facebook likes

Saturday, July 6, 2013

Kwa Akina DADA: Hizi ndizo sababu kuu TANO za kwa nini Hauolewi mpaka sasa..

1.We MUONGO
 
Mwanamke kuwa muongo katika mapenzi ni kitu kibaya sana kinachosababisha wanaume wengi kupoteza
imani naye kuweza kuishi naye kimaisha katika maisha yao yote.

2.MBINAFSI
Mwanamke hapaswi kuwa mbinafsi katika maisha ,waweza kuta mwanamke kila pesa ipatikanayo ye huanza kuipangia bajeti kwa vitu vyake binafsi visivyo na faida kwa wote,kwa mfano kuwaza kununua nguo mpya ,vipodozi n.k,pia mwanamke kupenda familia ya upande na kuichukia familia  ya upande wa mwanaume pia huo ni ubinafsi unao chochea kuto olewa.

3.MALAYA
mwanamke malaya siku zote wanaume ni vigumu kumuoa kwani wanajua hawezi kuishi naye kwa uaminifu kutokana na tabia yake hiyo mbaya,hivyo ataishia kuchezewa na mwisho wa siku ataachwa kwenye mataa

4.HUNA FIKRA PEVU
Mwanamke asiyekua na fikira ktk mahusiano ni vigumu kuolewa kwani utakuta ye kila kitu humtegemea mwanaume atoe maamuzi wakati dunia ya sasa yapaswa wote kushirikiana katika maamuzi

5.KUMPENDA MTU USIE ENDANA NAYE
hakikisha umpendae mnaendana naye kuliko kumpenda mwanaume kwa ulazimu bila kuendana naye,waweza kuwa umempenda sababu ya pesa,au umempenda sababu ya u staa wake ,mwishowe ye atakuchezea na kukuacha ukishangaa.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...