Akizungumza
 jijini Dar es Salaam baada ya Stars kuwasili, Meneja wa Bia ya 
Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe alisema licha ya habari hizi 
kutokuwa njema kwa watanzania, ni vizuri kukubali matokeo na kuangalia 
picha kubwa na malengo ya muda mrefu.
“Ni
 vyema tukumbuke kuwa kwenye mpira kuna kushinda na kushindwa,” alisema 
Bw Kavishe na kuongeza, “Tunapenda kuwahakikishia watanzania kuwa sisi 
kama wadhamini hatujakata tama na bado tuna imani na timu hii na kocha 
Kim Poulsen kwa hivyo tunawaomba watanzania wasife moyo.”
Alisema
 wakati  walipoanza kuidhamini Taifa Stars mwezi Mei mwaka jana na 
kuwekeza zaidi ya shilingi bilioni mbili kwa mwaka, kwa muda wa miaka 
mitano, walikuwa na malengo kadhaa ikiwemo kuinua hadhi ya Timu ya 
Taifa, kuhakikisha wanaingia kambini kwa muda unaotakiwa, wanalipwa 
vizuri, wanakula na kulala vizuri na kusafiri vizuri.
“Tumejitahidi
 kufanya mambo haya kwani wachezaji sasa hivi wana DVD zenye maelezo 
yao, tumewapa suti mpya na za kisasa na pia tumewapa basi jipya la 
kisasa. Mambo haya yote pamoja na mambo wanayofundishwa na Mwalimu Kim 
Poulsen yamesaidia kuleta mabadiliko kwa timu ya Taifa,” alisema.
Alisema
 kuna mafanikio mazuri ya timu ya taifa ambayo watanzania lazima 
wayakumbuke kama kuzifunga timu kama Zambia, Cameroon, Morocco na Kenya.
Kwa
 mujibu wa Meneja huyo walipoanza udhamini  Tanzania ilikuwa katika 
nafasi ya 145 kwa mujibu wa FIFA lakini sasa imesogea hadi 109. “Haya ni
 mafanikio makubwa kwani tumesogea hatua zaidi ya 40,” alisema.
Alisema
 safari ya mafanikio katika mpira ni ndefu na inahitaji uvumilivu wa 
hali ya juu na kuongeza kuwa Kocha Kim Poulsen anafanya kazi nzuri ya 
kuibua vijana.
“Kocha
 anahitaji kuungwa mkono na sisi sote kuanzia kwa TFF, sisi wadhamini na
 watanzania wote. Tunahitaji kuangalia picha kubwa,” alisema na 
kuongeza,”Nawaomba watanzania tuwe wazalendo wakati huu hii ni timu yetu
 na tunatakiwa kujivunia. Vyombo vya habari pia viwe mstari wa mbele 
kuonesha uzalendo.”
Alisema
 mechi  dhidi ya Gambia itakayochezwa mwezi wa 9 ya kuwania kufuzu Kombe
 la Dunia ni muhimu hata kama Tanzania haisongi mbele kwani itasaidia 
katika ngazi za FIFA.
source bin zubeiry
![]()  | 
| Wachezaji wa Taifa Stars wakiwasili jana usiku kutoka Uganda | 
source bin zubeiry

No comments:
Post a Comment