facebook likes

Wednesday, July 3, 2013

FEZA KESSY AENDEKEZA TABIA YA KUPIGWA DENDA NDANI YA JUMBA LA BIG BROTHER


Mshiriki  wa  Botswana, Oneal   ameendeleea  kuyafaidi  mate  ya  dada  yetu   ambapo  wakati  huu  jamaa  huyo aliamua kupiga magoti wakati akimwaga "sera za nguvu"  kwa Feza na kumwambia kuwa maisha yake yalikuwa shagala bagala kabla hajakutana na mwakilishi huyo wa Tanzania.


Maneno hayo matamu yalimwingia vyema Feza ambaye alikuwa akitabasamu muda wote kuashiria upendo mzito kwa jamaa huyo wa Botswana ambaye anataka wawe na maisha pamoja siku za usoni.


Washiriki wengine waliamka na kuwashangalia wapenzi hao kama yalivyo maisha ya kawaida. 

Muda  mfupi  baadaye, Feza  na  Oneal  walianza  kubadilishana  mate  na  ndimi...!!!!!!!

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...