
Dogo noma: Frazier Campbell amefunga mabao mawili Cardiff ikiibwaga Manchester City
MABAO mawili ya kichwa dakika za lala salama ya Fraizer Campbell tyameipa Cardiff ushindi wa kwanza katika Ligi Kuu ya England, baada ya kuilaza Manchester City 3-2.
Edin Dzeko alitangulia kuifungia timu ya Manuel Pellegrini dakika ya 52, lakini Cardiff ikasawazisha kupitia kwa Aron Gunnarsson dakika ya 60, kabla ya Campbell kufunga dakika za 79 na 87.
Alvaro Negredo akafungua akaunti yake ya mabao City kwa bao la dakika ya mwisho kabisa.
Kikosi cha Cardiff City kilikuwa: Marshall; Connolly, Caulker, Turner, Taylor, Bellamy/Cowie dk83, Gunnarsson, Kim/Mutch dk90, Medel, Whittingham na Campbell/Cornelius dk90.
Manchester City: Hart, Zabaleta, Garcia, Lescott, Clichy, Navas/Nasri dk55, Fernandinho/Milner dk77, Toure, Silva, Aguero na Dzeko/Negredo dk69.

Shuti hadi bao: Edin Dzeko akifunga

Kifaa: Fraizer Campbell akimruka kipa wa City, Joe Hart
Hapa ni namna Alvaro Negredo alivyoifungia Manchester City bao la pili - Gonga hapa kupata zaidi yaliyojiri Uwanja wa Cardiff City


Mpambano kwenye kiungo: Kiuno wa Cardiff, Gary Medel akipambana na kiungo wa City, Fernandinho

Kizaazaa: Mabeki wa City wakiwa wameduwaa baada ya Aron Gunnarsson kusawazisha

Amepagawa: Sergio Aguero haamini kipigo

Shujaa: Fraizer Campbell ameing'arisha timu mpya katika Ligi Kuu

Hatari: Alvaro Negredo alifunga dakika ya mwisho

Wakati wa kusherehekea: Mashabiki wa Cardiff wakishangilia bao la Campbell

Majanga: Alvaro Negredo akisikitika chini

Kipa bomu: Joe Hart ameonyesha tena hayuko katika kiwango kizuri

Shujaa wa United? Campbell ametokea kwenye akademi ya Old Trafford
No comments:
Post a Comment