facebook likes

Thursday, August 1, 2013

NEW MUSIC : OMMY DIMPOZ FT. J MARTINS - TUPOGO


KAMA UJAWAHI KUONA GARI DOGO LENYE JIKO NA KITANDA BASI TIZAMA HAPA PICHA NA VIDEO YAKE

Gari likiwa limefunguliwa na kuonesha maeneo yote
Hili ndilo jiko ambalo unaweza kupika ukiwa sehemu yoyotebila shida
Huu ndio mwonekano mzima wa jiko hilo

Baada ya kupika jiko hilo ubadilika na kuwa dining table 
Huu ndio mwonekano mzima wa Dining table
Hii ni sehemu ya  kunawia mikono kama unataka kula au kama unataka kuosha vyombo na pia unaweza kutumia maji haya kwa kupikia 
Hiki ni kitanda baada ya kuifadhiwa kwa chini na kitanda kuja juu

TIZAMA VIDEO YA HAYA YOTE HAPA CHINI

MASIKINI MLIMA WETU KILIMANJARO,BARAFU YOTE YAYEYUKA...!


 Taswira ya Mlima Kilimanjaro inavyoonekana kwa sasa baada ya kuyeyuka Barafu yote, ikiwa imebakia sehemu kidogo tu juu ya Kilele cha Mlima huo, ni kutokana na Mabadiliko ya Tabianchi na uhalibifu wa Mazingira uliokithiri. Picha na www.sufianimafoto.com
 Taswira ya mlima huo na Kilele cha Mlima Kibo. Picha na www.sufianimafoto.com
Mlima Kilimanjaro Kushney, kama unavyoonekana ukiwa hauna Barafu huku iliyobaki ikielekea kumalizika kwa kuyeyuka. Picha na www.sufianimafoto.com

Video za interview yote ya Nando kuhusu ugomvi BBA, msichana aliempenda, washiriki wanaoweza kushinda na mengine


7
Ni interview ya Mtanzania Nando alieshiriki kwenye shindano la Big Brother 2013 ambapo ametolewa siku kadhaa zilizopita baada ya kuvunja moja ya sheria za shindano hilo, yani chanzo ni ugomvi wake na Mghana Elikem.
Kwenye hii interview ya kwanza ya Nando toka ametoka ambayo pia afisa uhusiano wa Multichoice Tanzania Barbara Kambogi  amezungumza, Nando anakwambia kosa alilofanya lilikua ni kumwambia Elikem ukweli, haiwezekani mtu mzima na akili zake arushe barafu kwenye dancing floor.
Sasa nakualika kutazama hizi video za interview yote ya Nando.

source:millardayo




“Girl You Know Me, I’m the Best Thing” | Listen to Iyanya – Head Swell


Iyanya Manchester - June 2013 - BellaNaija (28)
‘Make my head swell oh, so I fit knack you well…’
What?! Did Iyanya just say that? Either way, he gives a very commendable effort on this raunchy new dancehall-inspired joint “Head Swell”. And, although this isn’t an official version, as it got leaked online yesterday, it’s still a worthy listen.

Produced by 2Kriss.

Check on it!

BBA UPDATES: Diary: ‘I Miss Being Kissed’ – Dillish


P_Aug01_135804 
 “I miss being with children. I miss my boyfriend. I miss being kissed,” Dillish shared with Big Brother during her Diary Session in the afternoon.
Having stayed on the Chase for 10 weeks and still counting, it’s clear that nature has started calling for the Namibian beauty. Dillish who has of late become close to Melvin seems to have formed a bond with the Nigerian and just yesterday, she played a little kiss game with him. She surely can’t wait to link up with her boyfriend after the show.
There are lots of hunky gents in the Big Brother house who would be willing to help out Dillish with what she’s currently missing but being the strong and faithful girlfriend that she’s, she’s keeping her word and not ready to cheat on him.

Hang in their Dillish-ious, it’s only a few weeks to go!

Madrid na Tottenham zakubaliana bei ya Bale.

Kichwa cha habari kwenye 'front page' ya gazeti la AS.
Kichwa cha habari kwenye ‘front page’ ya gazeti la AS.
Gazeti la kila siku la michezo nchini Hispania la AS limeripoti kuwa Tottenham Hotspurs na Real Madrid zimefikia makubaliano juu ya bei ya usajili wa Gareth Bale.
Madrid italipa paundi milioni 104 kwa mujibu wa taarifa hiyo na hivyo kumnasa mchezaji huyu ambaye amekuwa akisakwa na mabingwa hao wa zamani wa Spain kwa muda mrefu .
Makubaliano hayo hata hivyo ni ya msingi baina ya klabu hizo na hakuna kitu chochote ambacho kimewekwa rasmi .
Bado klabu hizo mbili hazijakubaliana mfumo wa malipo ya dili hilo na inatarajiwa kuwa Real Madrid itatoa kiasi fulani cha fedha kwa mikupuo kadhaa huku fedha hizo zikiambatana na wachezaji wawili ambao ni Angel Di Maria na Fabio Contreao au mmoja kati ya wachezaji hao . Andre Villas Boas ametajwa kuvutiwa na beki uwezo wa kucheza nafasi zaidi ya moja  uwanjani Fabio Contreao ambaye anamfahamu tangu nchini Ureno .
Roberto Soldado ambaye Spurs imemsajili hii leo.
Roberto Soldado ambaye Spurs imemsajili hii leo.
Wakati hayo yakiendelea Spurs wamekamilisha usajili wa mshambuliaji Roberto Soldado toka klabu ya Valencia.
Soldado amesajiliwa kwa paundi milioni 26 na taratibu za usajili wake zitakamilika baada ya mchezaji huyo kufanyiwa vipimo vya afya .

NEW SONG: PETER MSECHU FT. ALLY NIPISHE- KIBUDU


LISTEN AND DOWNLOAD HERE:

Jay Z Blasts Rihanna for Crazy Behaviour

Jay Z Blasts Rihanna for Crazy Behaviour 

Rihanna is currently more discussed for her antics than her music. She seems to be coming apart at the seams and is becoming a major source of worry for her friends. Jay Z, apparently, is among them.
Reliable sources have claimed that businessman and rapper, Jay Z, has grown increasingly annoyed with Rihanna’s uncontrolled and, partially, wild behavior.
The singer, who constantly arrives several hours late for her concerts and studio sessions is now on Jay Z’s nerves.
Jay Z has reached out to Riri a few times get her act together but she wild singer has changed her attitude and it seems to get from bad to worse.
Reports say Jay Z has since sent her an official warning letter to pull herself together or………..

Things Your Job Interviewer Will Hate You For!


photo
You probably know most of the interviewing tips that can help you forge a connection with a potential employer. Now it’s time to learn some of the things you must avoid in an interview to ensure the interviewer doesn’t end up hating you by the end of it.

These things really do happen. Just make sure they don’t happen to you.

1. Jump at the chance to trash your former boss.

“An interviewer will dislike you if you respond to the question, ‘What advice would you give your former boss, if asked?’” says Lee Evans, CEO and career coach at Free-Job-Search-Websites.com, adding that this is a trick question. “The interviewer will interpret your negative response as the answer you might give when asked about a manager at the interviewing company. It's also a test of your ability to respond appropriately to sticky questions. Your interviewer and prospective employer will side with your former manager, and view you as difficult to deal with.”


2. Comment on your interviewer’s appearance.

Whether you like the way your interviewer looks or not, keep it to yourself. Even “well, you look nice today” is inappropriate, according to Evans. Commenting on how people look when you’ve just met them can be a signal that you aren’t concerned with social boundaries or are rude. Comments about appearance are on the “interviewer’s red flag list,” Evans says.


3. Show up late.

It’s a killer, no matter why it happens. Showing up 10 minutes early is a common interview tip, but its importance cannot be overstated. “Tardiness shows one of two things: disrespect or poor planning, both of which are nonstarters for most hiring managers,” says Michael “Dr. Woody” Woodward, an organizational psychologist and author of “The YOU Plan.” Showing up late sets the tone for the rest of the interview, and you’ll have to be at the top of your game to come back from such a setback.

WAKATI SHEIKH PONDA AKITANGAZA KUGOMBEA URAIS, POLISI YATANGAZA KUMKAMATA KWA KUFANYA MIHADAHARA YA UCHOCHEZI



CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) visiwani Zanzibar kimemtuhumu Mwenyekiti wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu, Sheikh Ponda Issa Ponda, kuwa anaendesha kampeni za uchochezi wa kidini.

Uchochezi huo umedaiwa kuhatarisha amani ya nchi, hivyo kuvitaka vyombo vya ulinzi na usalama kumchukulia hatua za kisheria.

Katibu wa Kamati Maalumu ya Halmashauri Kuu (NEC) Zanzibar, Itikadi na Uenezi, Waride Bakari Jabu, alisema jana kuwa ni wiki moja sasa tangu Ponda afanye mihadhara kwenye misikiti ya Mbuyuni, Kwarara na Nungwi kisiwani Unguja.

Waride alisema kuwa hotuba za Sheikh Ponda alizozitoa kwa nyakati tofauti kwenye misikiti hiyo zinapandikiza mbegu ya chuki, kuondosha upendo na kuhatarisha amani.

Alisema matamshi yake ni hatarishi kwa amani na utulivu uliopo, kwani anawataka Waislamu kupigana vita ya dini (Jihad) na kushiriki harakati za kuikomboa Zanzibar, kwa madai kuwa serikali iliyoko madarakani inawakandamiza na kuwanyanyasa wananchi.

“Sheikh Ponda ni hatari,  anapanda shari na chuki miongoni mwa wananchi, anahamasisha  wananchi  wafanye uasi, kulipiza visiasi na kutaka waingie barabarani kwa maanadano ya kutetea haki kama inavyotokea Misri,” alisema.

Aidha, alisema CCM imeshangazwa na ukimya wa vyombo vya ulinzi na usalama wa raia kumtazama kiongozi huyo bila ya kumchukulia hatua za kisheria wakati akiwatukana matusi ya nguoni viongozi wa serikali na chama tawala.

Aliongeza kuwa Sheikh Ponda huenda anatumiwa na mtandao wa vurugu ili kuharibu na kuvuruga amani ambapo hamu yake ni kuona damu ya wananchi ikimwagika na nchi ikiingia kwenye machafuko.

Kwa mujibu wa Waride, kitendo cha Ponda kulitumia jukwaa la dini na kufanya siasa misikitini hakikubaliki na kwamba kikiachiwa kiendelee kinaweza kuleta madhara na mgawanyiko.

Kamishna wa Polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa, alisema jeshi hilo limeanza kumtafuta Sheikh Ponda tangu walipopokea taarifa za kuendesha mihadhara ya uchochezi katika baadhi ya misikiti, ikiwa na lengo la kuibua chuki.

Mussa alisema kitendo anachokifanya kinakwenda kinyume cha sheria, hivyo kumtaka popote alipo ajisalimishe kwa hiari yake.

Tangu kuingia visiwani Zanzibar, Sheikh Ponda amekuwa akifungamana na viongozi wa Jumuiya ya Uamsho wakipinga kitendo cha viongozi wa jumuiya hiyo kuendelea kubakia mahabusu baada ya kukamatwa na kufunguliwa mashtaka ya uharibifu wa mali na kuhatarisha usalama wa taifa.

Viongozi hao wa Uamsho wako mahabusu baada ya Mkurugenzi wa Mashitaka Zanzibar, Ibrahim Mzee Ibrahim, kuwasilisha ombi la kufunga dhamana yao kwa kutumia sheria ya Usalama wa Taifa na marekebisho yake ya mwaka 2002

chanzo:Tanzania daima

HUYU NDO MCHORA KATUNI MWENYE UBUNIFU WA HALI YA JUU..Angalia BAADHI KATUNI ZAKE HAPA




MSANII WA BONGO FLAVA "DAYNA" ATEMBELEA NA KUWEKA MISHUMAA KWENYE KABULI LA MANGWEA


Dayna akiweka Mshumaa juu ya Kabuli 
 
Mwimbaji wa nyimbo za mafungu ya nyanya, Fimbo ya mapenzi, Nivute kwako na ule unaotamba sasa wa Leo, Dayna Nyange mkali wao, ndani ya mwezi mtukufu, amefanya ziara ya kumkumbumbuka na kutembelea kaburi alilozikwa mwanamuziki mwenzie toka Morogoro, Albert Mangwea
Dayna ameonekana katika kabuli la Mangwea, mwanzoni mwa mwezi huu mtukufu wa Ramadhani. Akizungumza na mwandishi wa Habari hii mara baada ya tukio, Dayna amesema Albert Mangwea ni mmoja ya wasanii aliokuwa nao karibu sana na alikuwa akimsaidia kwa mambo mengi sna katika mziki

"Unajua Albert Mangwea ni zaidi ya msanii mwenzangu, alikuwa kama ndugu kwangu. Albart alikuwa akinishauli mambo mengi sana juu ya mzikim na hata maisha pia. Hivyo ni wajibu kwangu kumkumbuka mara kwa mara. Pia kitu ambacho hukijui, Ngwea ni mmoja ya wasanii walionisaidia sana hasa kusambaza wimbo wangu huu wa sasa nilioimba na Mr: Blue - Leo. sitamsahau my Brother Ngwea na ndiyo maana ndani ya mwezi mtukufu nimetenga siku ya leo kuja kumtembelea. Pumzika kwa amani japo pengo lako bado lipo'' Amemaliza huku akibubujikwa na machozi.
Dayna akipiga saluti ishara ya kumkubali Marehemu Albert Mangwea
Pumzika kwa amani Ngwea.

IRENE UWOYA KUJA NA SHOW YAKE YA KUTENGENEZA NA KUKARABATI NYUMBA ITAKAYO RUSHWA CLOUDS TV


Irene Uwoya anakuja na kipindi chake kipya cha Tv kwa ajili ya kutengeneza na kukarabati nyumba mbalimbali za watu atakazotembelea. Kipindi hicho kitarushwa kupitia Clouds Tv na tayari actress huyo ameanza kushoot kipindi hicho kama anavyoonekana pichani hapo juu. Irene Uwoya ni muigizaji mwingine aliyeamua kugeukia vipindi vya Tv pia ukiachilia mbali kuigiza filamu wengine ni Rose Ndauka na Wema Sepetu ambaye show yake kuhusu maisha yake halisi pia kitarushwa Clouds Tv kuanzia mwishoni mwa mwezi wa nane mwaka huu.

HIVI NDIVYO MBUNGE HALIMA JAMES MDEE ALIVYOFUNGUKA KUHUSU ISHU YA MADAWA YA KULEVYA. HUYU HAPA


Mbunge wa Kawe kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ameonekana kuzidi kufedheheshwa na uingizwaji wa madawa ya kulevya na biashara hiyo kuzidi kushamili nchini kwa kasi sana....

Aidha hivi karibuni binafsi wenyewe tumeweza kusikia na kushuudia watanzania wakikamatwa ughaibuni na hata wengine kufa kutokana na kumeza kete hizo na wengine kufungwa....

Hali hii naona ndio inayomchosha na kumuumiza Mbunge Halima Mdee na hizi ndizo

Tweets zake kupitia mtandao wake wa Tweeter alizotupia kufunguka Live kuhusiana na Madawa hayo na kukemea vikali...

HIKI NDICHO KILICHOMKUTA MADEE ALIPOWASILI NCHINI SOUTH AFRICA


Kwa takribani yapata wikii mbili sasa tokea tuhuma za
madawa ya kulevya kushamili
nchini hususani watanzania wanojishugulisha na maswala hayo....
Karibuni kulizuka tuhuma ambazo za kweli kwa watanzania
kukamatwa na madawa
ya kulevya nchini Afrika ya kusini na hii inaleta mtafaruku ya
ushirikiano wa baina ya
nchi na nchi...
Msanii Madee kutoka Tip Top cinnection jana aliwasili
nchi Afrika ya kusini
na alivyowasili anasema alivyojulikana anatoka Tanzania
aliwekwa pembeni kwa
takribani zaidi ya saa 1 na kusachiwa kuojiwa sana baada ya hapo
kuruhusiwa kuondoka
uwanjani hapo...
Anasema baaada ya kutaja anatokea Tanzania walikuwepo
askari waliovalia sare
walimuamuru kuvua tshirt na kubakia na nguo nyepesi ya
ndani hadi kumkagua
mabegi yake huku abiria aliokuwa amesafiri nao ndege
moja walipita
bila matatizo yoyote...
Sehemu yenyewe ambayo alivuliwa nguo sio kwenye
chumba maalumu
ilikuwa pale pale kwenye mstari,lakini baada ya ukaguzi
walimomba msamaha
na kumruhusu kuendelea na safari yake....!!

MAKAMU WA RAIS AIWAKILISHA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA VIONGOZI WAKUU WA NCHI ZA MAZIWA MAKUU JIJINI NAIROBI


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (katikati) akiwa na baadhi ya Viongozi wenzake kutoka nchi za Maziwa Makuu, wakati walipokuwa katika Mkutano wa Viongozi wa Nchi za Maziwa Makuu, alipoiwakilisha Tanzania katika majadiliano ya mkutano huo uliofanyika Jijini Nairobi, nchini Kenya jana Julai 31, 2013. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na mkewe Mama Asha Bilal, (wa pili kulia) Balozi wa Tanzania Nchini Kenya, Dk. Batrida Burian, na viongozi wengine wakati alipowasili Jijini Nairobi juzi Julai 30, 2013 kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Maziwa Makuu, uliofanyika Jiji humo jana Julai, 31, 2013. Makamu anaondoka leo Jijini Nairobi kurejea nchini baada ya kumalizika kwa majadiliano hayo. Picha na OMR  

===========   ========  =========
MAKAMU WA RAIS AIWAKILISHA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA VIONGOZI WAKUU WA NCHI ZA MAZIWA MAKUU JIJINI NAIROBI.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal ameiwakilisha Tanzania katika mkutano wa Wakuu wa nchi za Maziwa Makuu uliofanyika jijini Nairobi Kenya, jana Jumatano ya tarehe 31, 2013. Mkutano huu ulihudhuriwa na Mwenyeji wa Mkutano huo, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya, Mwenyekiti wa nchi za Maziwa Makuu na Rais wa Uganda, Yoweri Kaguta Museveni, Katibu Mtendaji wa Kamisheni yas Nchi za Maziwa Makuu Prof.Ntumba Luaba, Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Kamisheni ya Afrika, wawakilishi wan chi za DRC, Zambia, Afrika Kusini, Rwanda na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa.

Mkutano huo umepokea taarifa kutoka kwa Mawaziri wa Ulinzi kutoka katika nchi za Maziwa Makuu ambayo imepokelewa na kisha kujadiliwa. Pia ripoti kutoka kwa Kamati ya Kimataifa inayoshughulikia suala la Mazungumzo kati ya Serikali ya Kongo (DRC) na wapiganaji wa kikundi cha M23 kinachojihusisha na upingaji wa serikali ya DRC kikifanya machafuko katika Mashariki mwa Kongo (DRC) imepokelewa kujadiliwa na kisha kupitishwa mapendekezo ambayo nchi washiriki zimeyasaini.
Wakati wa uzinduzi wa mkutano huo, nchi washirika walisisitiza kutaka kuona amani inapatikana katika nchi za Maziwa Makuu na hasa DRC, Afrika ya Kati na Sudan. Wawakilishi hao walielezea kusikitika kwao kutokana na machafuko ya amani katika nchi hizo na wakawataka viongozi mbalimbali wanaotajwa kuhusika na machafuko haya kutambua kuwa athari inayotokana na machafuko haya ni kubwa na inaathiri wananchi wengi.
Viongozi hao walisema, nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu zinahitaji utulivu na kwamba mgogoro wa uvunjaji amani katika Kongo DRC unaotokana na kuwepo kwa kikundi cha M23, lazima upewe tiba ya kudumu ili eneo hilo libakie tulivu na watu wake waweze kupata fursa ya utulivu utakjaowasaidia kushiriki katika kazi zao za kila siku.

Akifunga mkutano huo kwa niaba ya Mwenyekiti Yoweri Museveni, Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta alisema ni wakati sasa nchi za Maziwa Makuu kutambua na kuazimia kwa kauli moja kuwa amani inahitajika katika nchi zote za ukanda huu. Akifafanua zaidi Mheshimiwa Rais Kenyatta alisema wananchi wa ukanda huu wanataka ajira na sio mapigano.

“Hata vijana wanaotumika katika mapigano, tukumbuke kuwa baada ya mapigano watakachohitaji ni ajira. Akina mama na watoto wanataka kuona maisha yao yanaboreshwa na sio vionginevyo. Kwa namna nilivyoona tukishiriki katika mkutano huu ni dhaihiri tumeonesha nia ya dhati ya kuhakikisha maeneo yetu yanakuwa na amani. Tudumishe nia hii nzuri,” alisema Rais Kenyatta.
Makamu wa Rais na msafara wake wanarejea nyumbani leo Alhamisi Agosti Mosi, 2013 tayari kuendelea na majukumu mengine ya kitaifa.
Imetolewa na: Ofisi ya Makamu wa Rais
Nairobi, Kenya

YANGA SASA YAMKAMATA OLOYA WA SIMBA, YADAIWA MANJI AMETOA FUNGU LA MAANA

WAKATI Simba SC imekwishatamtengea nafasi katika usajili mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda, Moses Oloya wapinzani wao wa jadi, Yanga SC wamepiga hatua na kuanza kumshawIshi aachane na Wekundu hao wa Msimbazi na atue Jangwani.
Vyanzo vinasema Mwenyekiti wa Yanga SC, Alhaj Yussuf Mehboob Manji ameipa Kamati ya Mashindano ya klabu, inayohusika na masuala ya usajili pia, chini ya Mwenyekiti wake, Abdallah Ahmed Bin Kleb fungu la kutosha ambalo ‘piga ua’ litatosha kumlainisha Oloya abadilie uamuzi wake.
Anagombewa; Moses Oloya anagombewa na Simba na Yanga

Aidha, inadaiwa tayari mazungumzo kati ya Yanga na Oloya yanaendelea na kuna makubaliano- kana kwamba mchezaji huyo mwenye kasi, nguvu na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira amekubali kuwapuuza Simba SC.   Simba SC imetenga nafasi katika usajili wake wa wachezaji wa kigeni na ipo tayari kumsubiri Oloya hata hadi Januari baada ya makubaliano ya kimsingi. Kiungo huyo mshambuliaji wa The Cranes, yaani ndege aina ya Korongo aliyezaliwa miaka 20 iliyopita anamaliza mkataba wake na Saigon Xuan Thanh ya Vietnam mwezi huu, Agosti na kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Kapteni wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Zacharia Hans Poppe aliwaahidi atakuja Septemba. Kwa sababu hiyo, Simba imepanga kusajili wachezaji wanne wa kigeni ambao ni Waganda, kipa Abbel Dhaira, beki Joseph Owino na Warundi wawili, mmoja beki na mwingine mshambuliaji, Amisi Tambwe.    
Mwenye kisu kikali nani? Bin Kleb kulia na Hans Poppe kushoto, nani atampata Oloya? 
Sasa ni wakati wa mpambano wa watani, kuwania saini ya mchezaji huyo aliyekwenda Vietnam akitokea KCC ya kwao, aliyoichezea tangu 2009 hadi 2010. Katika usajili wake, Yanga ina nafasi mbili za wachezaji wa kigeni, sasa ikiwa na watatu ambao ni beki Mbuyu Twite, kiungo Haruna Niyonzima na mshambuliaji Didier Kavumbangu- wakati bado ipo kwenye mazungumzo na Mganda, Hamisi Kiiza aongeze Mkataba.
Ametoa fungu; Yussuf Manji kulia anadaiwa kutoa fungu zito la usajili wa Oloya Yanga. Kushoto ni Waziri, Kapteni George Huruma Mkuchika
Wakati huo huo, habari zinasema, Yanga SC wana mpango wa kuleta kiungo mshambuliaji hodari kutoka Brazil.  Kwa sasa Hans Poppe amekwenda Ureno kushughulikia mpango mmoja mzuri kwa mustakabali wa klabu hiyo ya Mtaa wa Msimbazi, ambao amekuwa akiupigania kwa muda sasa na maendeleo yake ni mazuri.
 
source:binzubeiry

Mtu mmoja akutwa amekufa msitu wa kibamba.!

(apologies for this pic/samahani kwa picha hii)
Pichani ni Mwili wa Mtu aliyekutwa katupwa katika Msitu wa Kibamba Hospitali na Makondeko Luguruni, ukiwa katika hali mbaya kutokana na kudhaniwa kuwepo kwa takribani siku 4 na zaidi, mpaka sasa hajatambulika kwa jina, kutokana na kuharibika. Kikosi cha Askari kwa kushirikiana na Mjumbe wa Nyumba kumi kumi, Serikali ya Mitaa, kwa pamoja wamekubaliana kuuzika Mwili huo Pale alipokutwa katelekezwa. Halii hiyo imesababisha hofu kwa wakazi wa Maeneo ya Kibamba, Mbezi na Vitogoji vya Jirani. hivyo wameitaka serikali kuongeza jitihada za Ulinzi ususani wakati wa Usiku katika Bonde la Makondeko kuelekea Kibamba Hospitali.
 Baadhi ya wakazi wa Maeneo ya Kibamba na Makondeko, wakijaribu kutambua  Mwili huo ambao umekutwa Eneo alikokutwa katelekezwa, Bondeni kutoka katika Daraja la Kibamba Hospitali na Makondeko.
 Baadhi ya Askari wakiwa eneo la Tukio kwa Maziko na Uchunguzi.
Baadhi ya wakazi wa Maeneo ya Kibamba na Makondeko, wakijaribu kutambua  Mwili huo ambao umekutwa Eneo alikokutwa katelekezwa, Bondeni kutoka katika Daraja la Kibamba Hospitali na Makondeko

Read more: http://audifacejackson.blogspot.com/2013/08/mtu-mmoja-akutwa-amekufa-msitu-wa.html#ixzz2ahyJRfZw

MWANAJESHI AMGONGA RAIA BAADA YA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI KATIKA MATAA YA KUONGOZEA MAGARI ENEO LA TAZARA DAR ES SALAAM


Gari lililomgonga raia likipita katika upande wa kulia zinakotokea gari za Buguruni,Ubungo,baada ya dereva kukiuka sheria za usalama barabarani.
 Raia aliyegongwa akiwa hoi baada ya kugongwa na dereva wa gari la Jeshi akipepewa na askari Jeshi.
 Askari Polisi wa Usalama barabarani wakimshuhudia raia aliyegongwa eneo la TAZARA pamoja na dereva aliyemgonga akiangalia nyuma nje ya gari huku trafiki akiwa ndani ya basi hilo.
 Baadhi ya wananchi wakiangalia tukio.
 Raia wakiangalia na waliokuwa ndani ya gari wakimuangalia aliyegongwa.
 Askari akimsaidia aliyegongwa kumpeleka kwenye bajaj ili ampeleke hospital.
 Raia aliyegongwa ameumia sehemu za shingo,usoni,machoni,mkononi na miguuni akiwa amevuja damu nyingi.

 Raia akiwa hoi akipewa msaada wa kupakiwa ndani ya Bajaj.
Akiwa kwenye Bajaj pamoaja na Askari akipelekwa kupatiwa matibabu.Picha Na Yusuph Badi Wa Tanzania Live Blog

Read more: http://audifacejackson.blogspot.com/2013/08/mwanajeshi-amgonga-raia-baada-ya.html#ixzz2ahwDMDXw

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...