facebook likes

Thursday, October 10, 2013

STEPHEN WASIRA "SINA UFUNGUO WA IKULU, SIWEZI MCHAGULIA RAIS NANI WA KUONANA NAYE"

*Asema hampangii Rais nani aonane naye
*Mtikisiko mkubwa watarajiwa bungeni Dodoma
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu), Stephen Wasira, amesema hana mamlaka ya kumchangulia Rais nani akutane naye.
SOMA ZAIDI.......


Alitoa kauli hiyo katika mahojiano na Rai yaliyofanyika Jumanne wiki hii ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam kuhusu hali ya siasa nchini katika kipindi ambacho umma wa Watanzania unasubiri kusainiwa kwa Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete.

“Taarifa kwamba naweza kumwambia Rais Kikwete aonane na huyu au asionane na yule si za kweli, Rais ana mamlaka yake, ana ofisi yake binafsi, pia yeye ni kama baba hivyo mtu yoyote bila kujali itikadi ana haki ya kuonana na Rais.

 “Ninachofahamu muswada ukija Rais atasaini kwa sababu taratibu na kanuni zote zimefuatwa, lakini kama wenzetu wanahitaji kumuona Rais ni sawa, na amesikia wito na amekubali. Tusubiri matokeo ya mazungumzo,” alisema.

No comments:

COMMENTS

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...