facebook likes

Saturday, July 6, 2013

ZITTO KABWE NA KODI YA SHILINGI 1000 KWA MWEZI


Maneno haya yameandikwa na Mh. Zitto Kabwe, jana tarehe 4 Julai kupitia akaunti yake ya Facebook:

“Kodi ya Tshs 1,000 kwa mwezi Kwa kila kadi ya simu uliyonayo imeanza rasmi. Bunge la wananchi, wawakilishi wa wananchi, limepitisha kodi hii. Hailipwi na kampuni ya simu, inalipwa na Wewe mwenye simu. Kampuni ya simu inakusanya Kwa niaba ya serikali. Ingawa sikuwepo wakati kodi hii inapitishwa na Bunge siwezi kukwepa wajibu wa kuaibika kuwa sehemu ya Bunge hili. Ni aibu Kwa kuwa pendekezo la kodi hii 

liliondolewa na Waziri wa Fedha kwenye hotuba yake ya makadirio ya mapato ya Serikali. Pendekezo lilirudishwa namna gani kupitia muswada wa fedha, finance bill, Haieleweki. Ni skandali. Nasikia vibaya sana kuwa mbunge kwenye Bunge lenye maamuzi ya namna hii. Nasikia aibu zaidi kwamba hatukupiga kelele za kutosha kuzuia jambo hili.”

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...