facebook likes

Wednesday, July 24, 2013

Kwa aina hii mpya ya bajaj iliyoingia Tanzania…wachina wanaendelea kutisha kwa ubunifu.


OLYMPUS DIGITAL CAMERA
Wakati bajaj zinaanza kufanya kazi kulikuwa na ugomvi kati ya taxi na bajaj kwasababu ya kile kilichodaiwa kwamba ni kuchukuliana wateja hadi pale serikali ilipowatambua madereva bajaj kwa kuanza kulipa kodi. Hivi sasa kuna kampuni ya wachina ambayo imeingiza aina mpya ya bajaj tofauti na zilizoeleka hapa Dar na kwingineko. Bajaj za  kawaida zinauwezo wa kubeba abiria watatu tu nyuma na kama abilia ana mzigo itabidi aubebe mwenyewe.  Hii bajaj mpya inauwezo wa kubeba abilia watano nyuma na wakakaa vizuri bila shida. Kiti cha mbele kinabeba watu wawili hivyo kuongeza idadi ya abilia hadi sita. Kitu kingine kizuri ni kwamba kuna sehemu maalum kabisa ya kuwekea mizigo ya abilia na bajaj ikatembea bila hata watu wengine kujua kwamba kuna mizigo imebebwa. Watu wa sokoni hii kitu wataifurahia zaidi kwasababu ya hii sehemu ya kuwekea mizigo yao wakitoka kununua.
Hawa jamaa walikua wana-test kidogo raha ya bajaj mpya
Hii ni sehemu ya mizigo ya abiria ambayo bajaj nyingi hazina.
Ukishaweka mzigo panafunikwa kama hivi na safari inaendelea
OLYMPUS DIGITAL CAMERA
Kiti cha mbele kimezidi upande wa kushoto ili abilia mwingine akae
Hapo ni kwa mbele
Unaambiwa ukinunu moja ni milioni 6.5, ukinunua mbili kila moja ni millioni 6.4 na ukinunua kumi kila moja ni millioni 6.1. Zinapatikana Dar hivi sasa. Engine yake ni 150cc.
8745175
Lakini pia unazikumbuka hizi bajaj, zilikuwepo kadhaa ndani ya Dar es salaam chache sana kwa ajili ya promosheni ya Vodacom kipindi flani kilichopita lakini hazikuwa zinauzwa kubeba abiria.

source:millardayo

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...