facebook likes

Tuesday, July 16, 2013

Barcelona kumpoteza nyota wake mwingine?

Cesc Fabregas akiwa na washkaji zake Gerard Pique na Sergio Busquets.
Cesc Fabregas akiwa na washkaji zake Gerard Pique na Sergio Busquets.
Zikiwa zimepita saa karibu 24 tangu ilipotangazwa kuwa Bayern Munich wamekamilisha usajili wa Thiago Alcantarra , Barcelona huenda wakalazimika kupoteza mchezaji mwingine wa safu ya kiungo baada ya  klabu ya Manchester United kutuma ofa ya kumsajili kiungo Cesc fabregas . United wakiugulia machungu ya kumkosa Thiago wametuma ofa ya paundi milioni 26 kwa ajili ya Fabregas wakiwa kwenye harakati za kuimarisha kikosi chake hasa nafasi ya kiungo ambayo kocha mpya David Moyes anaiona inahitaji kuongezewa nguvu .

Je Cesc ataungana na mshkaji wake wa nguvu wa enzi hizo RVP ndani ya Old Traford?
Je Cesc ataungana na mshkaji wake wa nguvu wa enzi hizo RVP ndani ya Old Traford?
United baada ya kutangaza hapo jana kuwa wana fedha za kufanya usajili wa nyota yoyote ambaye Moyes atamhitaji kwenye kikosi chake walipata pigo la kwanza baada ya taarifa ya Thiago kwenda Bayern kutoka rasmi baada ya mchezaji huyo kuripotiwa kuwa kwenye rada za David Moyes ambaye amekuwa akimtazama kama mrithi wa muda mrefu wa kiungo Paul Scholes ambaye amestaafu .
Usajili wa Fabregas hautakuwa rahisi kwani mchezaji huyo aliwahi kuichezea Arsenal siku za nyuma na klabu hiyo (Arsenal) ina chaguo la kwanza la kumsajili au kukataa kumsajili Cesc kwa mujibu wa mkataba wake wakati alipouzwa toka Arsenal kwenda Barca misimu miwili iliyopita .
Ugumu mwingine unatokana na ukweli kuwa Fabregas ana nafasi ya kudumu kwenye kikosi cha kwanza cha Barca na haitakuwa rahisi kwa klabu hiyo kuruhusu kiungo mwingine kuondoka baada ya Thiago . Hata hivyo maisha ya Fabregas tangu arejee Barca toka Arsenal hayajakuwa mepesi kama ilivyotarajiwa na wengi na kocha aliyeondoka Pep Guardiola aliwahi kupendekeza kuuzwa kwa mchezaji huyo baada kutoridhishwa na na kiwango chake .

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...