facebook likes

Thursday, August 15, 2013

JESHI NIGERIA "LAMUUA" KAMANDA WA BOKO HARAM

Jeshi nchini Nigeria limetangaza kuwa limemua kiongozi wa ngazi ya juu wa kundi la Boko Haram. 
.....SOMA ZAIDI.....
Taarifa hizo za kijeshi zemesema kuwa kiongozi huyo aliyeuwawa ni Momodu Bama,ambaye ni wa pili katika uongozi wa kundi hilo la wapiganaji.
Mapema mwezi huu wafuasi wengine wa kundi hilo la Boko Haram ambao walikuwa wamekamatwa walifichua kwamba huyo kamanda wao alikuwa ameuawawa.
Msemaji wa Jeshi Brig Jenerali Chris Olukolade amesema Momodu Bama, ambaye pia anafahamika kama "Abu Saad", alikuwa na ujuzi wa kufyatua makombora ya kutungua ndege.
Mapema mwezi wa Mei, Nigeria ilitangaza hali ya hatari katika maeneo ya kaskazini Mashariki mwa nchi ili kupambana na wapiganaji wa Boko Haram.
Hata hivyo hadi sasa hakuna taarifa huru kuthibitisha kuuwawa kwa Bwana Momodu Bama nao Boko Haram wenyewe hawaja thibitisha kifo cha kiongozi huyo.
Jenerali Olukolade, alisema Momodu Bama alikuwa ni mmoja ya viongozi wa Boko Haram waliokuwa wakitafutwa zaidi na kulikuwa kuna zawadi ya dola $155,000, £100,000 kwa yeyote atakaye toa habari zitakazosaidia kukamatwa au kuuwawa kwake

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...