facebook likes

Saturday, October 19, 2013

Bosi wa facebook anunua nyumba 4 zilizozunguka nyumba yake


ImageView
Uamuzi wa hivi karibuni wa kampuni ya Facebook wa kulegeza sera ya kutoingilia uhuru wa wateja ulisababisha gumzo lakini katika taarifa nyingine, imeripotiwa kwamba aliyegundua kampuni hiyo ambaye pia ndio bosi wake, Mark Zuckerberg ametumia dola za Kimarekani milioni 30 kununua nyumba nne za jirani kwake kulinda uhuru wake.
SOMA ZAIDI........
 mark-zuckerberg-palo-alto-rental-home-exterior-590jn011411
Bilionea huyo mwenye miaka 29 mwenye jumba lake la kifahari kwenye eneo la Palo Alto, amelipia dau kubwa zaidi kununua nyumba hizo jirani yake ambako aliyokuwa anaishi tokea mwaka 2011.
Pamoja na kwamba ana uwezo wa kununua nyumba hizo kwa ajili ya kupanua nyumba yake, inasemekana kwamba uamuzi wake umetokana na mjenzi mmoja kutaka kununua eneo la jirani na nyumbani kwake na kulitangaza kwa kutumia jina lake.
kwa mujibu wa vyanzo vya habari, Zuckerberg anampango wa kuzikodisha kwa wapangaji wa sasa ili baadae waweze kuzinunua moja kwa moja.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...