facebook likes

Tuesday, August 13, 2013

Rais Jonathan: Waislamu hawabaguliwi Nigeria


Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria
Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria amesema kuwa, Waislamu nchini humo hawabaguliwi na kwamba serikali inaamiliana nao kama ilivyo kwa raia wa dini nyingine.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
.......SOMA ZAIDI.....
Taarifa ya ikulu ya Rais iliyotolewa kwa vyombo vya habari na msemaji wa Rais imekanusha tuhuma za kuweko muamala wa kibaguzi unaofanywa na Rais wa nchi hiyo dhidi ya Waislamu.

Reuben Abati, msemaji wa Rais Goodluck Jonathan amebainisha kwamba, serikali ya Rais Jonathan haiamiliani na raia wa nchi hiyo kwa misingi ya dini na kwamba, tuhuma za kufanywa ubaguzi dhidi ya Waislamu hazina ukweli wowote.

Wakati serikali ikitoa taarifa ya kukanusha madai hayo, wapinzani wameendelea kusitiza kwamba, Waislamu nchini Nigeria wanabaguliwa.

Nassir Rafai, kiongozi wa chama cha upinzani cha All Nigeria Peoples Party amesisitiza kwamba, rais Jonathan amekuwa akiamiliana na wananchi wa nchi hiyo kwa misingi ya kidini na ukabila. Waislamu nchini Nigeria wanaunda asilimia 62 ya wakazi milioni 170 wa nchi hiyo.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...