facebook likes

Wednesday, July 10, 2013

Matatu za Kenya a.k.a daladala zimekuja na ubunifu wa huduma mpya aisee


Nairobi - Kenya - East Africa
Ukiwa kwenye jiji la Nairobi na ukaona magari yamechorwa rangi tofauti na graffiti, basi hizo ni daladala zao jijini Nairobi maarufu kama Matatu ambapo sasa hivi wamiliki wake wamekuja na ubunifu mpya ambao unawasaidia katika kufanya biashara zaidi na kuvutia wateja wengi sana.
Mtu wangu wa nguvu najua internet ni moja kati ya huduma unazotumia kila  siku na imekuwa inatumika kama kivutio cha biashara pia kwenye sehemu kadhaa ya biashara kama kwenye migahawa, Bar au Night club kwenye nchi zilizoendelea utakutana na internet ya bure kupitia WiFi. Basi wenzetu wa 254 Kenya wameanza kupiga hatua mbele kwenye kitu hiki baada ya matatu zao kuanza kutoa free internet kwa kutumia WiFi. fikiria na foleni hizi zilizopo Dar kama daladala zingekua na internet ya bure ndani yake watu wasingeuona ukali wa foleni kabisa… bila kusahau uhakika wa kufanya biashara ungeongezeka kwa sababu watu wengine wangechagua daladala zenye internet yenye speed. ukiwa katika jiji la Nairobi na simu yako ikiwa ina support WiFi, ukipanda matatu ni kama upo nyumbani au kazini. abiri wengi hivi sasa hutumia muda wa asubuhi kuelekea ofisini huku wakiangalia habari mbalimbali kwenye simu zao na kupitia mitandao ya kijamii..
Hivi sasa makonda wa matatuu wanaita abiria kwa kuongezea kionjo cha internet ya bure ipo, kwa mfano hata Dar kungekua na hiyo huduma ungemsikia konda tu anasema “Kariakoo Sokoni hiyoo mia nne na internet yenye kasi bureee”

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...