facebook likes

Tuesday, July 16, 2013

GERRARD KUSAINI MIAKA MIWILI ZAIDI LIVERPOOL.


NAHODHA wa klabu ya Liverpool, Steven Gerrard anatarajiwa kusaini mkataba mpya wa miaka miwili na klabu hiyo baadae leo. Mazungumzo baina ya wakala wa Gerrard na mkurugenzi mtendaji wa Liverpool Ian Ayre yamekuwa yakiendelea toka mwishoni mwa msimu uliopita na pande hizo mbili zimefikia makubaliano ambaye yatamuweka Gerrard Anfield katika kipindi cha miaka miwili ijayo. Mkataba wa sasa wa Gerrard unamalizika mwishoni mwa msimu ujao lakini meneja wa Liverpool Brendan Rodgers amemuhakikishia kiungo huyo mwenye umri wa miaka 33 kuendelea kuwepo hapo siku zijazo. Ni zaidi ya miaka 14 toka Gerrard alipoanza kuchezea kikosi cha kwanza cha Liverpool na mkataba mpya atakaosaini utamuhakikishia kumaliza soka lake katika klabu hiyohiyo. Liverpool imeanza ziara yake ya maandalizi ya msimu mpya wa ligi huku Australia na barani Asia.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...