facebook likes

Wednesday, October 9, 2013

WATUHUMIWA WAWILI WA WIZI...MMOJA AKIWA NA KITAMBULISHO CA USALAMA WA TAIFA WAKAMATWA USIKU KAWE

Watu wawili wanaotuhumiwa kuwa ni wezi a.k.a Wapigaji/Matapeli wamekamatwa usiku huu kwenye hoteli ya Picolo,Kawe jijini Dar es Salaam.
SOMA NA ANGALIA PICHA ZAIDI...
Watu hao ambao wamekamatwa ni Bw. Takula Mayenga mkazi wa Mbezi Temboni na Bw. Juma Hamis ambaye ni mkazi wa Tabata wakiwa na nyaraka tofauti ikiwemo kitambulisho kinachotaja kuwa ni cha Idara ya Usalama wa Taifa, kadi za benki pamoja na simu zaidi ya kumi,wakiwa katika harakati za kumtapeli mwanadada mmoja aliejitambulisha kwa jina la Rebecca ambaye ni Mwanafunzi wa Chuo cha Biashara cha CBE,Mkazi wa Mbezi Beach jijini Dar es Salaa  .

Akisimulia tukio dada huyo ambaye alipatwa na tukio hilo la kutapeliwa Ijumaa ya wiki iliyopita alisema kuwa, ilikuwa ni Ijumaa iliyopita wakiwa wamekaa katika fukwe wakipunga upepo ndipo alipokuja tapeli huyo na kukaa nao na baadae aliwawekea madawa ya kulevya na kuondoka na dada huyo kwenda kumtupa baharini.
 Kava ya nje ya Kitambulisho hicho kinaonekana namna hii.
 Watuhumiwa hao wakiwa chini ya Ulinzi wa Polisi.
 Kitambulisho hicho kinavyoonekana kwa nyuma.
 Mtuhumiwa wa Uwizi aliejitambulisha kwa jina la Juma Hamis huku akiwa na Kitambulisho cha Kazi cha Idara ya Usalama wa Taifa chenye jina la Kenedy Magige.
 Mtuhumiwa mwenza wa Tukio hilo la Wizi,aliejitambulisha kwa jina la Takula Manyenga mwenye umri wa Miaka 28,akidhibitiwa kwa kufungwa kamba mara baada ya kukamatwa Usiku huu kwenye Hoteli ya Picolo,Kawe jijini Dar es Salaam.
 Watuhumiwa wote wawili wakipakiwa ndani ya Gari la Polisi kutoka katika Kituo cha Kawe,Jijini Dar es Salaam.
 Askari Polisi wakiwa eneo la tukuo kuhakikisha Usalama unapatikana eneo hilo.
 Askari Polisi wakiwa na Watuhumiwa hao wakati wakiendelea na Ukaguzi ndani ya Gari hilo aina ya Toyota Prado lenye nambari za Usajili T 445 BCY.
 Askari Polisi wakiendelea na Ukaguzi ndani ya Gari hilo,ambapo ndani ya Gari hilo kulikutwa na Simu zaidi ya kumi ambazo zilichukuliwa na Polisi hao.
 Gari walilokuwa wakilitumia Watuhumiwa hao.
 
 Ulinzi mkali kwa watuhumiwa hao.

Msafara wa kuelekea kituoni.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...