facebook likes

Friday, July 5, 2013

KABULA AKERWA NA ‘WANAUME SURUALI’

Na Imelda Mtema
MSANII wa filamu za Bongo, Miriam Jolwa ‘Kabula’ ameonesha kukerwa na wanaume ambao hawana hela ‘wanaume suruali’ lakini wamekuwa wakijifanya wanajua kupenda sana huku wakiwa na wivu kupitiliza.


Miriam Jolwa ‘Kabula'
Akipiga stori na paparazi wetu juzikati, Kabula alisema anajua kupenda ni suala la msingi lakini anawashangaa wale wanaokuwa na wivu wa kupindukia na wakati mwingine kutoa vipigo kwa wapenzi wao wakati wao ni wanaume ‘suruali’.
“Unajua nawashangaa sana wanaume wa aina hiyo, wanakuwa na wivu kupitiliza lakini hawawasaidii chochote wapenzi wao zaidi ya kuonesha wana wivu kweli na wakipishana kidogo tu kipigo kinatembea, mimi wananikera sana,” alisema Kabula.

SOURCE; Globalpublishers

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...