facebook likes

Saturday, July 6, 2013

Usajili unaomiliki Headlines NBA !

imageMchezaji wa Los Angeles Lakers Dwight Howard hatimaye amefikia maamuzi ya timu atakayoichezea baada ya kuwa kwenye hali ya utata kwa muda mrefu . Howard ameamua kujiunga na Houston Rockets ambayo ilikuwa moja ya timu tano zilizokuwa zinataka kumsajili.
Howard alijiunga na Lakers akitokea Orlando Magic msimu uliopita ambapo alicheza Lakers kwa mkataba mfupi huku akiwa na uchaguzi wa kusajiliwa na timu nyingine kwa muda mrefu .
Los Angeles Lakers walimtumia nyota wake Kobe Bryant kumshawishi Howard kubakia na Lakers lakini mchezaji huyo alivutiwa na Houston Rockets ambayo ilimuahidi kusajili wachezaji wengine nyota ambao wataipa timu hiyo nafasi ya kuwania ubingwa.
Timu nyingine zilizokuwa zinamsaka Dwight Howard ni Dallas Mavericks,Golden State Warriors na Brooklyn Nets .
Howard amesaini mkataba wa miaka mitano na timu hiyo ambapo ataungana na nyota wengine kama Jeremy Lin na James Harden huku Wakitarajia kumuongeza Josh Smith toka Atlanta Hawks kuongeza nguvu.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...