facebook likes

Thursday, June 27, 2013

UCHAMBUZI FEKI WA VICHWA VYA MAGAZETI YA LEO


 JAMANI serikali iwage na huruma nyeee. Yaani huyu binti mdogo namna hii yenyewe inamkalia kooni si atashindwa kupumua? Kiukweli nawashauri wabunge ambao ni muhimili mwingine waitoe serikali shingoni kwa Aunt wetu, bado tunamhitaji kwanza kaolewa juzijuzi tu halafu nyie mnamkalia shingoni, Not fea washkaji not fea

Yanga kiboko, hii triki lazima na Man U na timu nyingine wajifunze, kamata fowadi wa timu pinzani halafu unamficha, unakuwa umekata kabisa jeuri yao. Mechi ikianza fowadi hayupo, au ili utamu uzidi unamficha na kipa, mechi pyeee timu haina kipa shenzi zao, hapo ni mabao utadhani unacheza na Tahiti. Hongera Yanga kwa ubunifu.

 Blog hii imeshalalamika sana kitendo cha nchi moja kuiuwa nyingine. Sasa hapa itakuwaje? Ningeshauri Tahiti ijitoe muhanga na kwenda kuamulia sekeseke hili, nchi ikifa wananchi wake wanaenda wapi? Wasije wakawa wakimbizi Bongo maana ndio kituo kikubwa cha wakimbizi. Umoja wa Mataifa amka mambo yanaharibika huku

 Tunapinga hiki kichwa kwa nguvu zote. Sisi huku Manzese na Tandale hatukubali kutekwa tutafait mpaka mwisho, hayo mambo ya hukohuko kwenu Maostabe, Ma sijui Masaki, sisi hatutekwi , wajumbe wetu wa serikali za mtaa watabaki walewale. Habari ndio hiyooo. HATEKWI MTU HAPA

Mmesikia nyie wakuja, tumejaa huku, msijeeee, atakaebisha amri halali si mnajua maelekezo yaliyotolewa wiki iliyopita? Tusije kulaumiana ohoo, Msiije mpaka Bosi aondoke


DUH Yanga ndio sisi mnuso sio ishu hatutakiiii, na wala hilo pilau hatuliii, kawapeni jamaa zetu sisi hatuna dhiki. Yanga Hoyeeee




thanks to JOHN KITIME

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...