facebook likes

Tuesday, July 30, 2013

GUARDIOLA APANGA KUTOA UHURU ZAIDI KWA WACHEZAJI WAKE.


MENEJA mpya wa klabu ya Bayern Munich, Pep Guardiola anapanga kuacha umiliki wa chumba cha kubadilishia nguo chini ya himaya ya wachezaji wake ili waweze kujisikia huru wakati wa mapumziko. Katika Uwanja wa Allianz Arena ambao unamilikiwa na klabu hiyo, kocha huwa anakuwa na ofisi yake ndogo karibu na mlango wa kuingilia katika chumba cha kubadilishia nguo ambapo mara chache kocha aliyeondoka Jupp Heynckes alikuwa akiitumia kwa ajili ya kubakia karibu na wachezaji wake. Hata hivyo Guardiola anapanga kuwapa nyota wake uwanja mpana zaidi wa kuzungumza kwa uwazi na hata kukosoana wenyewe kwa wenyewe bila ya woga ndio maana ameamua kuanzisha ofisi nyingine mbali na chumba hicho. Guardiola amesema ni muhimu kwa wachezaji kupewa nafasi kwani ni eneo lao ambapo hutaniana na kuzungumza chochote bila woga na hata kumponda. Bayern inatarajiwa kuanza kutetea taji lao la Bundesliga Agosti 9 mwaka huu wakati watakapochuana na Borussia Monchengladbach.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...