KLABU ya Al Ahly ya 
Misri imeliomba Shirikisho la Soka barani Afrika-CAF kusogeza mbele 
mchezo wao dhidi ya Orlando Pirates ya Afrika Kusini mpaka Agosti 9 
mwaka huu. Mkurugenzi
 wa michezo wa Al Ahly Sayed Abdul Hafez alithibitisha timu hiyo 
kuandika barua rasmi kwa CAF ya kusogeza mbele mchezo huo mpaka Agosti 9
 badala ya Agosti kama ulivyopangwa kwasababu ya mfungo wa mwezi wa 
Ranadhan ambapo wacheza wengi wa timu hiyo wanakuwa wamefunga. Hafez
 pia aliongeza kuwa Wizara ya mambo ya Ndani ya nchi hiyo imekataa 
kuwawekea ulinzi kwa ajili ya mchezo huo jijini Cairo au Alexandria 
hivyo wanatarajia mechi hiyo kuchezwa katika mji wa El Gouna au Aswan. Hafez
 amesema wamefikia hatua hiyo baada ya timu hiyo kucheza dhidi ya 
Zamalek mchana na wachezaji kukataa kufungulia ambapo wote waliathirika 
mpaka hivi sasa kutokana na kucheza kwenye jua kali huku wakiwa 
wamefunga. Naye 
kocha wa Pirates Roger De Sa ameonyesha wasiwasi wake wa kucheza na Al 
Ahly jijini Cairo kutokana na vurugu zinazoendelea lakini anaamini kuwa 
CAF itatoa uamuzi sahihi kuhusiana na mahali patakapochezwa mchezo huo.

No comments:
Post a Comment