facebook likes

Thursday, July 18, 2013

SERIKALI YAOMBA WANANCHI KUSHIRIKI KATIKA ULINZI WA RASILIMALI NCHINI.



Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na 
“Wizara inaomba sote tuitafakari na kuitekeleza dhana ya Jeshi la Polisi 
ya Ulinzi Shirikishi ni muhimu kila mwananchi mzalendo wa nchi hii ashiriki kikamilifu kudumisha amani na ulinzi wa nchi na rasilimali zake zote”Alisema Yustina. 
Aidha Yustina alisema ulindaji wa rasilimali hizo hasa wanyama pori utasaidia kujenga na kuimarisha utalii wa nchi kutokana na zaidi ya asilimia 90 utalii unategemea wanyamapori na hivyo kuingizia nchi fedha za kigeni na pia kukuza uchumi.”Kwa hapa nchini zaidi ya asilimia 90 ya utalii unategemea wanyama pori hivyo, watalii wengi huja kuwaona, kuwapiga picha na kuondoka wachache huja kuwawinda kisheria na kuchukua nyara. Wanyamapori ndio wamebeba utalii katika Tanzania na kwa maana hiyo ndio, kwa kiasi kikubwa, wamebeba uchumi wa nchi hii” Alisema Yustina. 
Naye Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Kuzuia Ujangili kutoka wizara hiyo  Bw. John Muya aliwataka wananchi waliokatazwa kuishi maeneo ya njia za wanyama kutekeleza agizo hilo ili kuepuka uharibifu unaofanywa na wanyama hao kipindi cha uhamiaji.“Napenda kutoa wito kwa wananchi kuondoka kwenye yale maeneo ambayo ni mapito ya wanyama pindi wanapohama kuondoka ili kuondoa usumbufu na uharibifu wa mali” Alisema Muya.  
Yustina aliwataka wananchi kuacha kuwatazama baadhi ya wanyama kama Fisi na Tembo kama kero kwa wananchi, badala yake tuwatazame wanyamapori kama benki kubwa na kama mkombozi wa nchi yetu kiuchumi.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...