji hao walifika kwenye sehemu hizo siku tatu kabla ukiacha wale FBI ambao inadaiwa walikuja mwezi mmoja kabla.

MACHANGUDOA WALALAMIKA UKATA MKUBWA ZIARA YA OBAMA, WASEMA MATEGEMEO YAO ILI KUWA NI KUWA MAMILIONEA.WASEMA AFADHALI UJIO WA BUSH ULIKUWA NA NEEMA NYINGI.

Rais Barack Obama wa Marekani

Polisi wa Kimarekani waliokuwa mwiba mkali kwa ulinzi wa Obama

Machangudoa wakiwinda wazungu maeneo ya Oysterbay Karibu na Ubalozi wa Marekani


Machangudoa wakiwa kazini

Katika hali ilisiyokuwa ya kawaida wakina dada maarufu wanaojihusisha na biashara ya kuuza miili yao maarufu kwa majina ya machangudoa wameulalamikia ujio wa Rais Barack Obama kwa kile kilichodaiwa haukuwa na faida yoyote kwa kukosa dili za pesa.

Wakiongea na blog hii kwenye baadhi ya sehemu wanazopatikana wakina dada hao walisema kuwa” Tumesikitishwa sana na ujio wa Obama kwani tulikuwa tumejipanga kupiga hela ndefu sana lakini patupu kwani watu wake tuliokuwa tumewategemea kuwanasa walikuwa busy na usalama pia kukaa kipindi kifupi kumechangia sisi kukosa mapato" Walisema wakina dada hao waliokutwa maeneo ya Coco Beach

Aidha machungudoa hao waliongeza kusema kuwa kipindi cha Bush ambae alikaa nchini karibu wiki moja walinufaika sana ambapo wengi wao walijenga majumba kwa pesa za ziara ya Bush kwani walifanikiwa kuwanasa watu wake na kufanya nao biashara kwa bei nzuri.

MCHUNGAJI WA KANISA LA EAGT JIJINI MBEYA AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA 30 NA VIBOKO 12 BAADA YA KUBAKA NA KUMPA MIMBA MWANAFUNZI


MCHUNGAJI wa Kanisa la Evangelical Assemblies of God of Tanzania(EAGT) la Iwambi Jijini Mbeya Daniel Mwasumbi amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela na viboko 12 baada ya kukutwa na makosa mawili ya Kubaka na kumpa mimba Mwanafunzi wa miaka 19.

Akisoma hukumu hiyo Hakimu wa mahakama ya Wilaya ya Mbeya Ndugu Gilbert Ndeuruo amesema Mahakama imemtia hatiani kutokana na ushahidi uliotolewa na Shahidi namba moja katika kesi hiyo ambaye ni mhanga wa tukio hilo Neema Beni(19).

Amesema Mtuhumiwa huyo ilidaiwa kutenda makosa hayo kati ya Mwezi Januari 2008 hadi Mwaka 2011 katika eneo la Iwambi kinyume na Sheria kifungu cha 130(2)e na 131 (1) sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002 kwa kosa la ubakaji.

Kutokana na ushahidi huo Hakimu Ndeuruo alidai kuwa Mahakama yake imemkuta Mtuhumiwa na makosa mawili ya Ubakaji na kumpa ujauzito kwa ushahidi uliotolewa na Mhanga mwenyewe pamoja na Mwalimu wa Shule aliyokuwa akisoma ambapo alidai kuwa Shitaka limedhihirishwa pasipo shaka chini ya kifungu cha 235/1985.

Kwa upande wake Mwendesha mashtaka wa Serikali Archiles Mulisa aliiomba Mahakama hiyo kutoa adhabu kali kutokana na mtuhumiwa kutenda kosa la kinyama tofauti na umri wake na wa binti ambapo Binti anaumri wa Miaka 19 ili hali Mtuihumiwa akiwa na Miaka 57.

Pia alidai kuwa Mtuhumiwa huyo alimharibia masomo na maisha yake binti huyo na vitendo hivyo alikuwa akivifanyia sehemu mbali mbali ikiwemo kanisani , hivyo aliiomba mahakama hiyo kuvitaifisha na kutoa amri ya Matunzo ya Watoto kwa kutumia amri ya kutaifisha.

Hata hivyo Hakimu alimuuliza Mtuhumiwa kuhusu kupunguziwa adhabu ambapo Mshtakiwa huyo aliomba kupunguziwa adhabu kwa madi kuwa ameachiwa watoto na ndugu zake aliozaliwa nao wakiwemo wazazi wake hivyo akifungwa hawatakuwa na msaada.

Aidha kutokana na utetezi huo Hakimu Ndeuruo alimhukumu kifungo c ha Miaka 30 na viboko 12 kutokana na kosa la kwanza ili hali katika kosa la pili amehukumiwa kifungo cha Miaka 5 na kuongeza kuwa adhabu hizo zitaenda kwa pamoja na kulipa fidia ya Shilingi Milion 20 kwa fedha za Tanzania kwa familia ya Mhanga.

Ameongeza kuwa Mtuhumiwa anahaki ya kukata rufaa katika Mahakama kuu ya Mbeya kama hatakuwa ameridhika na adhabu aliyopewa na mahakama yake.

MCHUNGAJI wa Kanisa la Evangelical Assemblies of God of Tanzania(EAGT) la Iwambi Jijini Mbeya Daniel Mwasumbi akiwa mahakamani kungojea kesi yake.
Wananchi Mbalimbali wakisubiri Kusikiliza Kesi ya MCHUNGAJI wa Kanisa la Evangelical Assemblies of God of Tanzania(EAGT) la Iwambi Jijini Mbeya Daniel Mwasumbi
   MCHUNGAJI wa Kanisa la Evangelical Assemblies of God of Tanzania(EAGT) la Iwambi Jijini Mbeya Daniel Mwasumbi aliye vaa koti Jeupe   akiwa anatolewa mahakamani Baada ya kusomewa kifungo cha Miaka 30 Jela

  Watoto wa MCHUNGAJI wa Kanisa la Evangelical Assemblies of God of Tanzania(EAGT) la Iwambi Jijini Mbeya Daniel Mwasumbi wakiwa wanatoka Mahakamani Baada ya Baba yao kusomewa kifungo
  Mtoto wa MCHUNGAJI wa Kanisa la Evangelical Assemblies of God of Tanzania(EAGT) la Iwambi Jijini Mbeya Daniel Mwasumbi akiwa anaongeaa na waandishi wa Habari baada ya kesi kumalizika
 Waumini Mbalimbali wakiwa nje Baada ya kesi kumalizika


Watoto wa MCHUNGAJI wa Kanisa la Evangelical Assemblies of God of Tanzania(EAGT) la Iwambi Jijini Mbeya Daniel Mwasumbi wakiwa nje hawaamini  baada ya kusikia Baba yao anafungwa Miaka 30

  Binti  anaye daiwa kufanyiwa kitendo hicho akilia kwa Uchungu baada ya kesi kwisha

Mbeya yetu 

FEZA KESSY AENDEKEZA TABIA YA KUPIGWA DENDA NDANI YA JUMBA LA BIG BROTHER


Mshiriki  wa  Botswana, Oneal   ameendeleea  kuyafaidi  mate  ya  dada  yetu   ambapo  wakati  huu  jamaa  huyo aliamua kupiga magoti wakati akimwaga "sera za nguvu"  kwa Feza na kumwambia kuwa maisha yake yalikuwa shagala bagala kabla hajakutana na mwakilishi huyo wa Tanzania.


Maneno hayo matamu yalimwingia vyema Feza ambaye alikuwa akitabasamu muda wote kuashiria upendo mzito kwa jamaa huyo wa Botswana ambaye anataka wawe na maisha pamoja siku za usoni.


Washiriki wengine waliamka na kuwashangalia wapenzi hao kama yalivyo maisha ya kawaida. 

Muda  mfupi  baadaye, Feza  na  Oneal  walianza  kubadilishana  mate  na  ndimi...!!!!!!!

WATUHUMIWA WA MAUAJI YA MWANGOSI WAACHIWA HURU


Na Gustav Chahe, Mufindi( Kamanda wa matukio)
MAHAKAMA ya Wilaya ya Mufindi imetupilia mbali mashtaka  yaliyokuwa yakiwakabili Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Hamad Yusuph na wenzake 42.


Kiongozi huyo pamoja na wenzake walikuwa wakikabiliwa na makosa matatu likiwemo la kufanya mkutano bila kibali pamoja na kuharibu mali ambazo ni kofia za pikipiki (helmenti) 2 za polisi katika tukio lililosababisha kuuawa aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha Channel Ten Daudi Mangosi katika kijiji cha Nyololo wailayani Mufindi.


Kutokana na tuhuma hizo Chadema iliweka pingamizi za kutaka kesi hiyo ifutwe kwa kuwa ilifunguliwa kinyume cha sheria.

Wakili wa Chadema Lugaziya akisaidiana na mwanasheria wa Chadema Luka Sinkala Mwenda waliweka pingamizi kuwa aliyetoa amri ya kusitisha mkutano na kusababisha kifo cha mwandishi wa habari huyo ni kamanda wa Polisi Michael Kamuhanda ambapo aliingilia kazi ya OCD wa Mufindi kwa kuwa hakupaswa kutoa amri hiyo, kwamba wakati amri ya kusitisha mkutano ilitolewa wakati hakukukuwa na vurugu na polisi walipiga mabomu wakati watu wanatawanyika.


Pingamizi zingine ni kwamba aliyetoa amri ya kutawanya mkutano hakuwa na cheo chochote.Wakati Chadema ikizuiliwa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika jimbo la Bububu Zanzibar walikuwa na mkutano wa kampeni za uchaguzi..

Polisi walisema wanazuia mkutano kwa kuwa sensa inaendelea wakati huo sheria ya uchaguzi haizuii shughuli zingine kufanyika na kwamba walitaka polisi waeleze sheria ya sensa inayozuia shughuli zingine kufanyika inatoka wapi...

Watuhumiwa walipoambiwa watawanyike walitawanyika bila kugoma na  mkutano uliofanyika ulikuwa wa ndani kwa kuwa ulikuwa ukifanyika ofisini baada ya mkutano wa hadhara kusitishwa na kwamba watuhumiwa waliofikishwa mahakamani walikamatwa nje ya eneo la tukio kwa kuwa walikuwa wametii amri.


Watuhumiwa hao walikamtwa maeneo ya Igawa mpakani mwa Mkoa wa Iringa na Mbeya baada ya kutoka katika eneo waliloamriwa kutawanyika.

Akitupilia Mbali kesi hiyo, Hakimu wa Wilaya ya Mufindi D. Nyakunga alisema pingamizi zilizowasilishwa na Chadema hazikujibiwa hata moja na upande wa utetezi.


"Hakuna pingamizi yoyote iliyojibiwa na upande wa utetezi. Hayo ni matumizi mabaya ya kifungu namba 91 kinataka upande wa utetezi kujibu pingamizi.

"Pia ni matumizi mabaya ya muda na fedha za serikali  na walipa kodi. Kwa sababu hizo, kesi hii inafutwa" alisema Nyakunga.

Naibu Katibu Mkuu wa wa Chadema Zanzibar Hamad Yusuph na wenzake walifunguliwa kesi hiyo baada ya kukamatwa wakati wa ufunguzi wa matawi Septemba 2, 2012 ambapo Mwangosi aliuawa na polisi kwa kupigwa bomu.

Credit: Kamanda wa Matukio

HUU NI UJUMBE WA RAY C AKIWASHUKURU MASHABIKI WAKE KWA KUMUOMBEA MPAKA AMEPATA AHUENI TENA


Mwanadada Ray C leo hii kupitia ukurasa wake wa instagram ameachia ujumbe huu kwaajili ya mashabiki zake na kuwashukuru kwa support yao.

MTOTO WA MIEZI MINNE ATUPWA AKIWA HAI MAENEO YA BAMAGA


Huyu ndiye malaika wa Mungu aliyetelekezwa maeneo ya bamaga nje ya chuo cha ustawi wa jamii karibu na TBC hapa akiwa amebebwa na mmoja wa mfanyakazi wa ITV baada ya wasamaria wema kumleta ITV...


Anayeonekana kwa nyuma ni mmoja wa vijana waliomuokota mtoto huyo

 Baadhi ya wafanyakazi wa ITV wakimshangaa mtoto aliyetupwa.
mchomeblog

YALIYOJIRI KATIKA MKUTANO WA GEORGE BUSH NA WAKE WA MARAIS



Rais Jakaya Kikwete akiwa na Mke wake Mama Salma Kikwete wakizungumza na Rais Mstaafu wa Marekani Mheshimiwa George Bush wakati wa kikao cha wake wa Marais wa Afrika kinachofanyika katika hoteli ya Serena hapa Dar es Salaam.
 Rais Jakaya Kikwete akizungumza na Rais Mstaafu wa Marekani Mheshimiwa George Bush muda mfupi kabla ya kuhudhuria ufunguzi wa mkutano wa wake wa Marais wa Afrika unaofanyika Serena hotel.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na Rais Mstaafu wa Marekani  Mheshimiwa George Bush wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wake wa Marais na wakuu wa nchi za Afrika unafanyika Dar es Salaam kwa ufadhili wa Taasisi ya George Bush.  
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Rais Mstaafu wa Marekani  Mheshimiwa George Bush na baadhi  ya wake wa marais na wakuu wa nchi za Afrika  muda mfupi kabla ya Rais Kikwete kuufungua rasmi mkutano huo kwenye hoteli ya Serena.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete (kkulia) Mke wa Rais wa Marekani, Michelle Obama (katikati) na Mke wa Rais Mstaafu wa Marekani, Mama Laura Bush, wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wake wa Marais barani Afrika unaofanyika kwenye hoteli ya Serena.

======== =========  =========

MAMA OBAMA AMPONGEZA MAMA KIKWETE KWA KAZI KUBWA ANAYOFANYA YA KUWASAIDIA WATOTO WA KIKE

Mke  wa Rais  wa Marekani  Mama  Michelle Obama amempongeza  Mke wa Rais  Mama  Salma  Kikwete  kwa kazi  kubwa anayoifanya  ya kutoa elimu bure  kwa watoto Wa kike ambao ni yatima  na wanaoishi katika mazingira hatarishi .

Mama Obama  alizitoa pongezi hizo jana  wakati wa majadiliano baina yake na Mama Laura Bush kwenye mkutano wa   wake Wa Marais Wa afrika unafanyia katika hoteli ya Serena  jijini Dar es  Salaam.

Mama Obama alisema kuwa wake Wa Marais wanakazi kubwa ya kuhakikisha kuwa wanawasaidia  wanawake na watoto hasa katika upatikanaji Wa elimu na mahitaji mengine muhimu.

"Juzi nilitembelea  makumbusho ya taifa, nilikutana na watoto  ambao  baadhi yao walikuwa ni wale wanaosomeshwa na Mama Kikwete , niliongea nao watoto hawa wanapatiwa bure elimu, chakula na maladhi hakika nampongeza sana kwa kazi nzuri anayoifanya", alisema Mama Obama.

Akiongea wakati wa ufunguzi wa mkutano huo Mama Kikwete alisema kuwa wake wa Marais waliohudhuria mkutano huo wanawawakilisha wanawake wa Afrika  ambao wanahitaji kusaidiwa katika mambo ya afya,  elimu na ujasiriamali.

Mama  Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA)  alisema kuwa katika mkutano huo washiriki watapata nafasi ya kubadilishana ujuzi wa kazi  na kutembelea hospitali ya Kansa ya Ocen Road,kituo cha Mabinti na hospitali ya CCBRT ambako watajionea jitihada kubwa zinazofanywa na watanzania za kuisaidia jamii inayowazunguka.

Alisema kuwa baada ya kumalizika kwa mkutano huo anaamini kuwa washiriki watarudi katika nchi zao na kuweza kukubaliana na Serikali zao pamoja na wadau Wa wengine kuwekeza zaidi kwa wanawake ili kuimarisha bara  la Afrika.

Mkutano huo wa siku mbili   umeandaliwa na Taasisi ya Rais mstaafu wa Marekani George Bush na kuhudhuriwa na baadhi ya wake Wa Marais wa Afrika na Mke wa Waziri mkuu mstaafu Wa Uingereza Cherie Blair.

Mada kuu ni wekeza kwa wanawake imarisha Afrika lengo l ikiwa ni kuimarisha upatikanaji wa Afya  kwa wanawake, upatikanaji Wa elimu na uchumi katika Afrika.

Credit: Michuzi.

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...