facebook likes

Saturday, August 3, 2013

YALIYOJIRI WIKI YA UNYONYESHAJI : Miiko, mila zinazokwamisha unyonyeshaji


Mkazi wa eneo la  Losikito Paulina Richard akimnyonyesha mwanaye Magreth Richarde.
  • Anaeleza pindi anapokuwa mjamzito hapati vyakula vinavyohitajika kama lishe hivyo analazimika kutumia muda mwingi kufanya vibarua vya kumwingizia kipato, hivyo kutokana na uhaba wa fedha hulazimika kwa siku kupata mlo mmoja.

Wanaume wengine hukimbia wenza baada ya kuwapa mimba
Arumeru. Hali ngumu ya maisha ni  chanzo cha lishe duni kwa mama mjamzito hata mtoto anayetarajiwa kuzaliwa kwa kuwa wengi wao hutumia muda mwingi kujitafutia kipato.
Imekuwa ni jambo la kawaida kwa jamii ya Kimasai hasa wanaume kuwaacha wanawake zao nyumbani huku wakiwaachia majukumu yote wanawake hao wakihangaika kutafuta maisha ili waweze  kuendesha maisha inayomzunguuka.
Mama mjamzito anatakiwa ale chakula kwa siku mara nne asubuhi apate kifungua kinywa na kuanzia saa 3 hadi saa 4 asubuhi anatakiwa apike uji ambao ni lishe wenye mchanganyiko kama  mahindi, mtama mweupe na karanga ambao akinywa utamjenga mtoto aliye tumboni.
Vyakula hivyo vitamsaidia kutengeneza virutubisho muhimu katika maziwa ambayo anatarajiwa kunyonya mtoto atakayezaliwa.
Hivyo,  mtoto anapozaliwa zaidi ya saa moja anyonye maziwa ya mama yake kwanza ambayo yana virutubisho vyote vya kumlinda mtoto huyo.
 Hata hivyo, hali ni tofauti kwa jamii hiyo ya Kimasai ambako asilimia kubwa ya wanaume wakishawapa mimba wake zao, wengi husafiri na kwenda nje ya mkoa wao kutafuta maisha au hata kuoa mke mwingine .
Neema Sanare,  mkazi wa  eneo la Losikito Kata ya Mwandeti Wilaya ya Arumeru Magharibi mkoani Arusha anaeleza kuwa yeye ni mjamzito kwa sasa ana mtoto mwenye umri wa miaka mitatu lakini pindi anapokuwa mjamzito hadi kujifungua mume wake huwa anaondoka kwenda kwa mke mwingine.
Anaeleza pindi anapokuwa mjamzito hapati vyakula vinavyohitajika kama lishe hivyo analazimika kutumia muda mwingi kufanya vibarua vya kumwingizia kipato, hivyo kutokana na uhaba wa fedha hulazimika kwa siku kupata mlo mmoja.
Sanare anasimulia akiwa na hali hiyo au analea mtoto, mume wake huwa hamjali na anahamia kwa mwanamke mwingine au anasafiri kwenda Kenya kutafuta maisha.
“Kama hivi nina wakati mgumu ni kawaida yake nikishakuwa mjamzito hadi najifungua, mwanaume haonekani hadi mtoto atakapofikia umri wa miaka mitatu.
Anasema alipojifungua mtoto wake wa kwanza mume wake aliondoka na kumwacha akiwa na mama  mkwe  ambaye alikuwa anamtunza, lakini mtoto alipofika miezi minne alilazimika kufanya shughuli ya kumpatia kipato ili aweze kuishi.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...