facebook likes

Friday, September 13, 2013

CHEKI JINSI GARETH BALE ALIVYOKUTANA NA RONALDO KWA MARA YA KWANZA

1
Wachezaji wawili wenye historia ya kuweka rekodi ya kuwa wachezaji ghali kuliko wote hii leo wamekutana kwa mara ya kwanza kabla ya mazoezi ya timu yao .

SOMA NA ANGALIA PICHA ZAIDI...

Gareth Bale na Cristiano Ronaldo walikutana kwa mara ya kwanza tangu wakati Bale aliposajiliwa na Real Madrid toka klabu ya Tottenham Hotspurs .
Bale amevunja rekodi ya Cristiano Ronaldo baada ya usajili wake kwenda Real Madrid kuigharimu klabu hiyo ya Hispania paundi milioni 86 akiwa ameuzidi usajili wa Ronaldo kwa paundi mdilioni 6.

2
Ronaldo na Bale dakika chache baada ya kukutana kwa mara ya kwanza.
Bale na Ronaldo walikutana hii leo mapema dakika chache kabla ya kuanza kwa mazoezi ya Real Madrid wakiwa wamejiunga na klabu hiyo baada ya kuziacha kambi za timu zao za taifa .
Bale alicheza kwenye mechi mbili za Wales ikiwemo mechi dhidi ya Macedonia iliyochezwa jana huku Ronaldo akicheza na kuifungia Ureno kwenye mchezo dhidi ya Ireland Ya Kaskazini na aliukosa mchezo wa jana kati ya Ureno na Brazil.
3
Bale akiwa na kocha Ancelotti ofisini kwake.
4
Bale akisalimiana na wafanyakazi wa Real Madrid.
6
Gareth Bale wakati akiwa anaingia jijini Madrid hii leo.
8
Gareth Bale akielekezwa kitu na kocha wa Real Madrid Carlo Ancelotti .

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...