facebook likes

Tuesday, July 16, 2013

BREAKING NEWS: BAADA YA MAN UNITED KUPELEKA OFA BARCA - FABREGAS ASEMA ANATAKA KUENDELEA KUBAKI CAMP NOU


Siku chache baada ya kumkosa Thiago Alcantara inaonekana sasa Manchester United ipo njiani kumkosa mchezaji mwingine kutoka FC Barcelona, Cesc Fabregas. Hii inakuja baada ya kocha wa klabu hiyo  Tito Vilanova kusema kwamba ameongea na kiungo huyo wa Spain na ameambia na mchezaji huyo kwamba anahitaji kuendelea kubaki Camp Nou. 

Jana jumatatu iliripotiwa kwamba United walituma ofa ya kwanza ya kiasi cha £25.9 million  kwa ajili ya kumsajili Fabregas, ambaye amefeli kupata nafasi katika kikosi cha kwanza tangu aliporudi akitokea Arsenal.
Lakini akiongea na waandishi wa habari leo mchana, Vilanova amesema wazi kwamba Fabregas bado anataka kubaki kwenye klabu yake hiyo ya utotoni, na hana mawazo ya kuondoka kwa sasa.
 "Ninafahamu kwamba tumepokea ofa kadhaa kutoka kwa vilabu tofauti. Niliongea na Cesc na ameniambia kwamba anataka kubaki.
"Cesc hana mawazo ya kuondoka kwenda klabu nyingine. Anajua ushindani ni mkubwa hapa na ana ndoto za kuendelea kuwa hapa na kufanikiwa.


No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...