facebook likes

Monday, August 26, 2013

BILA MESSI, BARCA YAPATA USHINDI MWEMBAMBA LA LIGA, ILA NEYMAR ADHIHIRISHA

Youngster: £50million man Neymar came on in the second-half an upped the tempo for Barcelona

Nyota kinda: Mchezaji mwenye thamani ya Pauni Milioni 50, Neymar aliingia kipindi cha pili na kufanya vizuri
SOMA NA ANGALIA PICHA ZAIDI....
KLABU ya Barcelona imepata ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Malaga jana na kuendeleza mwanzo wao mzuri katika mbio za kutetea taji lao la La Liga.
Mabingwa hao walimkosa majeruhi Lionel Messi na ilisota kupata bao hilo pekee hadi beki wa pembeni Adriano alipokatiza upandd wa kulia kuingia ndani kabla ya kufumua shuti kali lililotinga nyavuni kabla ya mapumziko.
Mshambuliaji Mbrazil, Neymar aliingia kipindi cha pili na kuonyesha alistahili kuigharimu Barca Pauni Milioni 50.

Difference: Adriano celebrates with his Barcelona team-mates after scoring
Tofauti: Adriano akishangilia na wachezaji wenzake wa Barcelona  baada ya kufunga
Pants up: Malaga's Sergio Sanchez shows his annoyance when his side missed a glorious chance
Hasira: Sergio Sanchez wa Malaga akionyesha hasira zake baada ya timu yake kukosa bao la wazi
Speed: Barcelona's Alexis Sanchez runs away from Malaga's Vitorino Antunes
Kasi: Alexis Sanchez wa Barca akimtoka Vitorino Antunes wa Malaga
Physical: Malaga's defender Jesus Gamez gets a yellow card for ruthlessly blocking off Neymar
Kazi kazi: Beki wa Malaga, Jesus Gamez alipewa kadi ya njano kwa kumchezea rafu Neymar
Wry smile: Gerardo Martino looks on after as his side win their second La Liga match
Tabasamu: Gerardo Martino baada ya ushindi jana

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...