Mwandishi wa habari Shaffih
Dauda ameripoti kwamba nahodha wa timu ya Taifa ya Cameroon Samuel Etoo
amejiondoa kwenye kikosi chake kitakachocheza na Taifa Stars kwenye
mchezo wa kimataifa wa kirafiki february 6 2013 uwanja wa Taifa jijini
Dar Es Salaam.Mwanzoni Kocha wa Cameroon alisikika kwenye AMPLIFAYA ya CLOUDS FM akiomba radhi kutokana na baadhi ya wachezaji wake kuchelewa kufika Tanzania na akatoa ahadi kwamba mpaka february 6 asubuhi ana imani wachezaji wote watakua wamewasili.
Sababu hasa ambazo zimemfanya Etoo kushindwa kuja Tanzania safari hii ni matatizo ya mgongo unaomsumbua kwa sasa.
Kwenye line nyingine kocha wa Cameroon kasema sababu zilizofanya wachezaji wengine kuchelewa kufika Tanzania ni nchi za mbali wanapofanyia kazi, wanacheza Ulaya hivyo ni safari ambayo sio fupi.
No comments:
Post a Comment