facebook likes

Thursday, August 8, 2013

PFA KUWAPA SEMINA WACHEZAJI KUKABILIANA NA LUGHA ZA KIBAGUZI.


WACHEZAJI wa Ligi Kuu na ligi zote nchini Uingereza wanatarajiwa kupewa semina kutoka Chama cha Wachezaji wa Kulipwa-PFA kuhusu mbinu za kupambana na kauli za kibaguzi. 
...SOMA ZAIDI....

 Semina hiyo ya PFA italenga haswa kuangalia njia sahihi kwa mchezaji anazopaswa kuchukua pindi atakapokutana na tukio kama hilo. Mameneja wa vilabu 92 vinavyoshiriki ligi mbalimbali nchini Uingereza tayari wameshapewa taarifa na PFA kuhakikisha wachezaji wao wanahudhuria semina hiyo. Katika misimu miwili iliyopita kumekuwa na matukio ya kibaguzi ambapo beki wa Chelsea John Terry na mshambuliaji wa Liverpool Luis Suarez wote walipokea kibano cha kufungiwa baada ya kukutwa na hatia ya kutoa lugha za kibaguzi.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...