facebook likes

Monday, August 12, 2013

Chelsea waibamiza Roma bao 2 - 1 kwenye mechi ya kirafiki

Burudani ya mchezo wa timu mbili ziliminyana vikali  kwenye mchezo wa kirafiki mjini  Washington D.C nchini Marekani na kushuhudia timu ya Chelsea kushinda mabao 2-1 dhidi ya Rome,


Blunder: Roma's Erik Lamela opened the scoring, taking advantage of a mistake from Mark Schwarzer
Bao la kwanza: Mshambuliaji hatari wa Rome Erik Lamela alipofunga goli la kujishtukizia. Photo Credits: dailymail.co.uk
.......SOMA ZAIDI NA ANGALIA VIDEO....
Rome ndio walioanza kufungua dimba mnamo dakika ya 20 baada ya ya kipa wa timu ya Chelsea Mark Schwarzer kufanya kosa ndani ya lango kwa mpira uliorudishwa nyuma na beki wake wa kushoto Ryan Bertrand huku kipa akitaka kuremba mpira uliorudishwa nyuma matokeo yake kujikuta mpira umemcheza na kugonga mwamba bila ya kuweza kuudhibiti hapo mshambuliaji wa timu ya Roma Erik Lamela akijikuta kupata mwanya wa kufunga goli la kiubwete ndani ya lango la timu ya Chelsea kipindi cha kwanza.

Helping hand: Chelsea midfielder Frank Lampard celebrates his goal against Roma with his team-mates
Furaha za goli: Kiungo wa timu ya Chelsea Frank Lampard  akisherehekea  bao la kusawazisha. Photo Credits: dailymail.co.uk
Timu ya Chelsea katika kipindi cha pili iliingia uwanjani na nguvu mpya za matumani  ya ushindi kwa mpambano wa vuta ni kuvute dhidi ya timu ya Rome kutoka nchini Italy, bao la kusawazishwa lilifungwa dakika ya 60 na mshambuliaji hatari Frank Lampard  baada ya kuachi kombara kali njee ya 18 na kujikuta Rome kuelimewa duru la pili dhidi ya Chelsea iliokua ikipiga makombora ya mbali.

Rome walijitahidi sana kimchezo pamoja na kushambulia kipindi cha pili, wakipapatuana na kila mmoja kutaka usindi wa mchezo huo, mnamo dakika ya 89 ilikua vuta nikuvute katika lango la Rome ndipo mshambuliaji hatari wa Chelsea Romelu Lukaku alipopata mwanya wa kuipatia timu yake bao la pili,  hadi muamuzi wa mpambano waburudani hiyo, Amando Villarreal  alipopuliza pinga yake ya mwisho, na kujikuta timu ya Chelsea Roma inatoka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya timu ya Rome ndani uwanja cha RFK Stadium, Washington, D.C

Winner: Morgan de Sanctis turns to watch as Chelsea's Romelu Lukaku scores late on
Mshambuliaji w wa bao la ushindi Romelu Lukaku alipotingisha nyamvu za Rome Siku ya Jumamosi , Aug 10, katika uwanja cha RFK Stadium, Washington, D.C. Photo Credits: dailymail.co.uk

Wapenzi wa timu zote mbili waliofurika katika burudani ya mpambano kati ya Chelsea na Rome ya Italy  Siku Jumamosi , Aug 10, katika uwanja cha RFK Stadium, Washington, D.C
ANGALIA VIDEO HAPA

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...