facebook likes

Thursday, July 25, 2013

Uliwahi kuwaza kupima malaria kutafikia kutumia application ya simu kama hivi?



mini-IMAGINE2-e1374124657569
Sanyansi na teknolojia ndio vitu vinavyo run dunia kwa sasa, unaambiwa kutokana na ugunduzi ambao Microsoft wenyewe wameutambua na kuwapa zawadi ya dola za Kimarekani elfu kumi na mbili vijana waliofanikisha ugunduzi huo, hivi sasa inawezekana kupima malaria bila hata kutoa damu lakini hapohapo doctor wako akatumiwa taarifa za vipimo kwa njia ya electronic.
Kwenye mashindano ya  Microsoft Imagine Cup kwa ajili ya vijana, vijana wanne kutoka Uganda wameweza kujishindia kiasi cha zaidi ya millioni 19 za kitanzania kwa kutengeneza Windows Application ambayo inafanya kazi na kifaa kingine kidogo cha nje ambacho mgonjwa anaweka kidole kama inavyoonekana kwenye picha ili application itoe majibu ya hali ya malaria mwilini.
Application hiyo waliyoipa jina la Matibabu kwa sasa inafanya kazi  na windows phone lakini ili uweze kupima malaria unahitaji hiki kifaa cha nje.
safe_image

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...