facebook likes

Tuesday, July 30, 2013

MANCHESTER UNITED YA PIGA MTU 5-2


Mabingwa wa ligi kuu soka nchini England, Manchester United wamecheza mechi yao ya tano katika ziara yao ya kujiandaa na msimu mpya wa ligi dhidi ya  Kitchee ndani ya uwanja wa  Hong Kong  na kuibuka na ushindi wa mabao 5-2. (HM)
Mechi ya jana ilitakiwa kuchezwa mwishoni mwa wiki iliyopita, lakini Kocha wa United, David Moyes alilazimika kuahirisha mechi kwa madai kuwa uwanja wa Hong Kong ulikuwa mbovu kufuatia mvua kunyesha na uwanja kujaa matope, huku ukiwa umetumika mfululizo katika michuano ya kombe la  Barclays la Asia.
Hali ya uwanja siku ya jumamosi wakati wa fainali ya Sunderland na Manchester City ilikuwa mbaya sana, lakini viongozi walijitahidi kufanya jitihada za kurekebisha kabla ya mchezo wa jana.
Kikosi cha Kitchee: Comi, Rodriguez, Rehman, Kei, Alkande, Belencoso, Wai, Annan, Yang, To.
Wachezaji wa akiba: Jianqiao, Wen, To, Fung, Quankun, Hau, Fai, Paramo, Lam, Deshuai, Lung
Waliofunga Magoli yao: Lam (53), Alkande (69)
Kikosi cha Manchester United: Amos, Evra (Buttner HT), Anderson, Smalling, Carrick (Jones 72), Young (Januzaj HT), Welbeck (Lingard HT), Fabio (Rafael 72), Cleverley, Zaha, Keane.
Wachezaji wa Akiba: Lindegaard, Rafael, Jones, Ferdinand, Giggs, Van Persie, Buttner, Lingard, Januzaj.
Waliofunga mabao: Welbeck (16), Smalling (22), Fabio (26), Januzaj (47), Lingard (80).

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...