facebook likes

Saturday, October 19, 2013

Kutana na Mwanamuziki Mzuri wa Kiafrika Ambaye Awali Alikuwa Mwanaume


Titica
Mwanamke huyu  kwa jina akijulikana kama  Titica, amekuwa ni gumzo kubwa nchini Angola.
 Siku chache zilizopita UNAIDS ilimpa heshima  mwanamke huyu aliyejibadili jinsia kuwa  Balozi wake.
SOMA ZAIDI........
Alizaliwa Luanda kama Teca Miguel Garcia,  akiwa muimbaji na mchezaji, Titica alibadili  maumbile yake miaka minne iliyopita mara
 baaada kufanya upasuaji wa maziwa  nchini Brazil.

Sasa, akiwa na miaka 26, Titica amekuwa 
kioo cha Angola kwa aina ya muziki anaoufanya
 wenye mchanganyiko wa miondoko ya rap na
 techno unaojulikana kama “kuduro”.

Akiongea na BBC mwaka jana, akiwa kwenye 
kwenye utengenezwaji wa video ya wimbo wake unaotamba sasa uitwao Olha o Boneco, wimbo
 ambao amemshirikisha muimbaji mashuhuri wa  muziki aina ya kizomba aitwaye Ary, Titica  alisema amefanikiwa kukabiliana na  vikwazo vyake.

“Shukrani kwa Mungu, nina furaha sana, 
imechukua muda kufika hapa na imehusisha  mambo mengi ya kujitolea ila asante Mungu,
 kila kitu kinakwenda sawa kwangu.
 
Nilikuwa nikipigwa mawe, nimekuwa nikipigwa  na kumekuwa na vikwazo vingi vya kisheria dhidi
 yangu, watu wengi walionyesha hilo. Kuna miiko  mingi sana,”.

Licha ya miiko hiyo, bado Titica anaonekana 
kuwa hana upungufu wa mashabiki huku wengi  wakiwa wanavutiwa zaidi na muziki wake kuliko
 jinsia yake.


No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...