facebook likes

Monday, July 8, 2013

Historia yatengenezwa kwenye fainali ya Wimbledon Tenis.

Mwanadada toka UFaransa Marion Baroli ameweka historia ya kuwa mwanamke wa 18 kutwaa ubingwa wa michuano ya tenis ya Wimbledon akimshinda Mjerumani Sabine Liscki .
Bartoli ambaye alishinda kwa seti mbili bila majibu akishinda kwa michezo 6-1 na 6-4 aliweka historia nyingine ya kuwa mwanamke pekee kutwaa ubingwa wa Wimbledon bila kucheza na mchezaji aliyeko kwenye top 10 ya viwango vya Ubora duniani Huku pia akiwa mchezaji wa kwanza ambaye hayuko kwenye top 10 kutwaa ubingwa katika historia ya michuano hiyo.
Sabine Licki alionekana kuzidiwa tangu mapema kiasi cha kuanza kububujikwa machozi kabla ya mchezo kuisha hali iliyomfanya apoteze mwelekeo na kupoteza mchezo huo. Mwanadada huyo ameondoka na kitita cha dola milioni 1.6 kama zawadi ya kutwaa ubingwa huo .
Fainali hiyo kwa upande wa wanaume itafanyika hapo kesho ambapo Andy Murray wa Scotland atacheza na Novak Djokovic wa Serbia .

Marion Bartoli akionyesha Taji lake.
Marion Bartoli akionyesha Taji lake.
Sabine Licki alishindwa kuzuia machozi kwenye seti ya pili.
Sabine Licki alishindwa kuzuia machozi kwenye seti ya pili.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...