facebook likes

Monday, July 29, 2013

"TANZANIA SI MALI YA CCM WALA CHADEMA"......MSIGWA


Picture

Mheshimiwa Peter Msigwa akifunguka katika kipindi cha Makutano na Fina Mango


Picture


Fina Mango akimsikiliza Mchungaji Peter Msigwa wakati akijibu moja ya maswali katika kipindi cha Makutano.


Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa amesema Tanzania sio mali ya chama chochote cha siasa wala kundi lolote la watu wakati akihojiwa katika kipindi cha Makutano na Fina Mango. 

Mheshimiwa Peter Msigwa alitoa kauli hiyo alipoulizwa anaonaje mwamko wa kufanya mabadiliko unaoendelea ikiwemo mchakato wa katiba mpya. 

Aliwalaumu watu wa kipato cha kati kwa kusema wao ndio kikwazo cha maendeleo kwa sababu ya kuridhika na vitu vidogo walivyovipata, "Kila mtu aingie acheze huu mchezo kwamba ni wakati uliofika wa kuibadilisha Tanzania, tuibadilishe kifikra. 

Watu wengi mmekaa maofisini na kompyuta zenu na vijumba vidogo mmejenga na vigari vidogo mmeweka nje mnaogopa, lakini kama tutaendelea kuruhusu akili ndogo iendelee kutawala hatutaenda popote" alisema Mheshimiwa Msigwa. 

Hata hivyo aliipongeza tume ya katiba kwa kusema ameridhishwa na ilivyofanya kazi yake kutokana na hofu waliyokuwa nayo baada ya mchakato wa kuandaa katbiba mpya ambao ulianzishwa na CHADEMA kuchukukuliwa na kugeuzwa agenda ya chama tawala na hivyo kuleta wasiwasi wa haki isingetendeka hasa ile ya uwakilishi katika utoaji maoni ya katiba.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...