facebook likes

Wednesday, February 6, 2013

Mzee Majuto amwomba JK trekta



NGULI wa sanaa za maigizo na uchekeshaji nchini, Amri Athumani, maarufu kama ‘King Majuto’, amemwomba Rais Jakaya Kikwete amsaidie trekta ili ajikite zaidi kwenye kilimo cha kisasa mkoani Tanga.
Mzee Majuto alimwomba Rais Kikwete trekta hilo juzi alipohojiwa kwenye kipindi cha ‘Mkasi’ kinachorushwa na kituo cha runinga cha EATV, na kuongeza kuwa, anamiliki ekari 10 za shamba ambazo hawezi kulima kwa jembe kutokana na umri wake.
“Najua Rais Kikwete anawajali wasanii na sasa ananisikiliza, naamini atanisaidia, namwomba Rais Kikwete anisaidie kupata trekta ili nami nilime kisasa, bei ya trekta moja ni sh milioni 25, mimi uwezo huo kwa kweli sina… shamba langu lina ekari 10, umri wangu huu kulima kwa jembe mabega yatashuka.
“Nataka kuwekeza kwenye kilimo cha kisasa kule kwetu, hata mtu akinitaka nifanye filamu yake lazima anifuate kijijini, anikute na kazi yangu, najua hata malipo yatakuwa mazuri,” alisema.
Awali mwigizaji huyo alieleza masikitiko yake kwa serikali kushindwa kuendeleza viwanda, mashamba, bandari na reli vilivyokuwapo awali mkoani Tanga.
Kadhalika, Mzee Majuto ameishukuru serikali kwa kukubali kutambua kazi za wasanii na kuziweka stika za Mamlaka ya Mapato (TRA), huku akisisitiza umoja na mshikamano miongoni mwao

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...