facebook likes

Thursday, August 8, 2013

NIANG AICHOMOLEA SENEGAL.


MSHABULIAJI nyota wa kimataifa wa Senegal na klabu ya AC Milan, Mbaye Niang amekataa mwito wa majukumu katika timu yake ya taifa ambayo inakabiliwa na mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi Zambia Agosti 14 mwaka huu.
....SOMA ZAIDI.....
 Niang ambaye alizaliwa nchini Ufaransa, amekuwa akitakiwa na nchi zote mbili Ufaransa na Senegal lakini kufuatia kufungiwa kwa mwaka mmoja Novemba mwaka jana kucheza katika timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 21, kocha Teranga Lions aliamua kumjumuisha katika kikosi chake. Mechi hiyo kati ya Senegal na Zambia inatarajiw akuchezwa huko Saint-Leu karibu na jiji la Paris ambapo Senegal watawakosa pia nyota wake wengine ambao ni Demba Ban a Papiss Cisse. Pamoja na kuwakosa nyota hao, wachezaji wengine wanne wapya wameitwa kuongeza nguvu katika kikosi hicho ambao ni Issa Cissokho na Pape Djilobodji wanaocheza klabu ya FC Nantes, Alfred Ndiaye anayecheza Sunderland na Henry Saivet wa Bordeaux. Senegal wanaongoza kundi J la kutafuta tiketi ya kushiriki michuano ya Kombe la Dunia 2014 wakiwa na alama tisa wakati Zambia wao wanashika nafasi ya pili katika kundi D wakitofautiana alama moja na na vinara wa kundi hilo Ghana.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...