facebook likes

Thursday, July 25, 2013

MESSI AKIRI KUATHIRIWA NA KUONDOKA KWA VILANOVA.


MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Barcelona, Lionel Messi amekiri kuwa matatizo ya kiafya ya Tito Vilanova yamekuwa pigo kubwa kwao lakini ana uhakika kuwa timu hiyo itafanikiwa kupita katika kipindi hicho kigumu cha kuondoka kwa kocha huyo. Vilanova alitangaza kujiuzulu wiki iliyopita ili aweze kuendelea na matibabu yake ya saratani na Barcelona ikamteua kocha wa zamani wa Newell Old Boys, Gerardo Martino kuchukua nafasi yake. Messi amesema wamesikitishwa kwa kilichotokea kwa Vilanova lakini kikosi chao bado kipo imara na wataendelea kusonga mbele kwa heshima yake. Messi ambaye alicheza dakika 45 katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Bayern Munich jana ambao walichapwa kwa mabao 2-0, amesema kwasasa yuko fiti na majeruhi yaliyokuwa yakimsumbua msimu uliopita yamekwisha.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...