facebook likes

Wednesday, June 26, 2013

UCHAMBUZI WA KIMBUZIMBUZI WA MAGAZETI YA LEO


 Okay  okay okay, kuna maswali kadhaa yanahitaji majibu, Alinunua lini hii meli? Je aliicheki kama haina matundu chini? Je alinunua road licence? Ilikwisha lini? Alinunua Uchina? Kuna maswali kadhaa ambayo bodi ya wakurugenzi wa blog tumeona tujiulize kabala hatujatoa msimamo wa blog.

 Dah Mbunge kamloga nani tena? Inajulikana kuna wengi wanatumia teknolojia hiyo, sasa huyu mpaka akasimamishwa ina maana alipewa masharti ya ziada. Au alianza kuzima nyota za wenzie? Au alivunja yai viza kwenye ukumbi wa Bunge? Why why, aftaol ukubwa huku Afrika unaambatana na utamaduni kidogo au siyo?

 Ajali ni kitu kinachotokea kwa bahati mbaya, sasa ishu ya watu kufanya makusudi kwanini iitwe ajali? 

 Hii itakuwa ni kwa kuwa mashine zetu za kunyongea hazifanyi kazi, kwa hiyo tumelazimika kupata wawekezaji katika taaluma hiyo. Kwa hiyo ishu ya kunyongwa ukihukumiwa hapa kufanyika Ulaya.Teh teh teh kuna watu walivyo waroho wa kwenda majuu watang'ang'ania kwenda kunyongwa Marikani

Sasa huu ni ukorofi, nyie ndie wenye mitambo ya simu sasa na nyie eti mnabip dah, serikali ikiwapigia mtaidai hela ya kupiga, acheni hizo jamani pigeni simu kieleweke mnabip hata nyie?

Usupa sta kazi kweli, eti ukikuna kichwa watu wanaandika, ushauri kwa masupasta mkiona sehemu nyingine fulani zinawasha msikune hadharani watawaandika. Supasta nanihii kakuna tako, yule mwingine kakuna kwapa hahahahaha
 
 
THANKS TO CHEKA NA KITIME

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...