facebook likes

Wednesday, July 24, 2013

HATIMAYE JOSEPH OWINO KURUDI MSIMBAZI BAADA YA KURUDI KWENYE KIWANGO CHAKE


Beki wa URA ya Uganda Joseph Owino anategemea kujiunga na timu ya Simba ambayo alikuwa akiichezea misimu mitatu iliyopita kabla ya kujiunga na Azam kutoka Mbagala Jijini Dar-es-salaam.

Beki huyo alirejea kwao Uganda baada ya kupata majeraha na kushindwa kucheza katika timu za Simba na Azam akiwa kwenye kiwango chake kama alivyokuwa akicheza kabla ya kuumia.

Baada ya kurudi Uganda Owino alitibiwa na kupona vizuri kisha kujiunga na URA ambayo amekuwa mpaka sasa. Viongozi wa benchi la ufundi la Simba Kocha Abdallah King Kibaden, msaidizi wake Julio ana meneja Moses Basena wote waliridhishwa na kiwango cha Owino na hivyo kupeleka maombi kwa uongozi kumsajili mchezaji huyo. 

Viongozi wa Simba sasa wapo kwenye hatua za mwisho za kukamilisha dili hilo na kumrudisha Owino msimbazi, sehemu ambayo aliichezea kwa mafanikio makubwa sana alipojiunga na timu miaka kadhaa iliyopita.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...