facebook likes

Sunday, August 11, 2013

HUYU NDO MGONJWA ANAYESHINIKIZA KUHARAKISHIWA KIFO CHAKE ILI ACHANGIE VIUNGO VYAKE KWA WENGINE


Sherri Muzher (kushoto) na Dk Jack Kervorkian.
Mwanamke aliyefikia hatua za mwisho kabisa za uhai kutokana na ugonjwa anapambana kuhitimisha maisha yake ili aweze kuchangia viungo vyake kuwezesha wengine waishi.
.......SOMA ZAIDI.....
Sherri Muzher, mwenye miaka 43, kutoka Detroit, Michigan, alikuwa na miaka 27 tu pale alipogundulika na ugonjwa wa kukacha kwa tishu wakati wa majira ya joto baada ya mwaka wake wa kwanza katika shule ya sheria.
Hali hiyo ya kutoponyeka, ambayo husababisha mfumo wa kinga kushambulia mfumo wa fahamu mwilini, umeshuhudia mwili wake ukidhoofika kwa kasi, ukimwacha akiwa hawezi kutembea na kuongea kwa shida.
Anasema sasa anataka kushika hatamu za maisha yake - kwa kuchagua siku atakayokufa.
"Ni heri nisaidie kuwapa uhai wengine wakati viungo vyangu vingali vinaweza kutumika,"alisema. "Ni ukweli wangu. Ninazidi kudhoofika. Misuli dhaifu katika kuongea kwangu, kila kitu. Hii kwa haraka inafikisha ukweli mahali pake."
Kuhusiana na hali yake, aliongeza: "Ni hasara kubwa - hasara kwa kuongezeka MS. Ni mchakato wa kusikitisha, sababu unapoteza uhuru wako kwa kasi."
Mtaalamu wa weledi wa kitabibu alisema wakati kesi ya Muzher ikivutia mno, inatatizwa na ukweli kwamba anaishi mjini Michigan, ambayo bado inawindwa na kesi ya Dk Jack Kervorkian.
Daktari huyo, ambaye alipachikwa jina 'Dokta Kifo', alikuwa mwanaharakati wa kifo cha huruma ambaye alidai kuwa alisaidia vifo vingi vinavyofikia 130.
Mwaka 1999, alikamatwa na kujaribiwa kwa mchango wake katika kesi ya kifo cha hiari na akatumikia miaka minane ya hukumu ya kifungo cha miaka 10 hadi 25.
"Inafikiri hiyo itawezekana [sheria hiyo inaweza kubadilika mjini Michigan], lakini ni kitu fulani ambacho mjini Michigan pekee kinaweza kuzusha utata mno hasa kwa kuzingatia historia ya Dk Kevorkian," alisema Lance Gable, profesa wa sheria katika Chuo Kikuu cha Wayne State.
"Ushawishi wake unaonekana kukatisha mno tamaa. Anataka hatamu zote za hatima yake na pia kusaidia watu wengine, na nafikiri hiyo ni habari inayovutia mno kusimulia."
Kujiua kwa msaada wa daktari inaruhusiwa kisheria huko Oregon, Washington, Vermont na Montana pekee.
Mweledi wa tiba Dk Michael Stellini alisema kwamba kesi hiyo itawasilishwa kwa matatizo.
"Kama tunasubiri kwa muda mrefu, hatoweza kuchangia," alisema. Kama tutafanya mapema mno, hatokuwa mwishoni, na hiyo inaibua mambo yote yanayohusu masuala ya weledi."
Aliongeza kwamba sheria inaweza pia kuibua maswali mengi yahusuyo weledi katika siku za usoni.
Lakini wakati Muzher akisema mapafu yake hayawezi tena kufaa, anaamini kwamba kwa kuruhusiwa kufa pale atakapochagua kutamwezesha kugawa kwa figo, maini, moyo na viungo vingine kwa wote wanaohitaji.
"Ni heri nibaki mwenye umuhimu na msaada, kuliko kutupiliwa mbali na kutokuwa na uwezo wa kusaidia," alisema. "Kitakachonipa faraja ni kufahamu nimeacha urithi wa kuwapatia uhai wengine."

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...