facebook likes

Tuesday, July 16, 2013

Hawa ndio Watanzania wawili walioingia kwenye hii list ya Mamilionea 10 wa kutazamwa Afrika 2013

Patrick Ngowi 

Ninao uhakika kwamba hii ni ripoti nyingine ya kutoa nguvu kwa vijana ambao wamekata tamaa au bado hawaamini katika kile wanachoweza kukifanya kwa nguvu zao na akili zao, vijana ambao bado fikra zao ziko kwenye imani kwamba Matajiri wote wa sasa walianza kuingiza mamilioni mwezi wa kwanza tu baada ya kuanza biashara…. hawa hapa chini ni vijana chini ya umri wa miaka 39, wote ni kutoka Afrika na kila mmoja ana stori yake ya kuanzia mbali kimaisha…
Kwa mara nyingine tena kijana wa Kitanzania Patrick Ngowi (28) ametokelezea kwenye list ya Jarida maarufu la Forbes lakini kwa sasa katajwa kwenye 10 bora ya vijana wa Kiafrika mamilionea wa kutazamwa mwaka 2013 ambapo kampuni yake ya Helvetic Solar inayojishughulisha na ishu za umeme wa Solar inatarajiwa kuingiza dola za Kimarekani milioni saba kabla ya mwaka 2013 kumalizika.
Ni Mtanzania ambae aliwahi kusota sana kwenye kuzitafuta pesa, biashara yake ya kwanza ilikua ni vocha lakini kwa uvumilivu na malengo aliyokua nayo, kutokukata tamaa na kuota kuzifanyia kazi fikra za mbali ambazo vijana wengi wanazo ila hawajui jinsi ya kuzifikia, ndio kumempa haya mafanikio aliyonayo leo.
Ngowi
Mtanzania mwingine alietajwa kwenye hii list ni Mbunge wa Singida mjini (CCM) Mohammed Dewji a.k.a Mo Dewji mwenye umri wa miaka 38 ambae pia ni Young Global Leader kwenye World Economic Forum akiwa ni CEO wa METL ambayo unaambiwa imeajiri zaidi ya watu elfu 24
Mo Dewji Forbes
Dewji
Wengine ni Gerald Wamalwa (28) wa South Afrika, Sibongile Sambo, South Africa , Khanyi DhlomoSouth Africa , Colin Thornton, South Africa, Alan Knott-Craig Jr.South Africa, Igho Sanomi, Nigeria, Quinton van der Burgh, South Africa, Gerald Wamalwa, Kenya
na Ken Njoroge mwenye umri wa miaka 37 ambae ni Mkenya pia.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...