facebook likes

Wednesday, February 13, 2013

Missed the Live Kenya Presidential Debate? Watch It Here

Presidential candidates; Peter Kenneth (Eagle), Uhuru Kenyatta (Jubilee), Musalia Mudavadi (Amani), Martha Karua (Narc Kenya), Prof James ole Kiyiapi (Restore and Build Kenya - RBK), Raila Odinga (CORD), Paul Muite (Safina) and Mohammed Abduba Dida (Alliance of Real Change - ARK) on Monday night engaged in a live debate aimed at convincing the 14 million voters that they are best suited to succeed President Kibaki in the March 4 General Election.

In the first pre-election debate for all presidential candidates in Kenya, the eight contestants tackled a wide range of issues, including foreign policy, party politics, corruption and tribalism.


If you for some reason you missed it, you can watch it below and even keep a copy;

ZIJUE SABABU ZA GARI LA KANUMBA KUKABIDHIWA KWA DK CHENI


IMEBAINIKA kuwa lile gari la aliyekuwa nguli wa filamu Bongo, marehemu Steven Kanumba, aina ya Toyota Lexus limekabidhiwa kwa mwigizaji, Mahsein Awadhi ‘Dk. Cheni’.
Kwa mujibu wa chanzo makini, mama wa marehemu, Flora Mtegoa alifikia uamuzi wa kumkabidhi Dk. Cheni gari hilo baada ya kushindwa kuligharamia mafuta.
“Lilikuwa linakaa muda mrefu pale nyumbani kwao Kimara-Temboni (Dar) bila kutumika ndipo bi mkubwa akaona bora amkabidhi Dk. Cheni ili angalau aliendesheendeshe lisiharibike,” kilidai chanzo hicho kwa sharti la kutochorwa jina lake gazetini.

DK. CHENI LIVE TABATA
Wakati mapaparazi wakianza kazi ya kuchimba data zaidi juu ya gari hilo, Februari 9, walimnasa Dk. Cheni akiingia na gari hilo kwenye arobaini ya marehemu Juma Kilowoko ‘Sajuki’ iliyofanyika nyumbani kwake Tabata-Bima, jijini Dar.
LIMEPIGWA BEI?
Kwa mujibu wa Dk. Cheni kwa sasa gari hilo lipo mikononi mwake akilitumia kwa safari za hapa na pale ili kulifanya lisiharibike vifaa kwa kukaa muda mrefu bila kutumika.
“Wamenipa nilitumie kwa muda kwani lingeendelea kukaa pale basi lingeendelea kufa baadhi ya vifaa, wala halijapigwa bei,” alisema Dk. Cheni.
Katika hatua nyingine, kauli ya mama Kanumba kuhusiana na gari hilo ilitofautiana na ya mdogo wa marehemu, Seth Bosco ambapo mama huyo alisema gari hilo halijatoka nyumbani huku mdogo mtu huyo akisema limetoka.
“Mbona gari lipo hapa nyumbani halijatoka, kwanza limeisha bima na matairi hayana upepo sasa litatokaje?” alihoji mama Kanumba.
Seth alipoulizwa kuhusiana na uwepo wa gari hilo nyumbani, alitiririka:
“Gari limetoka kwa muda hata hivyo ni bovu na linahitaji marekebisho kidogo.

QUICK ROCKA KUACHIA NGOMA MPYA NA AKIWA NA NGWAIR HIVI KARIBUNI



Katika kile kinachoonekana #ChampagneBoyz wont stop at nothing this time... Quick Rocka a.k.a Kizzy one of the fastest rappers in TZ anataraji kuachia mdundo wake mwingine hivi karibuni. Track hiyo inayofahamika kama MY BABY, Quick amemshirikisha rapper mwingine, like ni mkali wa freestyle in Bongo... Based in East Zoo [Dodoma] I'be speaking about Ngwair... Now you get it on #ChampagneBoyz on this 1...
 Quick Rocka anaefanya vizuri redioni kwa sasa na ngoma yake ya KATIKA ameongea na GongaMx na kusema, zigo lipo kwenye final touches likiwa produced na Maneck kutoka AM Records na kwamba fans wakae tayari kuisikia ngoma hiyo hivi karibuni akisimama na Cowwizzy!!!
Keep speaking to Quick, aliongeza kuwa track hiyo pia ipo katika process ya matengenezo ya video ambayo pia itafuata baada ya audio. Shooting ya MY BABY itaanza hivi karibuni ikiwa chini ya Director Nick Dizzo kutoka E-Media.

Let's Go Champagne Boyz!!!

P SQUARE MAGICAL HEALING : NEW VALENTINES LOVE SONG

Peter Okoye na Paul Okoye wameshusha kitu kipya cha valentine...........
Producer wao ni VTEK na ni moja ya nyimbo zao mpya kabisa kwa mwaka 2013.
Isikilize hapa www.jovinbachwa.blogspot.com live.............

HUYU MWIGIZAJI NDIO ANATAJWA NA WENGI KWAMBA KAFANANA NA MAREHEMU KANUMBA.




Hii ni movie mpya ambayo imeingia sokoni siku mbili zilizopita, imetengenezwa na kampuni ya Marehemu Steven Kanumba, humo ndani wameigiza Seth mdogo wake Kanumba, Rose Ndauka, Muhogo Mchungu na Rammy wa kwanza kushoto ambae ndio anatajwa na wengi kwamba kafanana na marehemu Kanumba.

.

.

REKODI MPYA:BAGHDAD FT WABABA - MPAKA LINI


TANZANIA YAPETA MAAJABU SABA YA AFRIKA


TANZANIA imepata tuzo tatu za maajabu saba ya Afrika kupitia vivutio vyake bora vya utalii  vya  Mlima Kilimanjaro,Hifadhi ya Ngorongoro na Hifadhi ya Serengeti ambayo ndio iliongoza kwa kupata kura nyingi kuliko nchi nyingine yeyote.
Akitangaza matokeo hayo jana mjini hapa  rais wa taasisi iliyoandaa tuzo hiyo Dk. Phillip Imler wa nchini Marekani mbele ya waziri mkuu Mizengo Pinda alisema kutokana na Tanzania kuwa na vivutio vya kipekee ndio sababu iliyopelekea kupata ushindi huo.
Akielezea hifadhi ya taifa ya Serengeti alisema kuwa ndio hifadhi ya kipekee iliyopata kura nyingi na kutokana na tabia za misafara ya wanyama wanaohama kwa msimu.
Naye Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye alikuwa mgeni rasmi katika ghafla hiyo alisema kuwa nchi za Afrika zinavivutio vingi vya utalii na fursa kubwa ya kukuza pato kupitia utalii huo.
Alisema anaamini kutokana na sifa ambayo Tanzania imezipata kupitia vivuti vyake vitatu itaendelea kuvitunza kuhakikisha kuwa  vinavutia zaidi watalii na kuongeza pato la taifa.
“Afrika ina vivutio vingi  vyenye kuvutia hivyo kila nchi ni lazima ijivunie rasilimali hizo kwa kuvitunza na kuviendeleza,”alisema
“Alisema kwa Tanzania ni bahati ya pekee kwa kuweza kupata tuzo tatu za maajabu saba ya Afrika  ambazo ni za Mlima Kilimanjaro, Bonde la Ngorongoro pamoja na hifadhi ya Taifa ya Serengeti hivyo ni wajibu wa kuvitunza na kuviendeleza,”alisema Pinda.
Alisema kuwa iwapo watanzania wataendeleza tabia ya utunzaji wa vivutio vilivyopo nchini, nchi itaendelea kupata sifa duniani kote.
Naye Mkurugenzi wa Hifadhi za Taifa,(TANAPA),Dk, Alan Kijazi alisema mlima Kilimanjaro ni mlima mrefu barani Afrika na hivyo una kila sababu ya kushinda na watanzania waendelee kuutunza.
Akizungumzia kuhusiana alisema kuwa hifadhi hiyo imeshinda kwa kuwa kuwa na wanyama wa kila aina kama Big Seven, Simba, tembo, Viboko, Nyati, Vifaru, Sokwe na Mamba.
Mbali na Tanzania Dk.Imler alivitaja vivutio vingine vilivyoshinda kuwa ni Red sea Reefs, Okavango Inland  delta iliyopo nchini Botwasana, Sahara Desert na River Nile.
Aidha Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki ushindi huo ni historia kubwa duniani na kwamba ni jambo la watanzania wote kujivunia.
Pia aliwashukuru wananchi walioshiriki katika mchakato mzima wa kupiga kura na kuviwezesha kuingia katika ushindi kwa mara tatu

MAOMBOLEZO YAFANYWA KUFUATIA KIFO CHA MAMBA MKUBWA ZAIDI DUNIANI

Wananchi wakipiga picha mbele ya mwili wa mamba mkubwa zaidi duniani.



Mji mzima ulikuwa katika maombolezo jana baada ya Lolong, mamba mkubwa kabisa duniani kufa katika Ziwa lake la kujengwa kutokana na kuumwa ghafla.

Mamba huyo majichumvi mwenye urefu wa futi 21 na uzito wa tani moja, ambaye alikamatwa miezi chini ya 18 iliyopita na timu ya wanaume majasiri kusini mwa Philippines, alikutwa akiwa amelala chali katika eneo lake kwenye hifadhi ya biashara ya utalii.

Lolong, anaaminika kuwa na zaidi ya miaka 50, aliana kuumwa baada ya kumeza mfuko wa plastiki takribani wiki tatu zilizopita. Baada ya hapo akabaki akiharisha mfululizo, limeripoti gazeti la The Philippine Star.

Lolong, amepewa jina hilo na mwindaji maarufu wa Philippines, amekuwa akilaumiwa kwa vifo vya vya wavuvi kadhaa kabla ya kukamatwa kiaina kwenye ziwa lenye matope karibu na mji wa Bunawan (wenye wakazi 35,000), maili 515 kusini mashariki mwa Manila.

Wanaume 30 walitumia wiki tatu kujaribu kumkamata mnyama huyo mkubwa kabla mwishowe kufanikiwa Septemba 2011 kwa kutumia mzoga wa nguruwe kama chambo na kutupa nyaya juu kuzunguka mwili wake.

Ilibidi litumike trekta kumvuta hadi kwenye trela - lakini hapo kabla umati mkubwa wa watu ulimzingira kwa ajili ya kupiga picha na mamba huyo aliyevunja rekodi.

Tangu hapo, Lolong amekuwa kivutio nyota kwenye hifanyi ya kitalii na madiwani wa mji wametangaza kwamba mji wao mdogo hatimaye umepata nafasi kwenye ramani ya dunia.

Lakini jana, wengi wa wakazi wa mji huo walikuwa wakilia baada ya kugundua kwamba Lolong amekufa ndani ya mwaka na nusu tangu kuhamishiwa kwenye makazi yake mapya.

"Hatufahamu kilichomtokea," alisema Meya Edwin Elorde aliyeshitushwa mno na kifo hicho, ambaye aliripotiwa kumshika mnyama huyo kabla hajafa.
"Nimetokea kumpenda mamba yule. Ameleta umaarufu na hazina kwenye mji wetu na, katika njia ndogo, kuelekea Philippines."

Elorde alisema kwamba baada ya kukamatwa kwa mamba huyo - ambaye alitawala vichwa vha habari kwenye vyombo mbalimbali vya habari duniani - hifadhi maalumu ya utalii wa kibiashara ilitengenezwa kumhifadhi.

Wakazi wa nchi hiyo na watalii wa nje wamefanya safari maalumu kwenye jamii hiyo inayofikika kwa shida kushuhudia kiumbe huyo wa ajabu.

"Tulikuwa tumepanga kujenga barabara maalumu kuelekea kwenye hifadhi hiyo sababu tumekuwa tukipata watalii wengi, lakini sasa sina hakika kama tutaendelea na mipango hiyo," alisema Meya huyo.

"Pengine  mipango itaendelea kama tutaweza kukamata mammba zaidi - kuna wengine wengi kuzunguka eneo hilo - lakini siwezi kusema kama wanaweza kufikia ukubwa kama wa Lolong.

Uchunguzi ulitarajiwa kufanyika jana kujua sababu za kifo chake.

VIDEO:ASKARI POLISI AUWAWA NA MAJAMBAZI KWA KUPIGWA RISASI TAZARA DSM

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...