facebook likes

Thursday, February 7, 2013

UINGEREZA YAFUTA UTEJA WA MIAKA 23 KWA BRAZIL


ROO BEAUTY ... Wayne Rooney celebrates his goal
UINGEREZA jana usiku ilifanikiwa kupata ushindi wa kwanza dhidi ya Brazil tangu mwaka 1990 kufuatia ushindi wa mabao 2-1 ndani ya dimba la Wembley yaliyofungwa na Wayne Rooney na Frank Lampard.
Ikiwa ni mechi maalum ya kusherehekea miaka 150 ya chama cha soka Uingereza (FA), iliwachukua wenyeji dakika 26 kupata bao la kuongoza kupitia kwa Wayne Rooney baada ya kipa Julio Cesar kuutema mkwaju wa chini wa Theo Walcott.
WAYNE TO GO ... Wayne Rooney scores the opener for England
Rooney akipiga bao la kwanza
Brazil wangeweza kuongoza mapema baada ya refa Pedro Proenca wa Ureno kuwazawadia penalti dakika ya 19 kufuatia kiungo Jack Wilshere kuunawa mpiria wa krosi ya Ronaldinho.
Lakini Ronaldinho, Supa staa wa zamani wa Barcelona, alishuhudia mkwaju wake wa penalti ukiokolewa na kipa Joe Hart.
HART STOPPER ... Joe Hart saves Ronaldinho's penalty
Ronaldinho akikosa penalti
Kocha Hudgson wa Uingereza alifanya mabadiliko mawili wakati wa mapumziko kwa kuwatoa Tom Cleverley aliyempisha Lampard na Ashley Cole aliyepokelewa na Leighton Baines.
Lakini ni mabadiliko ya Brazil ndio yaliyoanza kuzaa matunda baada ya mcheaji aliyetokea benchi, Fred kuwasawazishia wageni dakika ya 49 kufuatia uzembe wa beki Gary Cahill aliyeshindwa kuumiliki vizuri mpira mbele ya Luis Fabiano.
Frank Lampard akaibuka shujaa kwa bao lake la dakika ya 60 kufuatia pasi ya Wayne Rooney.
Hii inakuwa ni mara ya kwanza kwa England kupata mabao mawili dhidi ya Brazil tangu mwaka 1984 iliyoshuhudia bao la kukumbukwa la John Barnes.
Katika mechi ya jana, Ronaldinho alizawadiwa jezi maalum ya kutimiza kwake mechi 100 katika timu ya taifa huku Steven Gerrard naye akikabidhiwa tuzo ya dhahabu na kipa wa zamani Peter Shilton kwa kutimiza mechi 101.
RON IN A MILLION ... Ronaldinho receives a special shirt to mark his 100th cap
Ronaldinho akipokea zawadi ya kutimiza mechi 100
STEVIE GLEE ... Steven Gerrard receives his 100th England cap from Peter Shilton
Gerrard  akipokea zawadi ya kutimiza mechi 100
Katika mechi nyingine kubwa za kirafiki zilizochezwa jana, Ujerumani iliichapa Ufaransa 2-1, Argentina ikashinda 3-2 dhidi ya Sweden, Uholanzi wakatoka 1-1 na Italia huku Hispania ikiichabanga Uruguay 3-1.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...